Mwanamama anayeitwa Pili aliyeishi kama mwanaume kwa miaka 30

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Jana nilikuwa na shost akanionyesha habari inato twmbea mitandaoni.

Ni mwanamama anaeitwa Pili, alitafuta kazi Mirerani Arusha na alifahamishwa kuwa wao hutoa ajira kwa wanaume tu. Aliamua kuanza kuvaa kiume na kujipa jina la kiume, alifanikiwa kupata ajira.

Wafanya kazi wenzako wote walikuwa wanaume, alikunywa nao pombe na kutaniana nao pasi wao kufahamu jinsi a yake kwa miaka mingi.

Ilitokea tukio la ubakaji, mmbakaji alimsinguzia Pili kuwa ndiye aliyefanya tukio lile. Pili alichukuliwa na polisi na kufika kuthibitisha ilibidi ajieleze kuepuka kuwekewa mahabusu ya wanaume.

Kuna mliyoisikia habari hii?
 
Tuwekee picha yake tafadhali! Tutajua mbivu na mbichi. Miaka 30 bila kushtukiwa!? Aligiza hadi sauti? Au alikua na besi kama wanaume? Umbile lake je? Lilikaa kiume sana? Tunakaa na mwenzetu miaka30 tunakunywa naye pombe lkn hatumjui demu wake nani? Hate zile chapa ilale pia? Alikua analala peke yake? Kama hilo eneo ni wanaume watupu lazima itakuwa hapauzwi pedi..! Alijistiri vipi kwa miaka yote 30!? Au alikua akienda kununua mbali halafu anazificha? Naamin huwezi kukuta kanga maeneo ya wanaume watupu.
 
Anaitwa UNCLE PILI huyo,kwa sasa anamiliki mgodi wake pale Mirerani.

Ameajiri wafanyakazi zaidi ya 50 lkn katika hao wanawake ni wa 2 tu tena kwa ajili shughuli nyepesi kama upishi.
 
Anasema khs pedi sijui alikua anatumia pamba na gozi hapo sielewi wanawake watasaidia.

Na alikua akiwa kwenye siku zake anaamua kuwa mpishi wa chakula kwa "manyokaa" haingii underground kuchimba.
 
Huyo mama yupo na anamiliki mgodi wa Tanzanite ila historia yake siifahamu kivile coz mm nimemfahamu miaka ya karibuni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…