Mama mmoja anayeishi huko kibaha na alikuwa mwalimu wa shule ya msingi na mlokole wa kanisa la kilokole picha ya ndege amefariki baada ya kutembea na rafiki wa mumewe.
jamani tego zingine mbaya kabisa.ni lini wake zetu watatulia?
[/QUOTE]
Hivi kwa nini kila kosa la zinaa linamwendea mwanamke na hali mwanaume ndiye huwa mwanzilishi????
Tukijifanya hatujui chanzo cha tatizo/au kurushiana lawama basi kamwe hatutatua tatizo na ukimwi utaendelea kutufagia. Nimesema hivyo kwa sababu hizi:
1. Tunalia na madangulo lakini Mteja Mkubwa wa hili soko ni wanaume (shame on you!);
2. Huyo mwanamke wa mtu aliyekufa baada ya ngono alikuwa anafanya ngono na nani🙄, siyo mme wa mtu huyo???
3. Mara zote mume akishikwa ugoni, basi aibu ni ya mwanamke, why???
4. Akifuatwa kimada kuonywa aache tabia yake, atakujibu huyo mumeo ananifuata mwenyewe, tena kwa maringo makuuu anakujibu "Mfungie mumeo ndani"
Myanaume imekuwa kama mizumbukuu, inapelekwa tu, halafu ndo yenyewe ya kwanza kulaumu wanawake! syeeeee!!!
R.I.P mama.
Mhh Sitaki kujibishana na wewe ChaMtuKinyesi, ila hoja yako ni kutaka kutulaumu wanaume. Mimi simlaumu yoyote kwa sababu Bible inasema wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu, pindi tunapomkosa Mungu yatupasa tutubu na kuomba neema yake kila wakati. Hii ya kunyoosheana vidole ndio iliyoleta kifo juu ya uso wa nchi. Adam na Eve walipofakamia tundi, Bwana Mungu alipomuuliza Adam inakuaje amikuli tundi alichojibu sio mimi ni huyu mwanamke uliyenipa, na Eve alipoulizwa akajibu sio mimi ni nyoka, ikapitishwa adhabu kwa wana wote wa Adam, mpaka nyoka nae, while Adam angeomba msamaha Mungu ni mwenye huruma angemsamehe, sasa sio namlaumu Adam bali naonyesha jinsi gani sisi binAdam tulivyo wadhaifu. Mungu atupe neema yake ya kujua lipi litupasalo kutenda. Huyo mama kamaliza safari yake hata tumseme mpaka mishipa ya shingo ikakamae haibadilishi kitu,hatujui hukumu yake na sisi sio MaJudge.