TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,763
- 11,873
Mwanamke mmoja mrembo wa nchini Urusi ambaye alikuwa akiwabaka wanaume walioingia nyumbani kwake amekamatwa baada ya kuwabaka jumla ya wanaume 10.
Mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina la Valeria K, mwenye umri wa miaka 32 anatuhumiwa kuwabaka wanaume 10 baada ya kuwalewesha kwa kuwapa vinywaji ambavyo aliviwekea madawa ya kuleta usingizi.
Mwanamke huyo amefananishwa na buibui jike mweusi anayejulikana kama "Buibui Mjane" ambaye huwaua na kuwatafuna buibui wanaume baada ya kujamiana nao.
Polisi wa Urusi walisema kwamba Valeria ambaye ni mrembo wa kuvutia kwa wanaume wengi huwashawishi wanaume waingie nyumbani kwake na baadae kuwapa vinywaji ambavyo aliviwekea madawa ya clonidine.
Madawa hayo ya Clonidine huwafanya wanaume hao wawe hawajitambui kwa masaa 24.
waendesha mashtaka waliiambia mahakama kwamba baada ya hapo Valeria huwavua nguo zote wanaume hao na kuwabaka.
Mwanamke huyo anayependa kuangalia filamu za kutisha anatuhumiwa pia kuzungushia kamba kwenye nyeti za wanaume anaowabaka ili kuzifanya ziwe kama zimesimama.
Polisi walisema kwamba wanaume wote waliobakwa na mwanamke huyo walizinduka wakiwa hospitalini wakiwa na maumivu makali kwenye nyeti zao.
Polisi walipata tabu kumkamata mwanamke huyo kwani wanaume waliobakwa na mwanamke huyo walikuwa hawakumbuki chochote zaidi ya kukumbuka kwamba walikutana na mwanamke mrembo aliyewapa kinywaji.
Maafisa wa polisi walifanikiwa kumgundua hivi karibuni wakati akiwa tayari ameishawabaka wanaume 10 katika siku tofauti tofauti.
Ni mwanaume mmoja kati ya hao kumi ndiye aliyeamua kumfungulia mashtaka mwanamke huyo.
Mwanaume mmoja ambaye yeye hajaamua kumchukulia mwanamke huyo hatua yoyote alisema kwamba yeye alifurahia kitendo hicho.
"Ulikuwa wakati mzuri sana kwangu, Napenda wanawake warembo natamani kama asingeniwekea madawa ya Clonidine" alisema mwanaume huyo ambaye hakupenda jina lake litajwe.
Source: Nifahamishe
Mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina la Valeria K, mwenye umri wa miaka 32 anatuhumiwa kuwabaka wanaume 10 baada ya kuwalewesha kwa kuwapa vinywaji ambavyo aliviwekea madawa ya kuleta usingizi.
Mwanamke huyo amefananishwa na buibui jike mweusi anayejulikana kama "Buibui Mjane" ambaye huwaua na kuwatafuna buibui wanaume baada ya kujamiana nao.
Polisi wa Urusi walisema kwamba Valeria ambaye ni mrembo wa kuvutia kwa wanaume wengi huwashawishi wanaume waingie nyumbani kwake na baadae kuwapa vinywaji ambavyo aliviwekea madawa ya clonidine.
Madawa hayo ya Clonidine huwafanya wanaume hao wawe hawajitambui kwa masaa 24.
waendesha mashtaka waliiambia mahakama kwamba baada ya hapo Valeria huwavua nguo zote wanaume hao na kuwabaka.
Mwanamke huyo anayependa kuangalia filamu za kutisha anatuhumiwa pia kuzungushia kamba kwenye nyeti za wanaume anaowabaka ili kuzifanya ziwe kama zimesimama.
Polisi walisema kwamba wanaume wote waliobakwa na mwanamke huyo walizinduka wakiwa hospitalini wakiwa na maumivu makali kwenye nyeti zao.
Polisi walipata tabu kumkamata mwanamke huyo kwani wanaume waliobakwa na mwanamke huyo walikuwa hawakumbuki chochote zaidi ya kukumbuka kwamba walikutana na mwanamke mrembo aliyewapa kinywaji.
Maafisa wa polisi walifanikiwa kumgundua hivi karibuni wakati akiwa tayari ameishawabaka wanaume 10 katika siku tofauti tofauti.
Ni mwanaume mmoja kati ya hao kumi ndiye aliyeamua kumfungulia mashtaka mwanamke huyo.
Mwanaume mmoja ambaye yeye hajaamua kumchukulia mwanamke huyo hatua yoyote alisema kwamba yeye alifurahia kitendo hicho.
"Ulikuwa wakati mzuri sana kwangu, Napenda wanawake warembo natamani kama asingeniwekea madawa ya Clonidine" alisema mwanaume huyo ambaye hakupenda jina lake litajwe.
Source: Nifahamishe