Mwanamke aliyebakwa siku ya harusi yake Kenya

Mwanamke aliyebakwa siku ya harusi yake Kenya

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Wakati Terry Gobanga, wakati huo akiitwa Terry Apudo alipotoweka katika harusi yake hakuna mtu aliyedhani kwamba alitekwa nyara ,kubakwa na kutuwa kandakando ya barabara akipigania uhai.

Lilikuwa janga la kwanza kati ya mawili kumkabili muhubiri huyo kijana.
Lakini ni manusura.Harusi iliopangwa ilitarajiwa kuwa harusi kubwa.
Nilikuwa muhubiri hivyobasi wanachama wote wa kanisa walitarajiwa kuhudhuria.

Mchumba wangu ,Harry na mimi tulikuwa na furaha tulikuwa tunafunga ndoa katika kanisa la All Saints Cathedral mjini Nairobi na nilikuwa nimekodisha rinda zuri sana la harusi.
Lakini usiku kabla ya ndoa yetu ,niligundua kwamba nina baadhi ya nguo za Harry .

Hakuweza kuja katika harusi bila tai kwa hivyo rafiki yangu mmoja ambaye alikuwa amekubali kubaki nami usiku wa kuamkia harusi alikubali kumpelekea mapema alfajiri.

_96745526_terrygobanga.jpg

Niliamka mapema na kumpeleka hadi katika kituo cha kupanda basi.
Nilipokuwa nikirudi nyumbani ,nilipita karibu na mtu mmoja ambaye alikuwa ameketi kati boneti ya gari na akanishika kutoka nyuma na kuniingiza katika viti vya nyuma vya gari hilo na kuondoka mahali hapo.

Yote haya yalifanyika katika chini ya sekunde moja. Nilifunguliwa mdomo na kuwekwa kipande cha nguo mdomoni. Nilikuwa nikirusha mikono na miguu nikitaka kupiga kelele. Nilipofanikiwa kutoa kitambara hicho nilipiga kelele: Ni siku yangu ya harusi! hapo ndipo nilipopigwa ngumi .

Mmoja ya wanaume hao wakaniambia nishirikiane nao ama niuwawe. Wanaume hao walinibaka kwa zamu. Nilihisi nitafariki,lakini bado niliendelea kupigania uhai wangu,hivyo basi mtu mmoja alipotoa kitambara kilichokuwa mdomoni mwangu nilimuuma uume wake.

Alipiga kelele kwa uchungu na mmoja wao akanidunga kisu tumboni.
Baadaye walifungua mlango na kunitupa kando ya barabara huku gari likiendelea kwenda.Nilikuwa mbali na nyumbani, nje ya jiji la Nairobi .

Ilikuwa zaidi ya saa sita baada ya kutekwa. Mtoto mmoja aliniona nikirushwa nje ya gari na akamweleza bibiye. Watu walikuja mbio. Wakati maafisa wa polisi walipokuja walijaribu kuangalia iwapo bado ninapumua, lakini hawakupata.

Wakifikiri nimefariki walinitia katika blanketi na kuanza kunipeleka katika chumba cha kuhifadhi maiti. Lakini njiani nilikohowa.Polisi mmoja alisema: Bado hajafariki, hivyo basi wakabadilisha njia ya kuelekea katika chumba cha kuhifadhi maiti na kunipelekea katika hospitali kuu ya serikali nchini Kenya.

Niliwasili nikiwa na mshangao mkubwa, nikizungumza mambo nisioelewa.Nilikuwa nusu uchi nikivuja damu huku sura yangu ikiwa na majeraha kutokana na kipigo nilichopata.

Lakini kuna kitu kimoja kilichomshtua mwanamke aliyekuwa akisimamia matibabu ,kwa sababu aligundua mimi ni bibi harusi. ''Twendeni kanisani tuone iwapo wanamkosa bibi harusi'', aliambia wauguzi.

Kwa bahati kanisa la kwanza waliloulizia ni All Saints Cathedral jijini nairobi ambapo waliambiwa kwamba kulikuwa na harusi mwendo wa saa nne Asubuhi lakini bibi harusi hakuonekana.


bbc swahili
 
BBC ndio wameandika kiswahili hovyo namna hii? Shame
 
Uzembe bibi harusi gani anazungukwa na mtu mmoja tu, anatembea peke yake sijui mpaka kituoni na inaleta picha kama vile eneo halikuwa na watu vile, tena mpendwa, hao wapambe wadada walikuwa wapi, ukikosa maarifa utaangamia halafu utamlaumu MUNGU bure tu, stupid!
 
Ni wao,vipi ni maeneo yapi wamebananga kiswahili,ainisha
"Wakati Terry Gobanga, wakati huo akiitwa Terry Apudo alipotoweka katika harusi yake hakuna mtu aliyedhani kwamba alitekwa nyara ,kubakwa na kutuwa kandakando ya barabara akipigania uhai."
(Lilikuwa janga la kwanza kati ya mawili kumkabili muhubiri huyo kijana) sasa hapa alietekwa ni muhubiri kijana au bibi harusi? kifupi niseme wameandika habari hovyo hovyo au alieileta hapa kakopi vibaya.
 
"Wakati Terry Gobanga, wakati huo akiitwa Terry Apudo alipotoweka katika harusi yake hakuna mtu aliyedhani kwamba alitekwa nyara ,kubakwa na kutuwa kandakando ya barabara akipigania uhai."
(Lilikuwa janga la kwanza kati ya mawili kumkabili muhubiri huyo kijana) sasa hapa alietekwa ni muhubiri kijana au bibi harusi? kifupi niseme wameandika habari hovyo hovyo au alieileta hapa kakopi vibaya.
Mbona inaeleweka sentensi zote za juu zinaelezea mhusika. Katika makala hii wamejitahidi. Kuna makala mengine unakimbia.
 
Yalikua majanga ila jamaa bado alimuoa hata baada ya yote hayo lakini bado akafuatwa na majanga, maana alimpoteza mumewe huyo.
Sasa ameolewa na mume mwengine ambaye tayari wana mtoto.
 
Nimeona hiyo story inasikitisha baadae yule mwanaume akafariki akaonekana ana maana ya mikosi ni ndefu aisee
 
Mmh pole sana kwa yote yaliyokukuta,ila kuelekea harusi ni muhimu maarusi kuwa karibu na watu ndugu,jamaa,marafiki na familia zao ,sio namna ambavyo huyu bibi arusi alikuwa peke yake mitaani.
 
Back
Top Bottom