Pre GE2025 Mwanamke anahaki ya kuongoza taifa hili. Watu waelewe nchi yetu haiongozwi na Dini wala Mila na desturi bali Katiba ya Nchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkûu dunia ya Leo Watu wengi hawaamini kuhusu Mungu.
Pili, hata wanaoamini kuhusu Mungu wanajua kuwa huyohuyo Mungu alitoa Uhuru wa Watu kujichagulia Maisha wayatakayo.

Ndîo maana unaona Mungu haingilii Kesi nyingi zinazoendelea Duniani
 
Tangu uumbaji mwanamke hakuumbwa kama kiongozi, asili inapinga. ASILI ina nguvu kuliko haki. Ikiwa haki ni sawa, Kwa nini tusigawane Koo Kwa watoto wanaozaliwa?!

Asili(Mungu) haipingi viumbe weñye utashi kujiamulia mambo wanayoyataka wènyewe.

Ukisoma Torati yôte hakuna sehemu yoyote àmbayo Mwanaume amepewa mamlaka ya Kiuongozi dhidi ya Mwanamke,

Tukirudi Edeni,
Mwanamke alipewa Laana ya kutawaliwa na Mwanaume. Lakini hiyo haipo kiasili.

Sheria za Mungu ndîo zinazotawala. Kwamba Mwanamke na Mwanaume wôte lazima Wazifuate Sheria za Mungu. Kidini.

Mwanamke aliambiwa amtii Mumewe Kwa sababu Mume ndiye alikuwa anajukumu la Kumtunza Mkewe Kwa kumpa mahitaji.

Kihaki, Mtu anayekupa Mahitaji na kukulea unatakiwa umtii.
Tunamtii Mungu Kwa sababu ndiye anayetupa mahitaji anayetulea.

Torati inaamrisha Watu kufanya Kazi lakini haitaji jinsia gàni ifanye Kazi. Hivyo hiyo ni Amri Kwa wôte(Wanaume na Wanawake).

Ikiwa Mwanamke atafanya Kazi na Akawa anajihudumia mwenyewe unafikiri atakuwa na wajibu wa kumheshimu mumewe? Kwa jicho la HAKI?

Au Ikiwa MTU anapata huduma Kutoka Kwa waganga wa kienyeji na Mizimu badala ya kupata mahitaji hayo Kwa Mungu aliyemuumba. Unafikiri Mtu huyo anaowajibu wa Kumtii(kumuabudu) Mungu aliyemuumba? Jibu ni hapana. Hawezi kuwa na huo wajibu.

Ndîo maana kûna Sheria Inasema, usiiabudu mîungu mingine Wala kuitumikia. Kwa sababu ukishataka mahitaji Kutoka Kwa mîungu Wengine automatically Mungu aliyekuumba anakosa Mamlaka juu yako. Na wéwe Huwezi kumuabudu.

Halikadhalika, Mkeo akihudumiwa na Mwanaume Mwingine automatically heshima kwako itashuka Kwa sababu Haki haitakuwa juu yako.
 
Mkûu dunia ya Leo Watu wengi hawaamini kuhusu Mungu.
Pili, hata wanaoamini kuhusu Mungu wanajua kuwa huyohuyo Mungu alitoa Uhuru wa Watu kujichagulia Maisha wayatakayo.

Ndîo maana unaona Mungu haingilii Kesi nyingi zinazoendelea Duniani
Huwezi kukwepa uwepo wake wakati ushahidi upo kila mahali. Hakuna aliyejua kuwa Samia mwaka 2021 angekuwa anaapishwa kuwa RaIS wa sita wa JMT.
 
What none sense is this? Ngoja nihamie zangu Kandahar kwa wanaume wanak jitambua
 
Mmeshinda na hayo mabundiki,hebu kwanza tumuulize sheikh ubwaubwa nasikia kapewa zawadi ya ndinga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…