Mwanamke atekwa na kubakwa siku ya harusi yake Kenya

Mwanamke atekwa na kubakwa siku ya harusi yake Kenya

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253
mwanamke.jpg

Wakati Terry Gobanga, wakati huo akiitwa Terry Apudo alipotoweka katika harusi yake hakuna mtu aliyedhani kwamba alitekwa nyara ,kubakwa na kutupwa kandakando ya barabara akipigania uhai.

Lilikuwa janga la kwanza kati ya mawili kumkabili muhubiri huyo kijana .Lakini ni manusura.

Harusi iliopangwa ilitarajiwa kuwa harusi kubwa.

Nilikuwa muhubiri hivyobasi wanachama wote wa kanisa walitarajiwa kuhudhuria.

Mchumba wangu ,Harry na mimi tulikuwa na furaha tulikuwa tunafunga ndoa katika kanisa la All Saints Cathedral mjini Nairobi na nilikuwa nimekodisha rinda zuri sana la harusi.

Lakini usiku kabla ya ndoa yetu,niligundua kwamba nina baadhi ya nguo za Harry .

Hakuweza kuja katika harusi bila tai kwa hivyo rafiki yangu mmoja ambaye alikuwa amekubali kubaki nami usiku wa kuamkia harusi alikubali kumpelekea mapema alfajiri.

Niliamka mapema na kumpeleka hadi katika kituo cha kupanda basi.

Nilipokuwa nikirudi nyumbani ,nilipita karibu na mtu mmoja ambaye alikuwa ameketi kati boneti ya gari na akanishika kutoka nyuma na kuniingiza katika viti vya nyuma vya gari hilo na kuondoka mahali hapo.

Yote haya yalifanyika katika chini ya sekunde moja .Nilifunguliwa mdomo na kuwekewa kipande cha nguo mdomoni.

Nilikuwa nikirusha mikono na miguu nikitaka kupiga kelele.Nilipofanikiwa kutoa kitambara hicho nilipiga kelele: Ni siku yangu ya harusi! hapo ndipo nilipopigwa ngumi .

Mmoja ya wanaume hao wakaniambia nishirikiane nao ama niuwawe.Wanaume hao walinibaka kwa zamu .

Nilihisi nitafariki ,lakini bado niliendelea kupigania uhai wangu, hivyo basi mtu mmoja alipotoa kitambara kilichokuwa mdomoni mwangu nilimuuma uume wake.

Alipiga kelele kwa uchungu na mmoja wao akanidunga kisu tumboni.

Baadaye walifungua mlango na kunitupa kando ya barabara huku gari likiendelea kwenda.Nilikuwa mbali na nyumbani ,nje ya jiji la Nairobi .

Ilikuwa zaidi ya saa sita baada ya kutekwa.Mtoto mmoja aliniona nikirushwa nje ya gari na akamweleza bibi yake.

Watu walikuja mbio wakati maafisa wa polisi walipokuja walijaribu kuangalia iwapo bado ninapumua ,lakini hawakupata.


Wakifikiri nimefariki walinitia katika blanketi na kuanza kunipeleka katika chumba cha kuhifadhi maiti .

Lakini njiani nilikohowa. Polisi mmoja alisema: Bado hajafariki ,hivyobasi wakabadilisha njia ya kuelekea katika chumba cha kuhifadhi maiti na kunipelekea katika hospitali kuu ya serikali nchini Kenya.

Niliwasili nikiwa na mshangao mkubwa, nikizungumza mambo nisioelewa.Nilikuwa nusu uchi nikivuja damu huku sura yangu ikiwa na majeraha kutokana na kipigo nilichopata.

Lakini kuna kitu kimoja kilichomshtua mwanamke aliyekuwa akisimamia matibabu ,kwa sababu aligundua mimi ni bibi harusi.

''Twendeni kanisani tuone iwapo wanamkosa bibi harusi'', aliwaambia wauguzi.

Kwa bahati kanisa la kwanza waliloulizia ni All Saints Cathedral jijini Nairobi ambapo waliambiwa kwamba kulikuwa na harusi majira ya saa nne Asubuhi lakini bibi harusi hakuonekana.

Chanzo: BBC Swahili
 
Aisee manyang'au yamenisikitisha sana kwa kitendo hiki😱😱😱
 
loh wanaume jamani? sasa aliolewa tena au anatafuta kama mimi bado?
 
Back
Top Bottom