Mwanamke na mwanamme inawezekana wawe na urafiki wakawaida tu ?

Mwanamke na mwanamme inawezekana wawe na urafiki wakawaida tu ?

Haiwezekani. Kama ww ni mwanamke na una rafiki wa kiume basi ujue siku moja lzm atakwambia kitu hicho....
 
Kama mlikua wapenzi penzi likatema na wote mkatambua kua you ar not meant to be wote kimapenzi inawezekana kabisa. Tena you become bffs.
 
hii mada kila mtu atajibu kulingana anavyoishi sasa, wale ambao wamejikusanyia marafiki wa jinsia tofauti watasupport na wale ambao hawaamini katika urafiki wa jinsia tofauti watapinga... mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa kuna uwezekano mdogo sana kutengeneza urafiki wa kawaida kati ya binti na kijana!! mwanzoni watu wanaweza kupretend kuwa wapo kawaida, ila mara zote katikati ya safari mambo hubadilika!! ila pia, inawezekana wewe unauona urafiki huo ni wa kawaida, je wajuaje huyo mwenzio anauona hivyo uuonanyo wewe?
 
inategemeana kama mmoja kati yao anamtaka kimapenzi mwenzake ataanza kumuwekea mitego ya kumnasa hadi atamla ila kama wote wawili hawatakani kimapenzi watakuwa marafiki wa kawaida.
 
Yeah,hii inawezekana sana.Sema inategemea sana na malezi na mazingira uliyokulia.Nachukulia mfano wangu nimekulia kwenye familia kubwa,i mean extended familly,ambapo nimekua na watoto wa kike watatu,wanne,na tulikuwa close sana,nimesoma co-education halafu day.Nimeenda JKT na Chuo ambako ni mchanganyiko na bahati nzuri nilikutana na mdada wakati nipo chuo tukawa kwenye group study moja pia.
Huyu mdada akatokea kuwa rafiki yangu sana,hakuwa na bf na mimi nilikuwa na gf anasoma chuo kingine lakini alikuwa mtu ambae hata love life yangu alikuwa anaijua.Baada ya kumaliza chuo miaka hiyo,tulipangia kazi mikoa tofauti lakini tulikuwa tunatembeleana na alikuwa akija kwangu wakati huo naanza maisha nilikuwa na chumba kimoja "fullsuite",yaani chumba,unapika humo humo,makochi yako humo,yaani kila kitu basi tulikuwa tunalala pamoja,yeye kitandani mimi kwenye kochi
Acha hiyo hata dadangu ninae mfuata ambae kulikuwa close pia wakati naanza maisha alikuwa akinitembelea tulikuwa tunalala chumba kimoja.
Hii nafikiri inategemea kama nilivyosema mwanzo na malezi na mazingira uliyokulia
 
Pitia uzi 'just a friend' wa The Boss nadhani, watu walimwaga mipweint ya kufa mtu hapo.

Ila hii huwa mazingaombwe tu.
 
mi rafiki yangu nilikuwa namwita paka.....yeye akawa ananiita samaki....you know what happened.....?
 
ha ha ha ha, you must be out of your mind.

Samaki alimla paka???

mi rafiki yangu nilikuwa namwita paka.....yeye akawa ananiita samaki....you know what happened.....?
 
Back
Top Bottom