TANZIA Mwanamuziki Adolf Mbinga, aka Chinga One afariki Dunia

Poleni sana wanafamikia ya muziki Tanzania.

Kuna taarifa zinasema marehemu alikuwa anaumwa na akazidiwa akarejeshwa nyumbani.

Ni jambo jema tukafahamu, wasanii wengi wanakuwa wahanga kijamii kwa sababu hakuna sheria nzuri zinazolinda maslahi yao pindi wanapokuwa nje ya game. Wengi wanakufa masikini na dhalili kabisa.

Inawezekana ndugu yetu angepata matibabu sahihi endapo angekikuwa na fedha ya kutosha. Kuna wakati tusimsingizie Mungu kwa mambo yaliyo ndani ya uwezo wetu.

Mungu ampokee mja wake
 
Ni kweli wiki 2 zilizopita alirudishwa kwao kijiji cha mpute nachingwea mkoani lindi akiwa na hali mbaya
 
Ni kweli wiki 2 zilizopita alirudishwa kwao kijiji cha mpute nachingwea mkoani lindi akiwa na hali mbaya
Unaona hii hali inavyokuwa?

Akina Kedmon Mapana wa BASATA wapo bize kufungia fungia nyimbo za wasanii badala ya kuwatafutia maslahi bora

COSOTA wapo bize kurekebisha sheria na kanuni zinazowafavor wao kama watendaji huku wakiacha jukumu la msingi wa kusimamia maslahi ya kiuchumi ya kazi za wasanii..


Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo wapo bize na kukusanya viingilio badalq ya kusimamia maslahi ya wasanii na wanamichezo.

Kimsingi, wapo wasanii nguli wengi wana hali mbaya sana kiuchumi diapite nguvu zao zilizotumika kwa jamii nq serikali. Akina mzee King Kiki bila kufanya show anakufa njaa. Hali ni mbaya.

Halafu utaona viongozi wanajazana kwenye misiba ya wasanii kana kwamba waliwajali enzi za shida zao
 
Kisa cha mpemba.. dah, utunzi mzuri saana.. wimbo umeanza kutiririka kichwani,nimemkumbuka na mwalimu wa walimu, ramadhani masanja.. kwenye aina ya mziki wao, bwana banza kwangu alikuwa hatati zaidi..

Wapumzike kwa amani.
"Upweke huu wa MKE ameutaka mwenyewe nani wa kumlaumu hakuna wa kumlaumu
Analia sana analia sana maamaaa
Unyumba hakuna unyumba hakuna mamaa
Tamaa mbaya tamaa mbaya mamaaa
Analiaaaa saaana" X 2

Hapo dakika ya nne mpk 5 utasikia kisauti furani cha Ramadhani masanja maridadi sana huku sauti ya JESICA CHARLES ikichomoza zaidi ile akitikia kibwagizo analia sana mamaa ikisoka zaidi kupita hata ile ya LUIZA NYONI
 
Ikiisha hapo anakuja mwenyewe fundi anarap.. banza alikuwa na kipaji kikubwa mnoo.
 
Ikiisha hapo anakuja mwenyewe fundi anarap.. banza alikuwa na kipaji kikubwa mnoo.
Yap yap kwanza utaanza kusikia disk za dram zinaanagaika kisha kinakuja kinanda fulani kinapigwa na MIXING kali ya COMPUTER ya mikono ya PRODUCER mkari wa modern DANCE wa muda wote MARONI LINJE
sasa baada hapo anaanza kuwataja wanamuziki wenzie kwa kujianza mwenyewe

"Ebwana masanja piga bao yoooh eeeh piga bao eeeh
Abuu semhando twanga pepeta twange pepeta eeh
Luiza NYONI sina mwana eeh
Jeaca chalee twanga pepeeta"

Huyu jamaa BABAake alikuwa SHEKHE mkubwa na kwa babaake palikuwa na madrsa kubwaa tulikuwa tukienda kwenye ZIARA kwao lakini sasa pameuzwa sijui na madrasa siioni tena
Nahisi pengine alianza kughani na filimbi za NAI madrasa kwao mana alikuwa na kipaji jikubwa cha kuimba na kubuni mitindo ya kusherehesha
zaidi ni vile namna anavyoweza kuibadirisha sauti anavyotaka na ukaipenda
 
Kuna rythim gitaa lilifunika mbaya kwenye wimbo huo, sijui lilipigwa na nani
 
Kuna rythim gitaa lilifunika mbaya kwenye wimbo huo, sijui lilipigwa na nani
Mtunzi wa hiyo nyimbo ambaye ni marehemu na moja ya wahasisi wa TWANGA pepeta
Ukiitaja Twanga pepeta basi lazima umtaje yeye ADORF MBINGA, ROGERT HEGA, LUIZA NYONI,JESCA CHARLES, RAMADHANI MASANJA hao walijitoa sana kuisimamisha TWANGA kiasi kikubwa
Baada kukabidhiwa rasm bendi aiendeshe ASHA hakuwa na pesa kabisa na alikuwa akitegemea mshahara pekee kuiendesha bendi
Hvyo wanamuziki hao walijitoa hata pesa zao kuisimamisha BENDI mpk kuja kutikisa
Ila niliumia sana Mwaka 2001 banza alivyohama. Na kuhamia TOT lkn kumbe ndo ilikuw kumfungulia milango ALI CHOKI aliyeifanya TWANGA PEPETA kwenda NEXT LEVEL kuwa bora zaidi ya BORA

Mpigaji wa GITA matata alikuwa ADOLF MBINGA


Hapo ni ALICHOKI MWIJUMA na KALALA wakiwa LINDI kwenye MAZISHI ya ADOLF MBINGA
 

Attachments

  • FB_IMG_1690071624385.jpg
    93.3 KB · Views: 3
Ni kweli wiki 2 zilizopita alirudishwa kwao kijiji cha mpute nachingwea mkoani lindi akiwa na hali mbaya
ukiona upo hoi unaumwa hlf unarudishwa nyumbani tena kijijini kabisa kule kwa bibi na babu wkt bado aujapona fresh mai fulend ujue imeisha iyo
 
Nilikuwa nampenda saana mwana masanja, alikuwa ni mwanamuziki haswaa, muandishi mzuri, rap zake kiboko. Mtu na pesa zake ilikuwa kiboko, alifanya hatari, elimu ya mjinga kule kwa wana achimenengule huwa zinanikosha nikisikiliza hata leo
 
Daaaa imenifanya nikumbuke ushindani wa Band za Dansi miaka ile ya mwanzoni 2000.
 
Muziki wa Dansi umeyumba sana, kizazi cha Gen Z yaaani hivi vitoto vya mwaka 2000 haviuelewi. Usiombe uende Bar ukute DJ ni hawa watoto wabana pua utaishia kusikiliza Mapigo ya Makarai na Mapipa wao wanaita Amapiano.

Zile nyimbo za Bendi zetu za Twanga, FM Academia, Extra Bongo, Rufita Band, Mashujaa Band na kitu Risasi kidole, Akudo impacteee, Diamond Musica ayseeeeeeee chaliii angu Band zilikuwa kama zote na burudani kama yote. Lkn leo kutokana na mabadiliko kwenye sekta ya burudani hakuna Vipindi vya redio wala TV vinavyopromote muziki wa dansi. Dansi imedorora sana, Anyway wazee wa Dansi leo Ijumaa kama kawaida na Bogos baadae pale Makumbusho tukajimwage mwage kukumbushia enzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…