Habari zenu,
Mimi ni mfanyabiashara wa duka la nafaka na bidhaa ndogo ndogo, sasa kuna star mmoja mwanamuziki naishi nae karibu na biashara yangu, akawa anakuja kukopa everyday mpaka ikafika 80,000.
Kwa kuwa yeye ni star mimi nilimuamini kwamba atalipa sasa kazi ipo kwenye kumdai mara oooh nilisafiri ntakupa, mara oooh natafuta. Mwaka na nusu sasa umekatika.
Nikimueleza mama yake anasema anatafuta, nikamueleza muajili wangu akaniambia nimuite aongee nae, nimemuambia mara oooh nasafiri..
Sasa naombeni ushauri wenu mimi nifanye nini ili niipate hiyo pesa, au nifanye nini ili na mimi nimkomeshe hata akiniona asinisahau!