mKaLI_mOkO
Member
- Aug 6, 2011
- 25
- 4
hali ni ngumu... ila inahitaji kuwa na mjadala wakuangalia elimu yetu.. kwa ushauri wangu pia hasa kwa shule za kata hizi ni wazazi na kata husika kuzimiliki kwa maana kuziangalia kwa makini na kujitolea kuangalia maslahi ya walimu wao.
watoto wa siku hizi mazuzu pia au hlo hamlioni?
No wonder hakuna atakayejiuzulu.
Mkuu sio watoto, hata wazazi mazuzu, ndani ya daladala utakutana na tubinti tuchafu twa maadili utafikiri hatukai na wazazi. Hivi mtoto wa shule ameweka nywele dawa, mkononi ana gazeti la UDAKU (hapa najua namuudhi EMT) na ana simu mbili. Wazazi utafikiri hawamuoni.
napingana na wewe kabisa !si mazuzu -wamendika vikaragosi,mashairi na upuuzi mwingine kwa kuwa wameletewa mitihani juu ya mambo ambayo HAWAJAWAHI KUFUNDISHWA!!!!!watoto wa siku hizi mazuzu pia au hlo hamlioni?
napingana na wewe kabisa !si mazuzu -wamendika vikaragosi,mashairi na upuuzi mwingine kwa kuwa wameletewa mitihani juu ya mambo ambayo HAWAJAWAHI KUFUNDISHWA!!!!!
Tena vitoto vya siku hizi ni vijanja kuliko unavyofikiri wala hawachezi michezo yetu ya zamani-" kariri utaelewa baadaye"
Kashfa nzito
Unakuta mwanafunzi anaeleza anavyolishangaa Bunge mtu anaandika nawashangaa wabunge, wamekaa kama wapo kijiweni, wabunge wamekosa ustaarabu, badala kujadili kero za wananchi waliowachagua, wanapokea timu zilizoshinda makombe timu ikishinda Kombe la Kagame inapokelewa bungeni. Bunge limekuwa kama kijiwe, bungeni siyo ukumbi wa starehe kama mnataka kupokea timu hizo nendeni katika ofisi zao au viwanjani alisema.
................denti huyu anayoakili sema mfumo tu umemuharibia maisha
Siyo utani dogo ana uewelewa wa hali ya juu kabisa, kama anaweza kuliona hilo yupo juu.
Kuna baadhi ya shule unakuta darasa zima watoto hawajajibu somo fulani kwa mfano Biolojia, wanaingia tu na kuandika namba. Tuliamua kuwapigia simu walimu wao, majibu waliyokuwa wakitupa ni kuwa hawajawahi kuwa na walimu wa somo husika kwa hiyo watoto hawakuwa na cha kujaza.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Joyce Ndalichako akionyesha karatasi ya majibu ya mmoja wa watahiniwa wa mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2012, Dar es Salaam jana. Picha na Edwin Mjwahuzi
Mimi bado siamini. Najua mimi na wewe tumepita huko, na wala sio jambo la ajabu kwenye mtihani kukutana na jambo ambalo ama ulijui au umesahau ndio maana ukaitwa mtihani. Je kwenye hali hiyo ulikua unaandika matusi au bongo fleva kwenye answer sheet? Kuna shida nyingine kubwa tu na watoto wa siku hizi
yani utashangaa form six wa saivi hajui chchte mpk aibu. Unabaki kujiuliza kafikaje apo alipotatizo siasa zinazofanywa kwenye matokeo ya darasa la saba na form 2 wakati wenzao wa necta wapo kikazi zaidi na hawataki masihara, kuna watu ambao hawakustahili kufika huko form4 sioni ajabu kwa majibu hayo,kama mtu anaingia form1 hajui kusoma na kuandika unatarajia nini, kama wanafunzi wangekuwa wanajiweza huo muda wa kusoma mashairi wangekuwa wanasoma kiswahili walau wapate c wasingepata ziro