Kabende Msakila
JF-Expert Member
- Oct 7, 2020
- 1,809
- 1,692
Wanabodi, Heri ya mwaka mpya wa 2021!
Nimekaa kwa muda nikitafakali, kujiuliza na kutafuta majawabu kuhusu mienendo ya viongozi kuwachapa bakora wananchi kufuatia tuhuma mbalimbali dhidi ya wachapwaji.
Huenda viongozi hao wana sababu za msingi au hawana - wengine huwachapa bakora wakosaji kwa provocation, wengine hufanya hivyo waonekane miamba, na wengine wameenda mbali mpaka wanaadhibu kwa push-ups watumishi jeshini kama Dkt Kigwangala nk.
SASA
Wewe mwananchi kama ungekuwa na mamlaka ya kuwachapa bakora viongozi au watawala ungemchapa nani na kwa sababu zipi?
= Ungemchapa kiongozi kwa kuwa ameshindwa kukufikishia maji kijijini?
= Ungemchapa kwa kuwa ameshindwa kuwa mbunifu wa vyanzo vya mapato ya Halmashauri / Wilaya?
= Ungemchapa kwa kuwa kijana wako kakosa mikopo ya elimu ya juu?
= Ungemchapa yupi sababu ya vijana wetu kukosa ajira katika vijiji, kata na wilaya?
Mwisho, nashauri viongozi wauweke pembeni utamaduni wa kuwachapa watu bakora na baada yake wajielekeze kwenye Sheria.
******** **********
Nimegundua kuwa wengi wetu hatuna sababu mahususi za kulaumu wale wanaochapa bakora - lkn pia wengi wetu tunasukumwa na kasumba ya visasi - kwa nini umcharaze mwenzako bakora?
Nimekaa kwa muda nikitafakali, kujiuliza na kutafuta majawabu kuhusu mienendo ya viongozi kuwachapa bakora wananchi kufuatia tuhuma mbalimbali dhidi ya wachapwaji.
Huenda viongozi hao wana sababu za msingi au hawana - wengine huwachapa bakora wakosaji kwa provocation, wengine hufanya hivyo waonekane miamba, na wengine wameenda mbali mpaka wanaadhibu kwa push-ups watumishi jeshini kama Dkt Kigwangala nk.
SASA
Wewe mwananchi kama ungekuwa na mamlaka ya kuwachapa bakora viongozi au watawala ungemchapa nani na kwa sababu zipi?
= Ungemchapa kiongozi kwa kuwa ameshindwa kukufikishia maji kijijini?
= Ungemchapa kwa kuwa ameshindwa kuwa mbunifu wa vyanzo vya mapato ya Halmashauri / Wilaya?
= Ungemchapa kwa kuwa kijana wako kakosa mikopo ya elimu ya juu?
= Ungemchapa yupi sababu ya vijana wetu kukosa ajira katika vijiji, kata na wilaya?
Mwisho, nashauri viongozi wauweke pembeni utamaduni wa kuwachapa watu bakora na baada yake wajielekeze kwenye Sheria.
******** **********
Nimegundua kuwa wengi wetu hatuna sababu mahususi za kulaumu wale wanaochapa bakora - lkn pia wengi wetu tunasukumwa na kasumba ya visasi - kwa nini umcharaze mwenzako bakora?