Mwanangu ana mwandiko mbaya

Mbangubangu

Senior Member
Joined
May 6, 2013
Posts
188
Reaction score
69
Kuna tatizo kubwa sana linanisumbua juu ya mwanangu shuleni.

Yupo class one na ni shule nzuri tu tena English medium.Tatizo ni kwamba mwandiko wake ni mbaya kupitiliza, sasa nashindwa kuelewa walimu hawaoni au wako busy?

Swala la pili ni kuwa shule tunalipa ada kubwa tu lakini bado unaambiwa mtoto apelekwe tution.

Sasa kama tution tunalipa bado uwe na mda wa kufanya homework na mtoto kwa maisha haya si tabu tu jamani.

Unapata tabu kumtafutia mahitaji muhimu bado nafasi ya ualimu pia uichukue
 
ungeitaja hiyo shule tungekusaidia zaidi,maana watanzania tulishakua na kasumba shule ni english medium na unalipa pesa nyingi ndio elimu bora,mwanzoni sikuelewa hili,iangalie hiyo shule vizuri utajua kuna tatizo,kulipa pesa nyingi sio solution ya elimu,kitu kingine mimi kitu nilichojifunza kwa wenzetu wazungu,sisi wabongo unataka mtoto wa darasa la kwanza awe anajua vyote kwa mara moja kusoma,kuandika etc,ni vitu ambavyo kwa wenzetu haviko hivyo ingawa kwetu tangia vidudu unamsukuma ajue vyote kwa mara moja,nadhani kunakua na age mtoto ni kujifunza kucheza na wenzake na ku socialise,huyo mwanao atakua pengine hana tatizo,ni shule aliyopo na wewe mzazi kutaka uharaka wako awe na mwandiko mzuri,kitu kingine mtoto wa darasa la kwanza kwenda tuition huo ni wehu,atapumzika saa ngapi huyo mtoto na atacheza saa ngapi,muundo elimu yetu imeshuka tukubalini ukweli,nawakilisha,CCM hiyo.
 
Chukua muda wa kumsaidia mwanao usiwaachie walimu kila kitu pia usiziamini sana english medium schools nyingi ni majanga
 
Kweli nakubaliana nanyi wadau mliochangia.ni wazi kabisa elimu ya sasa sio kabisa na nadhani hizi shule zipo kibiashara zaidi ns sio kutoa huduma.shule yenyewe ni St . Patrick sakina kwa Idd
 


Mkuu mtoto mdogo Kama huyo haina haja ya kumpeleka tuition..

Hakikisha anapata mda Wa kupumzika atokapo shuleni then umsaidie nyakati za jioni kumpa stadi za uandishi...

Jitahidini kuwa na mda mzuri Wa kukaa na watoto zenu mkiwasaidia maana umri huo anaamini mno wazazi...
 
Mwandiko mbaya sio hoja kuna watu wana miandiko pumba bt wanafanya poa sana pia tuition hata wewe mwenyewe mzazi its a part of tuition kwa mwanao, akirudi toka shule baada ya kupumzika mwambie achukue daftari mpige msasa kidogo ndio inashauriwa hivyo
 
Watoto wengi wanaosoma English medium wana miandiko mibaya hii ni kutoka na Elimu ya waalimu wao katika vyuo vyao vya ualimu.
Kwa hivyo ni jukumu lako sasa kumfundisha mwanao namna ya kuunda herufi
 
mpeleke city accademy njia panda makongo juu wapo vizuri sana wanamonita mtoto wako utpenda na wanakwambia atafanya interview b4 joining, wanampima uelewa wake na ada yake ni poa sana utapenda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…