Mwanangu hataki kula nimfanyeje?

Mtende

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2010
Posts
6,385
Reaction score
7,332
Wadau naamini jf ni mpango mzima,naombeni msaada wa kiushauri,mtoto wangu ana miezi saba sasa ila hataki kabisa kula,alipofikisha miezi sita nilimwanzishia vyakula vyepesi kama uji,mashed potatoes,mtori,in short vyakula vilaini pamoja na matunda, kadri siku zinavyoenda baby anagoma kabisaaaaa .

Though nimejaribu kumbadilishia vyakula ila hataki kabisa,yani anataka nyonyo tu, na kitu anachokula mbali na nyonyo ni matunda,hebu nipeni mauzoefu,ni vyakula gani labda vinaweza kumpa apetite au nimpe nini maana nilimpeleka hospital for check up wakasema yupo very ok.

Msaada plz
 
mpatie dawa ya kumuongezea apetite ya kula kwa watoto kama (APETAMIN-P) syrup zinapatikana maduka ya dawa.
 
Sikushauri umpatie mtoto dawa kwasababu kagoma kula.Huyo ni mtoto lakini ana akili zake na njama vilevile anajua akigoma kula chakula utampa nyonyo!Epuka kuweka chumvi au sukari nyingi kwenye chakula chake muache aonje ladha ya chakula.Usimnyonyeshe akipatwa na njaa atakula tu.Na jaribu vyakula tofauti mfano hizo potatoes changanya na carrots au na samaki,uji pia mjaribishe wa ladha tofauti mfano wa mchele,wa shayiri au mtama.
 
Unakionja hicho chakula? Unless ni kitamu hata kwako inawezekana ndo maana anakataa. Weka carrots nyingi na zuchini ufanye kitamu. Kama wewe haushindi nyumbani hakikisha analishwa kabla haujarudi home.
 
Lazima apelekwe hospital tujue loss of appetite related to what?unaweza ukatibu hiyo sign bt tukawa hatujamsaidia huyo baby!sawa zipo vitamin b complex and newtravit bt kampeleke kwa vipimo!
 
Jaribu kumpa chakula tofauti tofauti mpaka upate anachokipenda. Kama ni matunda unaweza ukachanganya na mboga za majani ili angalau apate lishe (hasa vitamin C na iron). Kama ni nyama unachanganya na carrot na viazi vitamu, huenda anapenda ile ladha tamu (sweetness). Unaweza kuendelea kumpa maziwa pia, lakini jaribu kupunguza kadri anavyokua, halafu unaongeza chakula. Huwa tunashauriwa kumpa mtoto si zaidi ya nusu lita ya maziwa kwa siku kwa umri huo. Give the baby some time, usimpe madawa hasa kama ni mzima wa afya. Watoto ni binadamu pia, huenda na wao wana vyakula ambavyo hawavipendi.
 
naomba nidandie hapa.........mimi wanagu wapo hivyo hivyo nimepiga mboko weeee hadi nimechoka mmoja ana 6 mwingine 3 kumbe wakiwa na mdada hom bwana wanakula vzri tukirudi tuuuu sio mideko hiyo wakati mwingine ni pozi tu
 
Mtoto wako ana miezi 7 unamlazimisha kula duh? kwanini haumnyonyeshi mpaka afike miaka 2? Umesha choka kumnyonyesha maziwa yako? unataka maziwa yako yasianguke nini?
 
Kuna picha hutolewa wakati wa uchaguzi hata kama mtoto hapendi kula ukimwoyesha hizo atakula. Hebu jaribu kutafuta hizo picha
 
Mpe juice ya machungwa na uji usiwe wa lishe bali mpe uji wa aina tofaiti in altenative days, kama leo ulezi, kesho maindi then .... Na mchuzi wa maini na mboga mboga au matembele kama una wwza blend, kumbuka kadiri wanavo kua wanapata lactulose intolarance so usisahau kumcheulisha
 
Mtoto wako ana miezi 7 unamlazimisha kula duh? kwanini haumnyonyeshi mpaka afike miaka 2? Umesha choka kumnyonyesha maziwa yako? unataka maziwa yako yasianguke nini?
Kwa iyo mtoto hatakiwi kula chochote mpaka afikishe iyo miaka miwilk?
 
Kwa iyo mtoto hatakiwi kula chochote mpaka afikishe iyo miaka miwilk?
Mtoto wa miezi 6 kama hataki chakula unacho mpa usimlazimishe kula kw anguvu mpe maziwa yako bado mtoto mdogo wa kunyonya maziwa ya mama. Mtoto wa kumlazimishakual ni mtoto wam miaka 2 sio mtoto wa miezi 6 acheni ukatili wa watoto nyie wazazi.
 
Mtoto wa miezi 6 kama hataki chakula unacho mpa usimlazimishe kula kw anguvu mpe maziwa yako bado mtoto mdogo wa kunyonya maziwa ya mama. Mtoto wa kumlazimishakual ni mtoto wam miaka 2 sio mtoto wa miezi 6 acheni ukatili wa watoto nyie wazazi.
Mafundisho tunayopewa huku ni kwamba mtoto akishafikisha miezi sita anatakiwa aanze kula vyakula vilaini pamoja na kunyonya.Sio kwamba ukimwanzishia vyakula vingine unamwachisha ziwa no.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…