Mwanangu hawezi kukaa na ana miezi mitano

Mwanangu hawezi kukaa na ana miezi mitano

Last edited by a moderator:
Kuna watoto huwa wazito tu,na miezi mitano bado ni mdogo labda mama atuambie kwa nini ana hofu?
Kama ni mtoto wa kwanza na hayuko na mzoefu Karibu akienda clinic aongee na nurse kuhusu hofu yoyote aliyonayo katika ukuaji wa mtoto,kama kuna tatizo litatambuliwa mapema na kutafutiwa ufumbuzi.
mi nataka nijue maxmum time ambayo mtoto anaanza kukaa.
 
Angalia usiwe umemuaribu mtoto na michepuko.atamaliza miez kumi bado ajakaa.kama ujafanya hivyo muache soon atakaa na kutambaa kwa pamoja
sina michepuko wala sijawahi kumgusa mama watoto tangu mimb iwe kubwa....kwani mwanamke akijifungua mwanaume siruhusiwi kula mambo yangu kwa wengine?
 
Watoto wengi tu huchelewa kukaa, kutambaa, kusimama, na hata kutembea. Miezi mitano si mingi ya kuanza kujipa pressure.

Mbona wangu alianza kukaa na miezi saba?? Acha wasiwasi,anza kumkalisha taratibu,atazoea
 
Usimlazimishe kukaa akiwa tayari atakaa mwenyewe...wewe unaweza kumfanyia mazoezi ukae nae lkn atakaa mwenyewe baada ya muda..ni kawaida kwa watoto wengine kuchelewa kukaa nakumbuka iuna mtoto wa rafiki yangu kakaa akiwa na miezi 6 au 7 na akaanza kutambaa hapohapo pia....kama umeshaanza kumuonjesha vyakula vya watoto unaweza umkalishe kwenye kiti cha watoto kama hiki itamsaidia akazane haraka!
View attachment 166170
tena nimesahau hata kuhesabu vizuri...huyu mwanangu ana approach mwezi wa saba yaani tar 10/7/2014 atakuwa tayari na saba kamili, ila hata akikalishwa(mazoezi) hawezi kukaa
 
uwe unamkalisha mara moja moja,na hakikisha ana mahali pa kuegemea vizuri
 
usiwe na haraka, atakaa tu mara shingo yake itakapokaza.

kuna umri wa kukaa, lakini watoto hawafanani.
 
Back
Top Bottom