John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Mkimbiaji wa mbio fupi wa Nigeria, Blessing Okagbare amefungiwa kushiriki mashindano ya riadha kwa miaka 10 kwa kukiuka taratibu za kuzuia matumizi ya dawa za kuongeza nguvu michezoni.
Kikosi cha kusimamia uaminifu kwa wakiambiaji (AIU) kimesema mwanariadha huyo mwenye miaka 33 amefungiwa kwa miaka mitano kwa matumizi ya dawa mbalimbali zilizopigwa marufuku michezoni na miaka mitano kwa kushindwa kutoa ushirikiano kwenye uchunguzi dhidi yake.
Okagbare alisimamishwa wakati wa mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika kwenye mji mkuu wa Japan, Tokyo kwa kukutwa na vimelea vya dawa za kuongeza nguvu kwenye vipimo vya kawaida kabla ya mashindano.
Mwanariadha huyo ana siku 30 za kukata rufaa kupitia mahakama ya usuluhishi wa michezo ya (CAS) kupinga hukumu hiyo.
Kikosi cha kusimamia uaminifu kwa wakiambiaji (AIU) kimesema mwanariadha huyo mwenye miaka 33 amefungiwa kwa miaka mitano kwa matumizi ya dawa mbalimbali zilizopigwa marufuku michezoni na miaka mitano kwa kushindwa kutoa ushirikiano kwenye uchunguzi dhidi yake.
Okagbare alisimamishwa wakati wa mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika kwenye mji mkuu wa Japan, Tokyo kwa kukutwa na vimelea vya dawa za kuongeza nguvu kwenye vipimo vya kawaida kabla ya mashindano.
Mwanariadha huyo ana siku 30 za kukata rufaa kupitia mahakama ya usuluhishi wa michezo ya (CAS) kupinga hukumu hiyo.