Mwanasheria halmashauri Arusha,atishwa na kasi ya chadema,aomba uhamisho

Mwanasheria halmashauri Arusha,atishwa na kasi ya chadema,aomba uhamisho

Mwan mpambanaji

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2008
Posts
482
Reaction score
131
Katika hali inayoonyesha kuogopa kasi ya madiwani wa chadema,mwanasheria wa halmashauri ya Arusha Bw Paul Mugasha,ameomba kuhamishwa ghafla,na sasa ataripoti Mwanga kwenye kituo kipya cha kazi.Hivi karibuni diwani mmoja wa chadema wa kata ya Levolosi alimweleza mwanasheria huyo kama mtu hatari kwa halmashauri na akasisitiza kuwa lazima ashughulikiwe kwa kuisababishia halmashauri hasara ya mamilion ya fedha.
Huyu mwanasheria ameingia mikataba mingi ya kifisadi,ukiwamo ule wa soko la kilombero uliovunjwa kwa shinikizo kubwa kutoka kwa diwani huyo wa chadema kata ya Levolosi.mkataba mwingine ni wa car park kati ya Halmashauri na Kilimanjaro printers eneo la stend kuu ya mabasi ,unaokusanywa kwa masaa 24,ilihali halmashauri haipati mgao huo.Kampuni hii ilitishia kumshitaki diwani wa kata ya Levolosi Mh Nanyaro,kwa kuwakataza kukusanya ushuru eneo la stend ya Loliondo,katika sakata hili ndio huyu diwani akamweleza mwanasheria ufisadi wake na kwamba umefika mwisho.
 
Mchawi anakimbia anapogundua tunguli zimeishiwa nguvu. Big up diwani wetu, kwani amekimbilia mwanga ndio hatuwezi kumfuatilia aletwe arusha kwenye kesi. My Godness. Yahani hata hela ya wagonjwa wa Loliondo anakula?:help:
 
Hata angeenda Mikoa ya kusini atafuatwa hukohuko,acha hapa Mwanga ya pua na mdomo. Lazima awajibishwe! Huu ni wkt wa UKOMBOZI!!
 
Kama amesababisha ubadhirifu wowote hata huko alikokimbilia tutaenda kumnyofoa tu.
 
Huyu ashughulikiwe ipasavyo kwa gharama yoyote ile. Heko diwani umeonesha kwamba unachukia ufisadi kwa kiwango cha juu sana songa mbele mpaka kielweke. Natamani angekuwa Manispaa ya Kinondoni huyu diwani maana ndo kuna ufisadi mkubwa kama huu wa kumlinda mkurugenzi kwa shilingi takriban milioni 90 na kuandaa uchaguzi wa CCM kwa zaidi ya shilingi milioni 40 huku hospitali ya Mwananyamala ikikosa dawa.
 
Du Kweli huyu mwanasheria anajua anachokifanya, amekimbilia Mwanga kule madiwani wote CCM, Wazee wakuungamkono hoja 100/100.
 
Hongera diwani kwa kazi nzuri nyota njema honekana asubuhi, Kero ya Parking Fee ktk Halmashauri ya Arusha imezidi kampuni zakukatsha ushuru wa Parking zimekua nyingi kila moja inatoza ushuru bilakuitambua nyingine pia wanatoza ushuru mpaka nje ya mji kwenye maeneo ya watu binafsi, chakusikitisha zaidi ni majina ya kampuni hizo ktk soko la kilombero kunakampuni moja inaitwa Piga Dili! ikiinia tu ktk soko hilo utakutana nao mlangoni.
 
Back
Top Bottom