unajua kuwa mtu hatakiwi kuhesabika kuwa ni mhalifu hadi pale itakapothibitishwa na mahakama kuwa yeye ni mhalifu?
pia, ni mazoea tu kwa hapa tz, kwa nchi za wenzetu, ikitokea mtu amefanya kosa la jinai na hana uwezo wa kumweka mwanasheria amtetee, serikali huwa inagarimia mwanasheria, yaani serikali inamtafutia mwanasheria na kumlipa ili yule mhalifu atetewe na mwanasheria kama vile waendesha mashitaka walio wanasheria wanavyoshitaki. ili haki iwe imetendeka haitakiwi kutamkwa tu kuwa imetendeka, inatakiwa ionekane kuwa imetendeka.
hakuna haki yeyote kwa mwanasheria mwenye degree ambaye ni mwendesha mashitaka, anapopambana na mtuhumiwa ambaye pengine ni la saba hajui chochote kuhusu sheria. unafikiri kuna usawa hapo? sasa ili pawepo na usawa, kunatakiwa kuwa na uwakilishi pande zote mbili halafu ndio zianze kuchapwa, mwanasheria huku na mwanasheria kule wazichapee wee atakayeshinda hapo kuna ushindi wa uhalali kidogo. ukiweka mwanasheria huku na mfugaji asiyejua hata kiswahili huku ni sawa na kumpiganisha tembo na sisimizi. na hapo inakuwa haina umuhimu wa kupeleka mtu mahakamani wangempeleka tu gerezani kwasababu lazima tu atashindwa, hawezi kushindana na mwenye degree ya sheria. vilevile, uwakilishi ni haki yako wewe mhalifu. haki hii haiondolewi hata unapokuwa na tuhuma, zile ni tuhuma tu na pengine ulichokifanya hata kama umekifanya kina justification ya sheria you never know.