TANZIA Mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania, Njelu Kasaka amefariki dunia katika Hospitali ya Rufaa Mbeya alipokuwa akipatiwa matibabu

TANZIA Mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania, Njelu Kasaka amefariki dunia katika Hospitali ya Rufaa Mbeya alipokuwa akipatiwa matibabu

Walikuwa na umoja wao kama sijasahau walikuwa wanajiita G20 bungeni.
Likikuwa kundi la maruhuni linaitwa G55 lililokuwa linataka kuvunja muungano yeye ndie Alikuwa kinara kilichomkuta ataenda kusimulia huko aendako Hakuna mtaka kuvunja muungano au muungana na wavunja anayeweza survive politically Abood Jumbe akishindwa ,Seif sharrif Hamad yalimshinda,Lowasa kuungana na wavunja muungano akina Chadema na Seif sharrf Hamad likawadodea Kama lilivyomdodea Malechela na Njelu Kasaka huyu aliyeongoza kundi la maruhuni wataka kuvunja muungano huu uliopo wa serikali mbili wakitaka tatu
 
Masache Kasaka amethibitisha kifo cha Baba Yake kwa kusema amefariki dunia kutokana na tatizo la moyo lililokuwa linamsumbua. “Wakati anaedelea na matibabu katika hospitali akapata mshituko wa moyo uliosababisha kufariki dunia,” . Msiba uko nyumbani kwake, Chunya mkoani Mbeya, “na mazishi yatakuwa Jumapili (tarehe 5 Julai,2020).”

Kasaka ambaye amepata kuwa mbunge, Waziri na mkuu wa mkoa, alijitoa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka 2015 na kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kugombea ubunge jimbo la Lupa.

Mwaka 2019, Kasaka alizindua kitabu chake alichokiita ‘Njelu Kasaka: Maisha, Siasa na Hoja ya Tanganyika-G55.”

Mzee Njelu Kasaka ameacha watoto saba na mjane mmoja.

Baada ya kusoma makala yake nikaisaka CV ya Njelu Kasaka

Njelu Kasaka: Hakuna aliye salama ndani na nje ya CCM

Njelu Kasaka ajiunga na CHADEMA

Wako wapi G55?

Kapumzike mzee wetu historia itakukumbuka kwa G55
 
Kipindi cha kina Philip Marmo sasa mbona huyu Marmo mfumo haukumtupa akiendelea kuwepo serikalini?
 
Poleni wafiwa!

Marehemu ameacha historia kubwa sana katika kupigania Tanganyika na bahati mbaya amefariki ndoto yake ikiwa haijatimia ila uzuri mapambono yanaendelea.
 
Kama siyo Nyerere basi leo tungekuwa na serikali ya Tanganyika.
Hivyo vichwa vya G55 vilipanga hoja zilizompoteza kabisa mzee wetu mpendwa Julius Kambarage Nyerere ambaye aliishiwa kabisa hoja za kuvikabili vichwa hivyo ikabidi asiye mbunge au kiongozi kwa wakati huo aombe kuingia bungeni ambako aliishia kutishia kwamba kama wataendelea kushikilia hoja hiyo basi yeye atarudisha kadi namba moja na kujitoa CCM.
SI kweli kwamba Mwl Nyerere alizidiwa hoja na kundi la G55 ila walishindwa alikuwa PM , Mzee Malecela kwa kubali hoja. Mwl Nyerere ameandika vizuri katiak kitabu chake cha Our Leadership and the Destine of Tanzania: Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Kinapatikan Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF). Pia alitisha PRESS CONFERENCE na kuelezea umma wa Watanzania juu ya hoja ya Serikali ya Tanganyika. Wengine katika kundi hilo ni Jenerali Ulimwengu, Matheo Qaresi n., Partick Qorro n.k Mwl Nyerere aliimbia CCM wakati wa mchakato wa kumpata mgombea wa Urais kwa awamu ya tatu maana Mzee Malecela bado alitaka kugombea, ndiyo JKN akasema kama huyu naye anagombea basi mimi narudisha kadi yangu ya CCM kwa jinsi alivyokuwa amechukia kuona PM anashindwa kumshauri Mzee Mwinyi juu ya hoja ya Serikali ya Tanganyika!
 
SI kweli kwamba Mwl Nyerere alizidiwa hoja na kundi la G55 ila walishindwa alikuwa PM , Mzee Malecela kwa kubali hoja. Mwl Nyerere ameandika vizuri katiak kitabu chake cha Our Leadership and the Destine of Tanzania: Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Kinapatikan Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF). Pia alitisha PRESS CONFERENCE na kuelezea umma wa Watanzania juu ya hoja ya Serikali ya Tanganyika. Wengine katika kundi hilo ni Jenerali Ulimwengu, Matheo Qaresi n., Partick Qorro n.k Mwl Nyerere aliimbia CCM wakati wa mchakato wa kumpata mgombea wa Urais kwa awamu ya tatu maana Mzee Malecela bado alitaka kugombea, ndiyo JKN akasema kama huyu naye anagombea basi mimi narudisha kadi yangu ya CCM kwa jinsi alivyokuwa amechukia kuona PM anashindwa kumshauri Mzee Mwinyi juu ya hoja ya Serikali ya Tanganyika!
Marmo hakuwa na kiherehere kwa hiyo aliweza kuendelea na siasa kama Mbunge lakini yule Njelu ndiye alikuwa kiongozi na hata historia ndogo ina onesha kuwa hata mashuleni au vyuoni wanaogonza mgomo nidyo huwa wanapata adhabu kubwa. Ndivyo ilivyotokea kwa Mzee Njelu
 
Nyerere ilibidi aingilie kati 1993

Mwinyi na Malecela walishatepeta wakakubali kurudisha serikal ya Tanganyika
 
Pumzika kwa amani mwana mwema wa mama Tanganyika na mtanganyika halisi. Utakumbukwa daima kwa ajili ya G-55. Gone are the days when men were men, and monkeys were still in the bush; unlike nowadays when you can find monkeys at Serena hotel in the city centre. 😢
 
Huyu mzee alianzisha kundi la wabunge 55 la kudai serikali ya Tanganyika wakati malecela akiwa waziri mkuu kitu kilichomuudhi Sana Nyerere na ndiyo sababu malecela kukataliwa kugombea urais.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Ukitaka kusambaratisha muungano huu uliopo uwe CCM au upinzani uraisi hupati

Mgombea yeyote Cha Kwanza Cha kumfanya ashinde ni msimamo wake kuhusu muungano

Wote waliotaka kuubomoa walibomoka wenyewe
 
Back
Top Bottom