MwanaSimba yeyote aniambie sababu zozote za maana za kumtimua Uchebe

Mwanachama yeyte wa Simba , Simba ni yake.
 
Uchebe naye alianza kuyumba na hata angekuwepo hali ingekuwa kama hii tu.

1.Alikuwa ameanza kuishiwa mbinu, ndio maana Simba ilianza kushinda kwa bahati nasibu. Graph ya ushindi wa Simba ilikuwa na mwendo wa diminishing progression.

2.Mnatumia Simba kufika robo fainali CCL kama credit kwake, ila hamjui kuna mbinu za nyuma ya pazia zitumike kuifikisha pale. Angalia mechi za away alivyokuwa anafanya utumbo, timu ikiwa home ground watu walikuwa wanaingia mzigoni kumsaidia, yet alianza kusaidiwa anaanza kulalama anaingiliwa majukumu.

3.Timu ilianza kuwa na nidhamu mbovu chini yake.

4.Kwamba yeye alikuwa hafungwi kwenye ligi? Hamjui kuna point 5 tumepoteza chini ya Aussems kwenye TPL?

5.Eti kwanini alifukuzwa ilhali Simba inaongoza ligi? Jibu la swali hili rejea hapo no.1. Na hii ndo sababu inayofanya Barcelona nao wamtimue kocha wao Ernesto Velverde. Ilifika kipindi tulianza kukosa imani kama Aussems angetuvusha, sawa na Barcelona ambavyo wamekosa imani na Ernesto pamoja na timu hiyo bado kuwa kwenye msimamo mzuri wa La Liga. Tatizo lao wote ni moja; kadri ligi inavyosonga mbele timu zinaanza kushinda kwa bahati nasibu at a diminishing rate.
 
Jibu umelipata Kiongozi. Ubabaishaji uliokithiri
 
unastahili kupata balimi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo si kuondoka Uchebe kwani kila mtu ataondoka Simba siku yake ikifika hata Mo ataondoka lakini unamleta nani wa kuziba pengo lake? Uchebe falsafa yake ni kushambulia kwa kwenda mbele akiwa na washambuliaji wawili kwa hiyo Simba iilikuwa inapiga kambi kwenye goli la timu pinzani muda wote wa mchezo. Huyu wa sasa hivi bado sijaelewa hasa falsafa yake ni ipi kwani mara nyingi naona anatumia mshambuliaji mmoja.

Kwa mfumo anaoutumia kocha mpya na msaidizi wake Matola wa mshambuliaji mmoja badala ya wawili wakati Simba ndio timu yenye viungo bora kabisa Tanzania natabiri hawa makocha pamoja na yule wa makipa hawana miezi miwili mbele watakuwa wameshatimuliwa.

Una Kagere na Boko wote wapo fiti halafu unampanga mmoja mwingine unamuweka benchi hapo ndio shida inapoanzia akishafichwa ng'ado kwa ng'ado (mtu na mtu) basi kwishney mashambulizi yaanahamia kwenu mnafungwa goli moja mpira umeisha halafu bado mnashangaa Mtibwa mwenye usajili wa milioni moja kachukuaje kombe mbele ya timu yenye usajili wa mabilioni.

Najua mzungu hakuwepo msimu uliopita lakini Matola alikuwa haoni ule utatu wa Kagere, Okwi na Boko ulivyokuwa unafanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu? Kwa nini sasa Boko na Kagere wasianze pamoja halafu wakaongezewa mtu mmoja mbadala wa Okwi?

Na kwa mechi ya jana na mtibwa walaumiwe makocha kwa upangaji mbovu wa timu ukizingatia ilikuwa fainali. Walishindwaje kupanga wanaume 11 katikia kundi la wanaume na wavulana lenye watu zaidi ya 25?
 
tatizo la mashabiki na wanachama wengi wa simba walikuwa hawamsikilizi mzee Kilomoni wakamwelewa leo hii Mo anafanya maamuzi yake wanaanza kuhoji wakati nguvu ya kuhoji walishamkabidhi sasa hivi wakubali tu wawe washabiki kama wanavyoshabikia timu za ulaya
 
Marefarii bado kichomi kabisa, goli la fraga ni halali kabisa, jamaa alikuwa onside ila kutokana na presha za waamuzi kwenye mechi za simba tumenyimwa goli halali kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…