Uchebe naye alianza kuyumba na hata angekuwepo hali ingekuwa kama hii tu.
1.Alikuwa ameanza kuishiwa mbinu, ndio maana Simba ilianza kushinda kwa bahati nasibu. Graph ya ushindi wa Simba ilikuwa na mwendo wa diminishing progression.
2.Mnatumia Simba kufika robo fainali CCL kama credit kwake, ila hamjui kuna mbinu za nyuma ya pazia zitumike kuifikisha pale. Angalia mechi za away alivyokuwa anafanya utumbo, timu ikiwa home ground watu walikuwa wanaingia mzigoni kumsaidia, yet alianza kusaidiwa anaanza kulalama anaingiliwa majukumu.
3.Timu ilianza kuwa na nidhamu mbovu chini yake.
4.Kwamba yeye alikuwa hafungwi kwenye ligi? Hamjui kuna point 5 tumepoteza chini ya Aussems kwenye TPL?
5.Eti kwanini alifukuzwa ilhali Simba inaongoza ligi? Jibu la swali hili rejea hapo no.1. Na hii ndo sababu inayofanya Barcelona nao wamtimue kocha wao Ernesto Velverde. Ilifika kipindi tulianza kukosa imani kama Aussems angetuvusha, sawa na Barcelona ambavyo wamekosa imani na Ernesto pamoja na timu hiyo bado kuwa kwenye msimamo mzuri wa La Liga. Tatizo lao wote ni moja; kadri ligi inavyosonga mbele timu zinaanza kushinda kwa bahati nasibu at a diminishing rate.