Kama vile umechanganya kati ya kutahiriwa na jando. Nadhani ulikuwa unamaanisha kutahiriwa tuu na siyo jando?
Kutahiriwa inaweza kuwa sehemu ya jando, lakini jando ina maana pana zaidi.
Kwa mfano, katika sehemu nyingi za duania, watoto wa kiume hutahiriwa kwa sababu za kiafya.
Katika sehemu nyingine za dunia ni kawaida kwa wanaume kutotahiriwa kamwe.
Watu kama Wayahudi na Waislamu wanatahiriwa kwa sababu tofauti na za kiafya.
Wao wanaona kutahiriwa kuwa jambo lenye maana ya kidini zaidi.
Hata hivyo, katika mataifa mengine, sherehe ya kutahiriwa inafanywa kwa mtoto wa kiume anapokuwa mtu mzima.
Hii inaitwa kumpeleka jandoni, yaani, shule ya kitamaduni, ambako anatahiriwa na kutengwa na jamii kwa majuma fulani mpaka apone.
Akiwa huko jandoni anafundwa kwa kuwa jamii husika huwa zinaamini kuwa kutahiriwa ni kidhibitisho kuwa amekuwa mtu mzima.
Kwahiyo, kutahiriwa ni kuondoa tuu ile ngozi, lakini jando inahusisha kutahiriwa pamoja na mtoto huyo kufundwa kuwa mwanamume.
Kwa hiyo sidhani kama ulitaka kujua kama kuna madhara gani ya kufanya mapenzi na mwanaume ambaye hajaenda jando, aka hajafundwa kuwa mwanaume.