mwanaume asiyetaka kuoa



Umeongea maneno mengi sana lakini sijaona hata 1 la maana hapo,mtoa mada kawakumbusha,wewe umeng'ang'ania kalawazimisha,kama wewe kuowa kwako ni mzigo waache wenye kuowa waowe,lakini usiwasemee wote kama msemaji wao,vijana kuowa muhimu,jambo 1 muhimu mtu akishaoa huwa linakuja automatically japo si kwa wote,mtu akishaoa mara nyingi mambo yake hunyooka kwa sababu mambo mengi ya upuuzi ataachana nayo automatically!
 


Umeongea maneno mengi sana lakini sijaona hata 1 la maana hapo,mtoa mada kawakumbusha,wewe umeng'ang'ania kalawazimisha,kama wewe kuowa kwako ni mzigo waache wenye kuowa waowe,lakini usiwasemee wote kama msemaji wao,vijana kuowa muhimu,jambo 1 muhimu mtu akishaoa huwa linakuja automatically japo si kwa wote,mtu akishaoa mara nyingi mambo yake hunyooka kwa sababu mambo mengi ya upuuzi ataachana nayo automatically! Ila hata mimi bado sijaoa na nina 28yrs mungu akipenda soon ntavuta jiko,
 
huyo ni ******* au anaogopa kua hayawezi vizuri mambo
ila pia sio lazima wote waoe jamani khaa!
 
Kuoa ni majaliwa, bado haijafika siku zao za kuoa, ikifika wataoa tu.

Mimi nilitaka kuoa toka na miaka 15, lakini sikuoa mpaa nilipo fika miaka 25 😱
 
siku hizi watu wanaingia kwenye hili zoezi 'kuondoa nuksi tu' baada ya hapo kila mtu anapuyanga kimpango wake
Sasa hapa unaondowa nuksi au unaingiza nuksi!!??.....
Kila mtu ana haki yake ya kuchaguwa maisha anayotaka kuishi, si vyema kuingia kwenye ndoa kwa sababu ya presha ya ndugu na marafiki zako, mwisho wa siku mke anabaki kuwa mkeo na sio wa familia.
 
Sasa wewe umeajiliwa na nani hapa kuwa msemaji wa wengine? porojo nyingi mbele giza, yaani unataka kuwaaminisha watu hapa mambo yako yanaweza kunyooka kwa sababu ya kuoa! je unaoa SACCOS au ndio nyinyi mkiona tu binti ana kigari chake cha mkopo basi mnatangaza ndoa, matarajio yenu ya umarioo yasipotimia ndoa zinasambaratika!!
 
Ndoa ipo kama sindano ya viatu, inaingia kiulaini lakini lazima irudishe uzi na kipande cha ngozi wakati inarudi. Ndio maana wengi wanaogopa kundowaniwa.
 
Kuoa/kuoelewa sio lazima.
Ni kitu ambacho watu wanatakiwa kufanya pale wanapoona wanae mtu anaefaa kuwa mume/mke wa maana badala ya kuoa/olewa na matatizo kisa tu mtu anaishi maisha ya kufuata mkumbo. Mtajajuuuuuuta kuwafahamu hao mnaokurupuka kuwaoa/olewa nao ili tu na nyie muwe kwenye kundi la waliooa na kuolewa.
 
jamani jamani.......


ndio hivyo preta, inatokea unaempenda hakupendi unampenda asiyekupenda.. Ingekua ndoa unaamua tu unaoa/olewa na yoyote mambo yasingekuwa magumu.
Off topic: mzima wewe.
 
katika mademu niliowafanyia interview ya ndoa hamna aliyekidhi viwango vya kuwa mke!!!tatizo madem zetu wa mjini ndo hawa hawa leo shemeji yako kesho demu wako!!
 
heheheheee a. We hapo juu umenipa raha kweli
 

Mtoa mada kaja hapa na template yake ya maisha ambayo anataka kila mtu aifuate, katuambia maisha yana "steji", na ni jukumu letu wanadamu kujipanga ili kuvukakila "steji".

Mie namuonyesha kwamba "steji" hizo anazoziona ni jukumu kuzivuka, kwa wengine si jukumu wala lazima.

Zaidi ya hapo, hajatueleza definition yae ya "kuoa" kwani tamaduni tofauti zinatafsiri "kuoa" tofauti.

Sasa watu kuanza kudiscuss "kuoa" bila hata kujua "kuoa" huku ni kuoa gani? Kuoa kisheria au kimila? Kuoa huku kunahusisha "common lawmarriage" au hakuhusishi? Kuoa huku ni kwa mwanamme tu, mwanamke anaolewa, au kama tamaduni nyingine hata mwanamke anaoa? et cetera et cetera.

Maana mtu anaweza kukaa na mwanamke wakazaa watoto na kufanya yote pamoja, bila ya kwenda kanisani, msikitini wala kwa mkuu wa wailaya, huyo kaoa au hajaoa? Common law inatambua ndoa, dini hatambui. Sasa kuoa kunakoongelewa hapa kupi?

Usitake ku simplify vitu zaidi ya vilivyo.
 


akili yangu ya utambuzi inaniambia kwamba huenda wewe ni mwanamke uliyekuwa na maringo enzi za usichana wako,sasa hivi umri umeenda na hupati bwana
 
yan mimi nimepita tuuuu ila bado saaaaaaaaaana nipo nipo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…