Mwanaume kuiomba airtime voucher!!!!


kama ana hela za mawazo kwenye fone y ana call? c a2me sms tu....yaan hii ni gia ya kumkimbia vibaya sana...m delete kabisa...hapo mpo mwanzo mkiyaanza mapenzi itakuwaje? yaan sio wapenzi but ana kubomu mkiwa wapenzi itakuwaje?....eti sweet na wewe ulishawahi kumuomba voucher?
 
Pole sana dada,
Ulizani umepata kumbe umepatikana!
Unatakiwa kulipa 2000 kwa maongezi mlioongea .
Jamaa yuko kiuchumi zaidi
 
Pole sana dada,
Ulizani umepata kumbe umepatikana!
Unatakiwa kulipa 2000 kwa maongezi mlioongea .
Jamaa yuko kiuchumi zaidi

he!kwani nilimtuma apige simu alaa
 

sijawahi kumuomba..kwanza alianzia mbali sana, mara anaomba flash nikampa hakurudisha siku hiyo akanipigia simu usiku kunambia ooh sorry nitakupa kesho,mie haya,mara hajamaliza kusema hivyo eti credit inaisha pls call me back,mi nikajua ana ishu ya kiofisi..nikamcall,kumbe anaongea upuuzi mtupu..ndo aliniudhiiiii
 
mshauri awe anakupigia usiku kuanzia saa 6 kwa tigo kama hawezi piga mchana
 
Imebidi nao waanze kuomba maana wadada wengine nao wamezidi!Hua wanatumia kipindi cha kutongozwa kumchekea mwanaume ili aendelee kuomba vocha hata kama hamtaki!Kama huna muda nae mwambie mapema ili asiendelee kumaliza vi300 vyake..kama unaelekea kumpa ndio mtumie tu bwana!
 
kazowea kulelewa huyo, mpige kibuti cha maana na usigeuke nyuma. atakutesa huyo ukimpa chance
 

nimeshaongea mpaka mate yametoka kuwa simtakii..ye analazimisha eti 'kwani shemeji anakutimizia mahitaji yote'...
hahhaha wanaume bwana...:lol::lol:
 

Huyo anakupima! ukimtumia inamaanisha umemkubalia (kua mpenzi) ...usipotuma inamaanisha bado hujaingia laini...ataaendelea kukutongoza..
 
Kuna ubaya gani kuombwa vocha wewe mtoto wa kike? Mmeadhimiasha MAMA MIA ya nini? Si mnataka usawa? Kwa hiyo mnapotuomba sisi mnafikiri tunafurahi? Inatuuma pia. Ndio usawa huo, wacha vyako navyo viliwe! Alaaaaaaaah
 
Kama mwanamke unaomba airtime kwa mwanaume sidhani ni kosa kwa mwanaume kuomba mwanaume..Mazoea na mazingira kati ya hao watu ndio inaweza kuwa tatizo.
 
mnataka usawa huku bado mambo mengine hamtaki kuyaaccept. buku 2 kitu gani?
 
nimeshaongea mpaka mate yametoka kuwa simtakii..ye analazimisha eti 'kwani shemeji anakutimizia mahitaji yote'...
hahhaha wanaume bwana...:lol::lol:
Mwambie "ananitimizia mpaka vocha anatuma badala ya kuomba!We unaweza?"Akiwa na ubavu wa kukwambia ndio mwambie akurushie buku 10 saa hiyo hiyo na kama hawezi achape mwendo!
 
Mwambie "ananitimizia mpaka vocha anatuma badala ya kuomba!We unaweza?"Akiwa na ubavu wa kukwambia ndio mwambie akurushie buku 10 saa hiyo hiyo na kama hawezi achape mwendo!

kweli kabisa amwambie hivo mwanamke huombi bana mwanaume mwenyewe anatuma bila kuambiwa kwa hiyo hata akikuta vijana wanalalamika wakiombwa anawashangaa tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…