Mwanaume kumpiga mwanamke ni ishara ya udhaifu

Mwanaume kumpiga mwanamke ni ishara ya udhaifu

King Jody

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2022
Posts
1,834
Reaction score
3,456
Wakati mwingine ni kweli wanakuwa na maneno ya kuudhi au kwa lugha nyingine unaweza kusema wana mdomo,

Kamwe huwezi kumbadilisha mwanamke tabia kwa kipigo, ni mtu mzima amelelewa kwao na wewe umelelewa kwenu mmekutana ukubwani, kila mtu na tabia yake.

Tafuta njia mbadala ya kukaa naye na kuzungumza kwa upendo, ni mtu mzima atakuelewa japo wapo ambao ni pasua kichwa, hawasikii wala hawaelewi, utapiga utaua bure.

Mwanake siyo mtoto mdogo eti umbadilishe tabia kwa kipigo, akiamua kutulia atatulia mwenyewe, tumia hekima na busara badala ya kipigo.

Mpende, mjali, mdekeze pale inapobidi na kumheshimu, mpige kwa maneno mazuri mf. wewe ni mwanamke mrembo kliko wote Duniani, msifie, mtamkie neno nakupenda mara kwa mara.

Biblia Takatifu inatuambia tuishi nao kwa kutumia akili. soma 1.Petro 3.7 Kadhalika enyi wanaume. Kaeni na wake zenu kwa akili: na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu:

Nb. Amani na upendo vikae nanyi siku zote.

download.jpg
 
Kuna wanawake wengine wakiwa na meno 32 hawaelewi
Mpaka awe na mapengo ndiyo anatulia
Muhimu kataa ndoa
 
Kwa nini upangie wanaume namna ya kuishi na wake zao?

Mi naamini hujawahi kuvutugwa makusudi.

Kama hujaombwa ushauri usitoe!

Wakati mwingine ni kweli wanakuwa na maneno ya kuudhi au kwa lugha nyingine unaweza kusema wana mdomo,

Kamwe huwezi kumbadilisha mwanamke tabia kwa kipigo, ni mtu mzima amelelewa kwao na wewe umelelewa kwenu mmekutana ukubwani, kila mtu na tabia yake.

Tafuta njia mbadala ya kukaa naye na kuzungumza kwa upendo, ni mtu mzima atakuelewa japo wapo ambao ni pasua kichwa, hawasikii wala hawaelewi, utapiga utaua bure.

Mwanake siyo mtoto mdogo eti umbadilishe tabia kwa kipigo, akiamua kutulia atatulia mwenyewe, tumia hekima na busara badala ya kipigo.

Mpende, mjali, mdekeze pale inapobidi na kumheshimu, mpige kwa maneno mazuri mf. wewe ni mwanamke mrembo kliko wote Duniani, msifie, mtamkie neno nakupenda mara kwa mara.

Biblia Takatifu inatuambia tuishi nao kwa kutumia akili. soma 1.Petro 3.7 Kadhalika enyi wanaume. Kaeni na wake zenu kwa akili: na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu:

Nb. Amani na upendo vikae nanyi siku zote.

View attachment 3056741
 

Attachments

  • IMG_5257.jpeg
    IMG_5257.jpeg
    54.9 KB · Views: 14
Tatizo mwanamke ukimpiga akianza kulia unamuonea tena huruma wanaume wajinga huwa wanaanza hadi kuwaomba msamaha.

la usikae kiboya kama kazingua sana na ameanza kupandisha sauti au dharau nyingi na ulishawahi kumuonya chapa tuvibao.

Wanawake ni kama watoto ishi nao kwa akili
 
Back
Top Bottom