Mwandishi wa Habari wa The Guardian anadai amepigwa na Walimu baada ya kupiga picha Wanafunzi wakisoma chini ya miti

Mwandishi wa Habari wa The Guardian anadai amepigwa na Walimu baada ya kupiga picha Wanafunzi wakisoma chini ya miti

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Nimeona ujumbe huu ukisambaa kwenye mitandao ya kijamii pamoja na picha husika, nikaona niusogeze hapa ili Wadau watie neno.....

Mimi ni Dickson Ng'hily Mhariri wa Biashara na Mkuu wa Kitendo cha Digital The Guardian

Wakuu hamjambo.. Nimekamatwa na Walimu wa Shule ya Msingi Kwembe, Kata ya Kwembe, Wilaya ya Ubungo wakaanza kunipiga na kisha wakaagiza Wanafunzi waanze kunishambulia kwa kunipiga baada ya kunikuta nikipiga picha Wanafunzi wanasomea nje na chini ya mti.

Baada ya wao kuniumiza wamenipeleka Serikali ya Mtaa, yakatokea mabishano wakitaka nifute picha nilizopiga ndio waniachie.

Walioona nimegoma wakaamua kunileta Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wa Ubungo. Wakaninyang'anya kitambulisho na simu, ila simu zilipokuwa zikipigwa walinipa nipokee, nikatumia muda huo kuwa nazituma sehemu picha bila wao kujua.

Baada ya mabishano marefu ambayo pia yalihusisha DAS ambaye naye aliingilia baada ya kupewa maelekezo na DC mbaye hakuwepo eneo la tukio, wakaniambia nifute picha ndio waniruhusu niondoke.

Hoja yao waliniambia nimepiga simu Watoto na nikiwa eneo la shule, nikawaeleza kuwa sikuwa eneo la shule, nilikuwa mbali kabisa na Shule na hata mtu akisema atambue sura ya mtoto au Mwanafunzi hawezi kumtambua kutoka na umbali.

Mimi niliamua kupiga picha kwa kuwa nimekuwa nikiona wanakaa chini ya miti mara kwa mara, hivyo nikachukua kwa umbali ili niweze kutumia kwenye matumizi yangu ya baadaye.

Wameniumiza na wameharibu simu yangu sehemu ya kioo lakini sina mpango wa kuwashtaki kwa kuwa naamini nilichokuwa nakifanya ni kwa ajili ya Taifa na faida kwa haohao Wanafunzi walioambiwa wanipige.


Wanafunzi chini 4 .jpg

Wanafunzi chini 1.jpg

Wanafunzi chini 3.jpg

Tamko la THRDC ~ THRDC yakemea Mwandishi wa Habari kukamatwa kwa kupiga picha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe wakisoma chini ya mti

Majibu ya Serikali ~ Madai ya Wanafunzi kusomea chini ya mti Shule ya Msingi Kwembe (Dar), Serikali yasema walikuwa katika programu maalumu
 
Hivi kusoma mpka mjifungie ndani ya chumba. Naona hapo ndio pazuri wanasoma huku wanapigwa na upepo.
We uko sawa kweli?
Mtoto ataweza kuandika vizuri akiwa umekaa chini?
Huoni hapo ubao na wanafunzi wamekaa chini wengine wanapigwa na jua?
Mtoto anaweza ku-concetrate anachofundishwa sehemu kama hiyo?
Shida hapo inaonekana ni hamna madarasa ya kutosha.

Wewe inawezekana ni mmoja wa maticha waliompiga mshkaji.
 
Kwa Wabobezi kitendo tu cha Kukamatwa na Kupigwa na hao Walimu kwa Kupiga hizi Picha tayari kimeonyesha kuwa hufai kuwa Mwandishi wa Habari na huna Ethics kwani kuna maeneo kadhaa ya Kitaaluma nimeona yamekosewa / umeyakosea hivyo napongezwa Kupigwa Kwako na tena nawalaumu kwa Kukupiga kidogo hivyo.
 
DC kazi anayoiweza ni kufukuzana na machangudoa usiku wa manane ila kufuatilia mambo muhimu aaahh!

Alafu kesi inaenda mahakamani Kila siku ushahidi haujakamilika.

Kuna mwingine kule Simiyu analipwa marupurupu tele anaenda kulawiti kibinti Cha miaka 21.

#serikali kuu ya walawitaji.
 
Wilaya ya Ubungo,huko mikoani ndani ndani itakuwaje?

Kwamba serikali hupeleka pesa halafu zinaliwa?
 
Walimu wa Tanzania jinsi akili zao zilivyo mbovu, Badala ya kutoa ushirikiano mzuri kwa huyo Mwandishi wa Habari ili awapazie sauti kuhusu taabu zao kusudi zitatuliwe, wao wameamua kumpa adhabu. Ni aibu gani hii kwa Walimu hao?
 
Mwandishi wa habari Hakuwa sahihi:
1. Kwenda kupiga picha shuleni bila kibali maalumu ni kosa.
- kajitetea kuwa alikuwa mbali na walipokuwa wanafunzi, kwanini avizie badala ya kwenda moja kwa moja na kujitambulisha kwa uongozi wa hiyo shule?

2. Amekiri kuzisambaza hizo picha jambo linaloenda kinyume na Sheria ya makosa ya kimtandao ya mwaka 2015.

NB: SITETEI UZEMBE WA SERIKALI KATIKA UHABA NA UBOVU WA MIUNDOMBINU YA SHULE, ILA NAMNA MWANDISHI ALIVYOFANYA YUKO KINYUME NA SHERIA.
 
Whistle blower ana haki zake. Ametuamsha wengi. Ni vizuri tujue mazuri na mapungufu yetu. Walimu hao ni vichwa maji hawaoni fursa hapa!!!!!
 
Kaka Bora walivyo kupiga. Tena wangekuitia Wananchi wakupige ukome hivi kwa joto la dsm c Bora usomee njer pia wewe ni mbeya tu kma ni mwandishi wa habari kweli ungeenda kuwagoji Nini tatizo Sasa unawapiga picha harafu unaweka maneno yako
 
Back
Top Bottom