Mwandishi wa kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Azory Gwanda apotea. Ni siku 10 na hajulikani alipo

Mwandishi wa kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Azory Gwanda apotea. Ni siku 10 na hajulikani alipo

Hii Dunia au hii Tanzania?
Popote mkuu siasa imeacha vidonda vikubwa sana kwenye maisha ya watu...juzi tu trump alikuwa aendee..huki rusia na ukraine mwaka wa 4 sijui vitaa tuuu.
 
Mwandishi wa @MwananchiNews apotea. Siku 10 hajulikani alipo. Alikuwa anafanya uchunguzi wa Habari nyeti. Nataraji kesho tutajua zaidi - ZZK.

View attachment 643853

KUHUSU AZORY GWANDA
Azory Gwanda alizaliwa 1975 na alikuwa ni mwandishi wa habari wa Kampuni ya ya Mwananchi Communications iliyopo jijini Dar es Salaam.

Azory Gwanda alikuwa ana umri wa miaka 42 wakati wa kutoweka kwake. Gwanda alikuwa akiishi katika shamba karibu na Kibiti, Tanzania, na mkewe Anna Pinoni. Mama yake, Eva Mpulumba kutoka kijiji cha Msimba katika Mkoa wa Kigoma, aliishi na familia yake yote, lakini ndiye ndugu pekee aliyehojiwa kuhusu kupotea kwa Gwanda.

Wakati akifanya kazi katika Kampuni ya Mwananchi kama mwandishi wa habari wa kujitegemea, Gwanda aliandika mfululizo wa habari za mauaji yaliyokuwa yakitekelezwa huko. Inadhaniwa utekaji wake unahusiana na mfululizo wa habari za mauaji ambazo Gwanda alikuwa akiziandika.

Kupotea kwa Gwanda kumechochea mashirika mengi kujitolea kusimamia na kulinda haki za waandishi wa habari ulimwenguni kote. Haukupita hata mwezi mmoja baada ya kutoweka kwa Gwanda, shirika MISA Tanzania ilitoa tamko la kufadhaika kwao juu ya ukosefu wa taarifa kamili kuhusiana na kutoweka kwa Gwanda, na kukiita kitendo hicho kuwa "shambulio la uhuru wa waandishi wa habari ambalo lazima lihukumiwe"

Theophil Makunga, mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri wa Tanzania, alisema watu wenye nia mbaya na Gwanda na taifa kwa ujumla walikuwa wakiendelea kufanya uovu wao hata kwa waandishi wa habari akiwemo Gwanda.

PIA, SOMA:
VISA DHIDI YA WANAHABARI WENGINE WA TANZANIA:
PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
Watuhumiwa watano akiwamo katibu wa Mbunge wa jimbo la Kilolo Kefa Walles, Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi kupitia CCM wilaya ya Kilolo Hedikosi Kimwaga, Diwani kata ya Nyanzwa Boniface Ugwale maarufu kama 'Katili', Wille Chikweo na Silla Kimwaga wamefikishwa mbele ya Mahakama ya wilaya ya Iringa kwa tuhuma za kumuua aliyekuwa katibu wa CCM Wilaya ya Kilolo Bi. Christina Kibiki.

Kesi hii ya Jinai namba 34404 ya Mwaka 2024 iliyowahusisha baadhi ya viongozi wa CCM imesomwa mbele ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Iringa Rehema Mayagilo na kusimamiwa na mwendesha mashtaka upande wa Jamhuri Sauli Makori.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa hilo Novemba 12, 2024 eneo Banawanu lililopo kata ya Mseke majira ya usiku nyumbani alipokuwa akiishi Marehemu Bi. Christina Kibiki.

Hata hivyo watuhumiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwani upelekezi wa kesi hii bado unaendelea hivyo kesi imeahirishwa hadi Januari 7, 2025 ambapo itakuja tena kwa ajili ya kutajwa.

Ikumbukwe Bi Christina Kibiki aliuawa kikatili kwa kuchomwa na vitu vyenye Ncha kali eneo la tumboni kisha kupigwa risasi na watu wasiojulikana usiku wa novemba 12, 2024 akiwa nyumbani kwake.

Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande wakisubili tarehe tajwa kwaajili kujibu kesi inayowakabili baada ya upelekezi wote kukamilika.
 

Attachments

  • 1735906670129.png
    1735906670129.png
    865.6 KB · Views: 3
Back
Top Bottom