Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Mwandishi wa habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL) Zanzibar, Jesse Mikofu ameshambuliwa na askari wa vikosi vya SMZ wakati akitekeleza majukumu yake ya kazi leo asubuhi Jumatano Aprili 21, 2021.
Mikofu amekumbwa na kadhia hiyo baada ya kuwapiga picha askari hao wakati wakitekeleza jukumu lao la kuwahamisha wamachinga waliopanga bidhaa zao barabarani katika eneo la darajani.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Awadh Juma Haji amesema hana taarifa za tukio hilo na kuahidi kutoa ushirikiano zitakapomfikia.
Mwandishi wa habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL) Zanzibar, Jesse Mikofu
Akisimulia hali ilivyokuwa, Mikofu amesema pamoja na kupigwa, kuvutwa, kutakiwa kugaragara kwenye maji machafu na kupiga push-up, vifaa vyake vya kazi ikiwemo simu ya mkononi aliyoitumia kupiga picha vimeharibiwa.
“Nilifika darajani na kukuta askari wanabeba meza zilizokuwa zikitumiwa na wamachinga na kuzipandisha kwenye magari yao, nikatoa simu na kuanza kupiga picha, nyuma yangu wakatokea askari wakanihoji nikajitambulisha na kuonyesha vitambulisho.”
“Hawakuridhishwa wakanipeleka kwa kiongozi wao ambako huko ndiko nilikokutana na adhabu, niliambiwa nikae chini ninyooshe miguu, nipakate mawe makubwa wakiniambia niyabembeleze kama mtoto,” amesema.
Pamoja na adhabu hiyo Mikofu aliendelea kupigwa na askari hao wakimtaka kuonyesha picha alizopiga na baadaye kumlazimisha kubadili nywila kwenye barua pepe yake.
“Kiongozi wao akaandika namba yake kwenye simu yangu ili nimtumie zile picha nikazituma, wakaniambia nibadilishe passwords (nywila) nikagoma, akaitwa askari mwingine akabadilisha palepale, kisha wakanilazimisha niipige ile simu kwenye mawe hadi ivunjike, sikuwa na namna nyingine nikafanya hivyo,” amesisitiza.
Mwandishi wa habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL) Zanzibar, Jesse Mikofu
Amesema pia akaelekezwa kuingia kwenye dimbwi la maji ya mvua yaliyotuama na kugaragara kwenye maji hayo na baada ya kitendo hicho aliruhusiwa kuondoka katika eneo hilo.
VISA DHIDI YA WANAHABARI WENGINE WA TANZANIA:
Mikofu amekumbwa na kadhia hiyo baada ya kuwapiga picha askari hao wakati wakitekeleza jukumu lao la kuwahamisha wamachinga waliopanga bidhaa zao barabarani katika eneo la darajani.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Awadh Juma Haji amesema hana taarifa za tukio hilo na kuahidi kutoa ushirikiano zitakapomfikia.
Mwandishi wa habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL) Zanzibar, Jesse Mikofu
Akisimulia hali ilivyokuwa, Mikofu amesema pamoja na kupigwa, kuvutwa, kutakiwa kugaragara kwenye maji machafu na kupiga push-up, vifaa vyake vya kazi ikiwemo simu ya mkononi aliyoitumia kupiga picha vimeharibiwa.
“Nilifika darajani na kukuta askari wanabeba meza zilizokuwa zikitumiwa na wamachinga na kuzipandisha kwenye magari yao, nikatoa simu na kuanza kupiga picha, nyuma yangu wakatokea askari wakanihoji nikajitambulisha na kuonyesha vitambulisho.”
“Hawakuridhishwa wakanipeleka kwa kiongozi wao ambako huko ndiko nilikokutana na adhabu, niliambiwa nikae chini ninyooshe miguu, nipakate mawe makubwa wakiniambia niyabembeleze kama mtoto,” amesema.
Pamoja na adhabu hiyo Mikofu aliendelea kupigwa na askari hao wakimtaka kuonyesha picha alizopiga na baadaye kumlazimisha kubadili nywila kwenye barua pepe yake.
“Kiongozi wao akaandika namba yake kwenye simu yangu ili nimtumie zile picha nikazituma, wakaniambia nibadilishe passwords (nywila) nikagoma, akaitwa askari mwingine akabadilisha palepale, kisha wakanilazimisha niipige ile simu kwenye mawe hadi ivunjike, sikuwa na namna nyingine nikafanya hivyo,” amesisitiza.
Mwandishi wa habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL) Zanzibar, Jesse Mikofu
Amesema pia akaelekezwa kuingia kwenye dimbwi la maji ya mvua yaliyotuama na kugaragara kwenye maji hayo na baada ya kitendo hicho aliruhusiwa kuondoka katika eneo hilo.
VISA DHIDI YA WANAHABARI WENGINE WA TANZANIA:
- Mwandishi wa kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Azory Gwanda apotea siku 10 na hajulikani alipo
- Mhariri Mtendaji wa Gazeti la MwanaHALISI, Saed Kubenea avamiwa na kumwagiwa tindikali akiwa ofisini kwake
- Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA
- Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa
- Mwandishi wa Watetezi TV mbaroni kwa madai ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni juu ya watuhumiwa kulazimishwa kulawitiana Kituo cha Polisi
- Mwandishi wa Habari, Kazimbaya Makwega ashikiliwa na Polisi, asafirishwa kutoka Mwanza hadi Dodoma
- Mwandishi wa Habari, Kazimbaya Makwega ashikiliwa na Polisi, asafirishwa kutoka Mwanza hadi Dodoma
- Mchora katuni Opptertus John Fwema ashikiliwa na Polisi kwa Makosa ya Mtandao