Mwandishi wa Watetezi TV mbaroni kwa madai ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni juu ya watuhumiwa kulazimishwa kulawitiana Kituo cha Polisi

Mwandishi wa Watetezi TV mbaroni kwa madai ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni juu ya watuhumiwa kulazimishwa kulawitiana Kituo cha Polisi

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKAMATWA KWA MWANDISHI WA HABARI ZA KIUCHUNGUZI JOSEPH GANDYE WA WATETEZI TV.

1.0 Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu una laani tukio la kukamatwa kwa Mwandishi wa Habari Joseph Gandye, ambaye ni Mhariri wa Uzalishaji Maudhui msimamizi msaidizi wa Watetezi TV.

Gandye alikamatwa leo tarehe 22.08.2019 baada ya kupigiwa simu na askari aliyejitambulisha kwa jina la Godfrey Mkude ambaye alimtaka mwandishi huyo kwenda kituo cha polisi Urafiki kwa ajili ya mahojiano.

Baada ya kuchukuliwa maelezo chini ya wakili Jones Sendodo, dhamana yake ilikataliwa kwa maelezo kwamba amri ya kumkamata imetoka Iringa hivyo kituo cha polisi Urafiki wao wanamuhifadhi na baadae atapelekwa Iringa kwa ajili ya taratibu zingine.

2.0 Mnamo Juni 17, 2019 Waandishi wa habari wa Kituo cha Luninga cha mtandaoni (Online TV) cha Watetezi TV walipokea taarifa ya kuwepo kwa vitendo vya udhalilishwaji wa watuhumiwa katika Kituo cha Polisi Mafinga mkoani Iringa.

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Mwandishi Joseph Gadye alifunga safari hadi mkoani Iringa kwa ajili ya kufuatilia habari hiyo kwa kufanya uchunguzi wa kutosha na mnamo Agosti 09, 2019 Watetezi TV iliripoti tukio la ukatili wa Askari wa jeshi la polisi katika Kituo cha Polisi Mafinga mkoani Iringa katika mitandao yake (Facebook, Twitter na You tube channel).

Katika tukio hilo inadaiwa kuwa vijana sita (Majina yao yanahifadhiwa) wakazi wa Mafinga walikamatwa na kuteswa na maofisa kwa jeshi la polisi na inadaiwa kuwa walipigwa na kulazimishwa kulawitiana wao kwao wakiwa kituoni.

Watuhumiwa hao sita walikamatwa na jeshi la polisi mnamo mwezi Mei 19, 2019 na kushikiliwa kwa takribani siku 10 katika Kituo cha Polisi Mafinga, ambapo inadaiwa kuwa walipigwa na kulazimishwa kulawitiana wao kwa wao mbele ya maofisa wa jeshi la polisi kituo cha Mafinga wakati wakifanyiwa mahojiano.

Baada ya Watetezi TV kutoa ripoti yake sehemu ya kwanza Agosti 09, 2019 kuhusu ukatili huo, jeshi la polisi mkoani Iringa kupitia kwa Kamanda wa Polisi mkoa (RPC), ACP Juma Bwire ilikanusha taarifa hiyo na kudai kuwa ni uongo unaosambazwa mitandaoni kwa lengo la kulidhalilisha jeshi la polisi na kuichafua serikali kwa ujumla.

“Jeshi la polisi mkoa wa Iringa linaonya hao watu wanaotoa taarifa za uongo na upotoshaji zenye lengo la kudhalilisha jeshi la polisi Tanzania na serikali kwa ujumla. Hivyo, tunatoa onyo watu wenye tabia hizo kuacha mara moja. Aidha, nimemuagiza mkuu wa upelelezi afuatilie kwa watu wanaopotosha na kutoa taarifa za uongo. Pindi watakapopatikana basi hatua za kisheria zichukuliwe. Na sasa hivi tunaendelea kufuatilia kwenye mitandao taarifa mbalimbali zikirushwa. Kwahiyo, atakayebainika tutachukua hatua kali za kisheria,” alisema RPC Bwire katika taarifa yake na wanahabari mnamo Agosti 14, 2019.

3.0 Leo Agosti 22, 2019 Mwandishi wa habari Watetezi TV, Joseph Gandye aliyechapisha habari hiyo ametakiwa kuripoti Kituo cha Polisi Urafiki, Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Gandye ambaye alipigiwa simu leo majira ya saa 05.20 alifika kituoni hapo na kusubiri zaidi ya masaa 2.

Hatimaye Mwandishi huyo alihojiwa mbele ya Wakili Jones Sendodo kwa tuhuma za kuchapisha habari za uongo mtandaoni kinyume na Sheria ya Makosa ya Mtandao.

Mwandishi Joseph Gandye amekamatwa rasmi katika kituo cha polisi Urafiki jijini Dar es Salaam . Mkuu wa kituo hicho amesema hawezi kumpa dhamana kwa kua hana mamlaka yoyote kwa kua aliemkamata ni polisi kutoka Iringa .

Polisi kutoka Iringa wanafanya mipango ya kumsafirisha Joseph Gandye kwenda mkoani Iringa.

4.0 Itakumbukwa mwandishi huyu ndie alietoa habari ya mwanafunzi Hosea Manga, aliechapwa na mwalimu mpaka kuvunjika uti wa mgongo mkoani Njombe.

Vilevile aliripoti kuhusu uonevu uliokua unafanywa na polisi Loliondo na kwa taarifa hiyo kupitia Watetezi TV Waziri wa mambo ya ndani Mh. Kangi Lugola aliweza kufatilia suala hilo na kulifanyia kazi.

Mwandishi Joseph Gandye si tu miongoni mwa mwandishi mahiri bali mtayarishaji mzuri wa kipindi cha vya vipindi Haki za Binadamu kinachorushwa live kila siku ya ijumaa saa 10 kamili jioni ndani ya studio za Watetezi TV.

5.0 WITO KWA JESHI LA POLISI MAFINGA

1. Kuzingatia haki zote za mtuhumiwa , kuto kuteswa wala kutwezwa utu wake

2. Haki ya dhamana itolewe kwa kua kosa analotuhumiwa linadhaminika

3. Uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma za udhalilishwaji na uvunjwaji wa haki za binadamu unaofanywa dhidi ya watuhumiwa katika kituo hicho cha polisi.

4. Kuwaacha Waandishi wa Habari wafanye kazi zao bila kuwakamata mara kwa mara .

Imetolewa na Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania.
Onesmo Olengurumwa

Dar es Salaam
22. 08.2019

Zaidi, soma;


Naona katendewa haki kisheria kwa kuwa kwanza ameitwa kituoni, pili amehojiwa mbele ya wakili wake. Naamini siyo tu kwamba haki itatendeka bali itaonekana inatendeka. Kama ana vipicha vya hao kulawitiana ama confession yao kwamba wamelawitiana, basi anaweze ku prove mahakamani kwamba alichoandika/alicho ripoti ni sahihi.
 
Jeshi la polisi hua wanakurupuka na kukanusha kila kitu bila uchunguzi wowote, kuna uwezekano mkubwa kabisa tukio hilo ni la kweli kwasababu polisi wetu sio mara ya kwanza kuthibitika kuwa wamefanya vitendo vya kinyama,
tusisahau walivyowaua na kuwapora mali zao wale wafanyabiashara wa madini, taarifa zilipotoka awali walikanusha hivihivi na kudai waliouawa walikua majambazi.
 
Waliofanyiwa ukatili huo wahojiwe mubashara na vituo vya luninga ( television) ili Watanzania wajue nani anstahili kuadhibiwa.
 
Police tukubaliane mapema..tunaanzia kwenye uraia au turuke moja kwa moja kwenye uhujumu uchumi?
#MembeSemaNeno#
#MwagaPombe2020#
Nadhan kitaalam tungeanza kwanza na ya kukutwa na Meno ya tembo ili akipanda mahakamani ndo wanaikuta ya kutakatisha hela, waonaje hii mkuu.
 
Hii habari niliiona ukienda you tube ya hao watetezi online TV ipo, huyu jamaa alikuwa anawahoji vijana waliofanyiwa hivyo vitendo viovu sasa, washitakiwa wameongea wenyewe jamaa yy katuhabarisha tuu, sasa sijui kosa Lake ni lipi yaani jeshi letu kwa kuficha maovu kisa kulindana ni suala linalotufanya tuendelee kutokuwa na imani nalo katika kulinda usalama wa raia
 
Kwa wenzetu yaani hapo ungeona umahili wa wapelelezi kwa kufichua uovu hata kama ni wa wakubwa zao yaani muovu ni muovu tu hata kama ni askari mwenzao, hivi hapa kwetu tumelogwa na nani, yaani A tunaita B na k tunaita W yaani ni Sanaa tu dah I au a sana aisee
 
Hivi wandishi wa habari wamejifunza kuandika uongo!
 
Serikali mpya, jeshi lile lile. Ilipaswa hawa ma igp wapya wakiingia na wao tusikie wanapanga safu zao upya, kuanzia ocs hadi rpc
 
Hii habari niliiona ukienda you tube ya hao watetezi online TV ipo, huyu jamaa alikuwa anawahoji vijana waliofanyiwa hivyo vitendo viovu sasa, washitakiwa wameongea wenyewe jamaa yy katuhabarisha tuu, sasa sijui kosa Lake ni lipi yaani jeshi letu kwa kuficha maovu kisa kulindana ni suala linalotufanya tuendelee kutokuwa na imani nalo katika kulinda usalama wa raia
Nadhani yeye hakutakiwa kukamatwa kwa kuchapisha au kusambaza habari hii.
Labda kama hakufuata taratibu za kuwapa polisi nafasi ya kuwahoji waeleze maoni yao walihusika vipi na tukio hili.

Kama aliwahoji na chanzo chake cha habari walalamikaji wanaonekana wakihojiwa basi wa kukamatwa ni walio lalamika kutendewa hilo jambo endapo tu polisi wana uhakika walalamikaji wasema na taarifa za tukio la uongo.

Kwa hili jeshi la polisi watazidi kijichafua na kuichafua serikali kuhusu ukandamizaji waandishi wa habari bila sababu za msingi. Kama taarifa za uongo wa kukamtwa ni wale walio zusha uongo ambao ni walalamikaji.

Sasa kama huyu muandishi au mtu yeyite aliwarubuni waseme uongo watajifunza na vijana wengine wataogopa kushiriki matukio kama hayo. Vinginevyo askari walio husika wasilindwe waadhibiwe kama kweli walifanya uhuni huo.
 
Ipo youtube mkuu, wanahojiws na huyu mwandishi na wanasema wao kuwa walilazimishwa kulawitiana. Kama ni uongo basi waongo ni wale vijana sio yeye
Waliofanyiwa ukatili huo wahojiwe mubashara na vituo vya luninga ( television) ili Watanzania wajue nani anstahili kuadhibiwa.
 
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKAMATWA KWA MWANDISHI WA HABARI ZA KIUCHUNGUZI JOSEPH GANDYE WA WATETEZI TV.

1.0 Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu una laani tukio la kukamatwa kwa Mwandishi wa Habari Joseph Gandye, ambaye ni Mhariri wa Uzalishaji Maudhui msimamizi msaidizi wa Watetezi TV.

Gandye alikamatwa leo tarehe 22.08.2019 baada ya kupigiwa simu na askari aliyejitambulisha kwa jina la Godfrey Mkude ambaye alimtaka mwandishi huyo kwenda kituo cha polisi Urafiki kwa ajili ya mahojiano.

Baada ya kuchukuliwa maelezo chini ya wakili Jones Sendodo, dhamana yake ilikataliwa kwa maelezo kwamba amri ya kumkamata imetoka Iringa hivyo kituo cha polisi Urafiki wao wanamuhifadhi na baadae atapelekwa Iringa kwa ajili ya taratibu zingine.

2.0 Mnamo Juni 17, 2019 Waandishi wa habari wa Kituo cha Luninga cha mtandaoni (Online TV) cha Watetezi TV walipokea taarifa ya kuwepo kwa vitendo vya udhalilishwaji wa watuhumiwa katika Kituo cha Polisi Mafinga mkoani Iringa.

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Mwandishi Joseph Gadye alifunga safari hadi mkoani Iringa kwa ajili ya kufuatilia habari hiyo kwa kufanya uchunguzi wa kutosha na mnamo Agosti 09, 2019 Watetezi TV iliripoti tukio la ukatili wa Askari wa jeshi la polisi katika Kituo cha Polisi Mafinga mkoani Iringa katika mitandao yake (Facebook, Twitter na You tube channel).

Katika tukio hilo inadaiwa kuwa vijana sita (Majina yao yanahifadhiwa) wakazi wa Mafinga walikamatwa na kuteswa na maofisa kwa jeshi la polisi na inadaiwa kuwa walipigwa na kulazimishwa kulawitiana wao kwao wakiwa kituoni.

Watuhumiwa hao sita walikamatwa na jeshi la polisi mnamo mwezi Mei 19, 2019 na kushikiliwa kwa takribani siku 10 katika Kituo cha Polisi Mafinga, ambapo inadaiwa kuwa walipigwa na kulazimishwa kulawitiana wao kwa wao mbele ya maofisa wa jeshi la polisi kituo cha Mafinga wakati wakifanyiwa mahojiano.

Baada ya Watetezi TV kutoa ripoti yake sehemu ya kwanza Agosti 09, 2019 kuhusu ukatili huo, jeshi la polisi mkoani Iringa kupitia kwa Kamanda wa Polisi mkoa (RPC), ACP Juma Bwire ilikanusha taarifa hiyo na kudai kuwa ni uongo unaosambazwa mitandaoni kwa lengo la kulidhalilisha jeshi la polisi na kuichafua serikali kwa ujumla.

“Jeshi la polisi mkoa wa Iringa linaonya hao watu wanaotoa taarifa za uongo na upotoshaji zenye lengo la kudhalilisha jeshi la polisi Tanzania na serikali kwa ujumla. Hivyo, tunatoa onyo watu wenye tabia hizo kuacha mara moja. Aidha, nimemuagiza mkuu wa upelelezi afuatilie kwa watu wanaopotosha na kutoa taarifa za uongo. Pindi watakapopatikana basi hatua za kisheria zichukuliwe. Na sasa hivi tunaendelea kufuatilia kwenye mitandao taarifa mbalimbali zikirushwa. Kwahiyo, atakayebainika tutachukua hatua kali za kisheria,” alisema RPC Bwire katika taarifa yake na wanahabari mnamo Agosti 14, 2019.

3.0 Leo Agosti 22, 2019 Mwandishi wa habari Watetezi TV, Joseph Gandye aliyechapisha habari hiyo ametakiwa kuripoti Kituo cha Polisi Urafiki, Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Gandye ambaye alipigiwa simu leo majira ya saa 05.20 alifika kituoni hapo na kusubiri zaidi ya masaa 2.

Hatimaye Mwandishi huyo alihojiwa mbele ya Wakili Jones Sendodo kwa tuhuma za kuchapisha habari za uongo mtandaoni kinyume na Sheria ya Makosa ya Mtandao.

Mwandishi Joseph Gandye amekamatwa rasmi katika kituo cha polisi Urafiki jijini Dar es Salaam . Mkuu wa kituo hicho amesema hawezi kumpa dhamana kwa kua hana mamlaka yoyote kwa kua aliemkamata ni polisi kutoka Iringa .

Polisi kutoka Iringa wanafanya mipango ya kumsafirisha Joseph Gandye kwenda mkoani Iringa.

4.0 Itakumbukwa mwandishi huyu ndie alietoa habari ya mwanafunzi Hosea Manga, aliechapwa na mwalimu mpaka kuvunjika uti wa mgongo mkoani Njombe.

Vilevile aliripoti kuhusu uonevu uliokua unafanywa na polisi Loliondo na kwa taarifa hiyo kupitia Watetezi TV Waziri wa mambo ya ndani Mh. Kangi Lugola aliweza kufatilia suala hilo na kulifanyia kazi.

Mwandishi Joseph Gandye si tu miongoni mwa mwandishi mahiri bali mtayarishaji mzuri wa kipindi cha vya vipindi Haki za Binadamu kinachorushwa live kila siku ya ijumaa saa 10 kamili jioni ndani ya studio za Watetezi TV.

5.0 WITO KWA JESHI LA POLISI MAFINGA

1. Kuzingatia haki zote za mtuhumiwa , kuto kuteswa wala kutwezwa utu wake

2. Haki ya dhamana itolewe kwa kua kosa analotuhumiwa linadhaminika

3. Uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma za udhalilishwaji na uvunjwaji wa haki za binadamu unaofanywa dhidi ya watuhumiwa katika kituo hicho cha polisi.

4. Kuwaacha Waandishi wa Habari wafanye kazi zao bila kuwakamata mara kwa mara .

Imetolewa na Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania.
Onesmo Olengurumwa

Dar es Salaam
22. 08.2019

Zaidi, soma;



Aisee

Fvxk the regime!
 
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKAMATWA KWA MWANDISHI WA HABARI ZA KIUCHUNGUZI JOSEPH GANDYE WA WATETEZI TV.

1.0 Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu una laani tukio la kukamatwa kwa Mwandishi wa Habari Joseph Gandye, ambaye ni Mhariri wa Uzalishaji Maudhui msimamizi msaidizi wa Watetezi TV.

Gandye alikamatwa leo tarehe 22.08.2019 baada ya kupigiwa simu na askari aliyejitambulisha kwa jina la Godfrey Mkude ambaye alimtaka mwandishi huyo kwenda kituo cha polisi Urafiki kwa ajili ya mahojiano.

Baada ya kuchukuliwa maelezo chini ya wakili Jones Sendodo, dhamana yake ilikataliwa kwa maelezo kwamba amri ya kumkamata imetoka Iringa hivyo kituo cha polisi Urafiki wao wanamuhifadhi na baadae atapelekwa Iringa kwa ajili ya taratibu zingine.

2.0 Mnamo Juni 17, 2019 Waandishi wa habari wa Kituo cha Luninga cha mtandaoni (Online TV) cha Watetezi TV walipokea taarifa ya kuwepo kwa vitendo vya udhalilishwaji wa watuhumiwa katika Kituo cha Polisi Mafinga mkoani Iringa.

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Mwandishi Joseph Gadye alifunga safari hadi mkoani Iringa kwa ajili ya kufuatilia habari hiyo kwa kufanya uchunguzi wa kutosha na mnamo Agosti 09, 2019 Watetezi TV iliripoti tukio la ukatili wa Askari wa jeshi la polisi katika Kituo cha Polisi Mafinga mkoani Iringa katika mitandao yake (Facebook, Twitter na You tube channel).

Katika tukio hilo inadaiwa kuwa vijana sita (Majina yao yanahifadhiwa) wakazi wa Mafinga walikamatwa na kuteswa na maofisa kwa jeshi la polisi na inadaiwa kuwa walipigwa na kulazimishwa kulawitiana wao kwao wakiwa kituoni.

Watuhumiwa hao sita walikamatwa na jeshi la polisi mnamo mwezi Mei 19, 2019 na kushikiliwa kwa takribani siku 10 katika Kituo cha Polisi Mafinga, ambapo inadaiwa kuwa walipigwa na kulazimishwa kulawitiana wao kwa wao mbele ya maofisa wa jeshi la polisi kituo cha Mafinga wakati wakifanyiwa mahojiano.

Baada ya Watetezi TV kutoa ripoti yake sehemu ya kwanza Agosti 09, 2019 kuhusu ukatili huo, jeshi la polisi mkoani Iringa kupitia kwa Kamanda wa Polisi mkoa (RPC), ACP Juma Bwire ilikanusha taarifa hiyo na kudai kuwa ni uongo unaosambazwa mitandaoni kwa lengo la kulidhalilisha jeshi la polisi na kuichafua serikali kwa ujumla.

“Jeshi la polisi mkoa wa Iringa linaonya hao watu wanaotoa taarifa za uongo na upotoshaji zenye lengo la kudhalilisha jeshi la polisi Tanzania na serikali kwa ujumla. Hivyo, tunatoa onyo watu wenye tabia hizo kuacha mara moja. Aidha, nimemuagiza mkuu wa upelelezi afuatilie kwa watu wanaopotosha na kutoa taarifa za uongo. Pindi watakapopatikana basi hatua za kisheria zichukuliwe. Na sasa hivi tunaendelea kufuatilia kwenye mitandao taarifa mbalimbali zikirushwa. Kwahiyo, atakayebainika tutachukua hatua kali za kisheria,” alisema RPC Bwire katika taarifa yake na wanahabari mnamo Agosti 14, 2019.

3.0 Leo Agosti 22, 2019 Mwandishi wa habari Watetezi TV, Joseph Gandye aliyechapisha habari hiyo ametakiwa kuripoti Kituo cha Polisi Urafiki, Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Gandye ambaye alipigiwa simu leo majira ya saa 05.20 alifika kituoni hapo na kusubiri zaidi ya masaa 2.

Hatimaye Mwandishi huyo alihojiwa mbele ya Wakili Jones Sendodo kwa tuhuma za kuchapisha habari za uongo mtandaoni kinyume na Sheria ya Makosa ya Mtandao.

Mwandishi Joseph Gandye amekamatwa rasmi katika kituo cha polisi Urafiki jijini Dar es Salaam . Mkuu wa kituo hicho amesema hawezi kumpa dhamana kwa kua hana mamlaka yoyote kwa kua aliemkamata ni polisi kutoka Iringa .

Polisi kutoka Iringa wanafanya mipango ya kumsafirisha Joseph Gandye kwenda mkoani Iringa.

4.0 Itakumbukwa mwandishi huyu ndie alietoa habari ya mwanafunzi Hosea Manga, aliechapwa na mwalimu mpaka kuvunjika uti wa mgongo mkoani Njombe.

Vilevile aliripoti kuhusu uonevu uliokua unafanywa na polisi Loliondo na kwa taarifa hiyo kupitia Watetezi TV Waziri wa mambo ya ndani Mh. Kangi Lugola aliweza kufatilia suala hilo na kulifanyia kazi.

Mwandishi Joseph Gandye si tu miongoni mwa mwandishi mahiri bali mtayarishaji mzuri wa kipindi cha vya vipindi Haki za Binadamu kinachorushwa live kila siku ya ijumaa saa 10 kamili jioni ndani ya studio za Watetezi TV.

5.0 WITO KWA JESHI LA POLISI MAFINGA

1. Kuzingatia haki zote za mtuhumiwa , kuto kuteswa wala kutwezwa utu wake

2. Haki ya dhamana itolewe kwa kua kosa analotuhumiwa linadhaminika

3. Uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma za udhalilishwaji na uvunjwaji wa haki za binadamu unaofanywa dhidi ya watuhumiwa katika kituo hicho cha polisi.

4. Kuwaacha Waandishi wa Habari wafanye kazi zao bila kuwakamata mara kwa mara .

Imetolewa na Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania.
Onesmo Olengurumwa

Dar es Salaam
22. 08.2019

Zaidi, soma;


Polisi wao ndio watuhumiwa halafu wenyewe wajichunguze?
 
Back
Top Bottom