Prof. Mwandosya alichukua uamuzi wa maana wa kutokumshambulia Mwakipesile waziwazi pamoja na kwamba alikuwa anajua kwamba aliachwa pale Mbeya ili amwangalie prof. Mwandosya.
Sasa kama unafahamu hilo unamshangaa vp Kubenea?
. Mwakyembe hakufurahia hilo, yeye alitaka kuendelee kuwa na mikiki mikiki kati ya hao viongozi ili ile vita yake na Mwakipesile nayo ipambe moto.
Kwa taarifa yako, nyuma ya Dk Mwakyembe, yupo Mwandosya na Hilda Ngoye sasa kama Mwakyembe hakufyrahia elewa na Mwandosya= Ngoye nao hawafurahii.
mama yake prof. Mwandosya, mkuu wa mkoa alienda na prof alimpokea bila vinyongo vyovyote.
Alivyofariki mama wa Mwakipesile, prof. Mwandosya naye alienda kumwona.
Mkuu, Siasa ni Unafiki. Bifu za Mwandosya zimekaa kisayansi sio kama za kina EL et al (Mwakipesile akiwamo) Na ndio maana Mwakyusa anatambua kuwa Mwandosya anamfitini asirudi bungeni ili nafasi yake aichukue Hilda Ngoye lakini huwezi kuwakuta Mwakyusa na Mwandosya wana bifu za waziwazi. Wanapanda gari moja, wanakula pamoja na wanatembeleana.
na Mwakyembe ni maadui wakubwa.
Mwakyembe na Mwandosya ni MAADUI wakubwa wa Mtandao wa JK ambao Mwakipesile ni mmoja wao. Uadui wao hautaisha. Uliza kilichotokea wakati wa uchaguzi wa wajumbe ya NEC ya CCM kisha pima intensity ya mgogoro wao.
za chuki na visasi ndizo hata zimesababisha kupungua sana kwa uhusiano kati ya Prof. Mwandosya na Dr. Mwakyembe. Inasemekana prof hapendi hizo siasa za jino kwa jino na anaanza kujiweka pembeni ili asionekane wazi kwamba yuko upande mmoja.
Uongo uliokubuhu, fanya utafiti kisha futa kauli yako.
alivyoenda Mbeya katika sehemu alizotembelea na kufungua miradi ya maana ilikuwa jimbo la prof. Mwandosya. Sidhani kama itakuwa busara eti kumpeleka rais nyumbani kwa waziri? Ataenda nyumbani kwa prof kufanya nini?
Alienda kijijini kwa Mwandosya na hii ilitokana na ombi maalumu la Mwandosya kwa Bosi wake ambapo mara ya kwanza Mwakipesile aliipunch lakini mara ya pili alichemsha.
tujihadhari sana na hawa watu ambao wanataka mkoa uwake moto shauri ya visa vyao binafsi. Huyu Kubenea anatumika sana kuchapisha habari ambazo zinaandikwa na watu wengine na yeye faida kwake ni kuuza hilo gazeti lake.
Ni suala la muda tu, Mbeya moto ulishawaka siku nyingi, Kumbuka ugomvi uliokuwapo kati ya Mulla (Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya) na Mwandosya mwaka 2008.
Mimi ni mfuasi mkubwa wa prof. Mwandosya na naunga mkono strategy yake ya kukaa kimya na kufanya mambo kwa vitendo kule kwake. Hii inamjengea sifa mkoani na hata hao wanaotaka kumwondoa hawatafanikiwa.
Hayuko kimya kama unavyomfikiria, huyu bwana ni hatari. Anaendesha mapambano kisayansi na watu alionao wanaomsaidia vita sio aina ya MAKAMBA.
Kyela Rhoda wala haungwi mkono na mkuu wa majeshi. General Mwamunyange ameamua kuwa pembeni kabisa inapokuja siasa za Kyela maana anajua madhara yake. Huyo Mwakalinga naye anatajwa kuwa mwanafunzi, mbona wote tunajua hapa kwamba ni mfanyakazi tena wa siku nyingi sana? Makosa mengine yanaharibu habari kabisa.
Hapa kidoooooooooooogo umejaribu kuwa mkweli.
MZITTO