Mwanza mwanza mwanza

luofe

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2011
Posts
330
Reaction score
143
Nimechaguliwa kujiunga na chuo kikuu cha afya CUHAS (BUGANDO) kusoma MD but hali ya kiuchumi nyumbani sio nzuri sana nimefanikiwa kupata michango kutoka kwa watu mbalimbali na baada ya kulipia michango nimebakiwa na 1500000 na nisingependa kuendelea kuomba tena kwa miaka minne iliyobaki naomba mnishauri biashara ya kufanya katika mkoa tajwa hapo juu ambayo haiitaji usimamizi wa hali ya juu ili nisifanye vibaya chuoni! PLEASE KAMA HAUNA CHA KUNSHAURI PITA TU!
 
Unafikiri MD ni ya mchezo mpaka uje kufanya biashara, kama utaweza uwe unakaanga mandazi unasupply kuanzia kule hostel na wodini kuanzia C1 mpaka no 9 nina uhakika utakuwa unapiga hela nzuri Dr. luofe.
 
Unafikiri MD ni ya mchezo mpaka uje kufanya biashara, kama utaweza uwe unakaanga mandazi unasupply kuanzia kule hostel na wodini kuanzia C1 mpaka no 9 nina uhakika utakuwa unapiga hela nzuri Dr. luofe.

kaka hali tete huku siku wakisema hawana maana yake ni kwamba hakuna chuo tena!
 
Nunua injini ya Boti ya mchina uje nayo uwe unakodisha kwa wavuvi...
 
kaka hali tete huku siku wakisema hawana maana yake ni kwamba hakuna chuo tena!

Pole sana Doc! Maisha yana changamoto zake, cha msingi ni kutokata tamaa na kupambana tu!

Mwanza ina fursa nyingi sana. Tatizo kubwa ninaloona ni kuwa watu tunapenda kukopi sana matokeo yake watu wengi wanafanya shughuli inayofanana na mwisho wa siku, hakuna faida ya kueleweka.

Ukipitia nyuzi za miezi michache iliyopita, utakuta uzi wa dogo mmoja wa Mwanza aliyeomba ashauri kama unaohitaji wewe kwa mtaji wa 2m. Wadau walimpa ushauri mwingi mzuri, ukiwemo Mradi mdogo sana wa Cafe ya Maziwa ya kienyeji.

Ninaamini Chuoni utakutana na wenye changamoto na nia kama yako. Jaribu kuunganisha nguvu na mmoja wao ili kukuza mtaji na kupunguza gharama za usimamizi.

Vinginevyo, kila la kheri kwenye ma-bugando ya Ng'wanza!
 
Hakuna biashara inalipa mwanza kama ya bia ungefungua ka simple pub ingekuwa poa sana ila mtaji wako mdogo may be ununue boda boda hesabu kwa wiki 45000 mpaka 50000 inategemea atleast hapo unaweza jikwamua
 
asante ndugu kwa wiki 50000 kwa mwezi 200000 kwa mwaka 2400000 its reasonable nnaeza nkalipa ada kwa biashara ya boda boda thank"s ndugu!
 
asante ndugu kwa wiki 50000 kwa mwezi 200000 kwa mwaka 2400000 its reasonable nnaeza nkalipa ada kwa biashara ya boda boda thank"s ndugu!


Piga hiyo kitu dogo,,but at the back of your mind remember that your have a great load (MD)
 
asante ndugu kwa wiki 50000 kwa mwezi 200000 kwa mwaka 2400000 its reasonable nnaeza nkalipa ada kwa biashara ya boda boda thank"s ndugu!

kuwa mchuuzi wa samaki unawahi asubuhi unachukua samaki kwa wavuvi unapeleka sokoni au kwenye mahoteli au unafuata mpunga sengerema unaleta mwanza.
 
kuwa mchuuzi wa samaki unawahi asubuhi unachukua samaki kwa wavuvi unapeleka sokoni au kwenye mahoteli au unafuata mpunga sengerema unaleta mwanza.

kaka molembe mbona unaniponda mwanzo mwisho! hii dunia kaka unaijua leo yako but you know nothing about tomorrow! asante wote mlionipa mawazo positive
 
Jamani to be honest Cuhas imezidi gharama, wamediriki kupandisha hadi tuition's fee khaaa!!! Hivi hawa watu hawajui kuwa watu huchagua faculties za kuchukua kwa kuangalia gharama pia!!! ? Kaka luofe wahanga ni wengi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…