Mwanza: Wamachinga waandamana kutaka kupewa vizimba katika maeneo waliyopangiwa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Ni patashika. Ndivyo unavyoweza kuelezea mvutano kati ya wafanyabiashara wadogo jijini Mwanza na mamlaka ya Jiji hilo baada ya wafanyabiashara hao kuandamana leo Jumamosi Oktoba 23,2021 na kufunga barabara ya Nyerere eneo ya Voil kushinikiza kupewa vizimba kwenye maeneo rasmi.

Kundi la wafanyabiashara hao lilijumuisha walioondolewa katika mtaa wa Makoroboi na kuhamishiwa katika soko la Mchafu Kuoga na maeneo mengine ambayo ni rasmi kufanya biashara zao.

Athuman Makelele, aliyekuwa katika soko la Makoroboi ni miongoni mwa wafanyabiashara walioshiriki maandamano hayo huku akidai wamelazimika kuchukua hatua hiyo baada ya juhudi za kushinikiza viongozi wa Jiji kuwapangia maeneo yanayowatosha kugonga mwamba.

"Tumefika hapa asubuhi hakuna muafaka wowote kutoka kwa viongozi, tunapiga simu wamezima tukaona sasa tuzibe barabara ili waje watusikilize ikibidi watupangie maeneo yanatosheleza idadi yetu kama machinga," amesema Makelele

Naye Khalfan Mohammed amesema soko la Mchafu Kuoga ni finyu ikilinganishwa na idadi ya wafanyabiashara waliyoondolewa katika soko la Makoroboi.

"Hawa waliowahi wakapewa meza hapa sio waliyokuwa Makoroboi, sasa sisi tuliokuwa kule mjini tukaambiwa tuje hapa tumefika tukakuta watu wameshagawana maeneo yameisha," amesema Khalfan.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Amina Makilagi amesema amepokea malalamiko ya wafanyabiashara hao huku akiwataka kujiorodhesha majina yao kwa viongozi wao kwa ajili ya kupewa vizimba katika maeneo mengine.

"Ombi lenu limepokelewa , tutalifanyia kazi na kuwaletea majibu kupitia uongozi wenu, ninachowaomba andikeni majina kwa viongozi wenu ili tuweze kuwapangia maeneo rasmi," amesema Makilagi

Chanzo: Mwananchi
 
Shida ya nchi yetu ni kila mara kuleta tatizo na kulitatua na kulileta tena na kulitatua na kulileta tena...........yani huo mzunguko hauishi. Hao machinga wanaoondolewa sasa hivi tusishangae mwaka 2024 hadi 2025 wakarudishwa tena huko walipoondolewa, muda utaamua.
 
Huyo mama mkuu wa wilaya ni muongo muongo sanaa....kajaliwa sanaa maneno ya kuongea...tulikuwa kwny kikao hapo jiji yaan anayoongea ukimwangalia uson kwa makini unajua kabxa anawachora tu
 
Kwa wanawake kusema maneno mema na yasiyo tekelezeka ni kawaida ni kama mama yetu huyu . Hivi tuseme kwamba serikali imeshindwa kutengeneza mbinu sahihi na yenye kuondoa migongano ya watu katika utekelezaji wa sera ya kuwaondoa watu kwenye mazingira yasiyo rasmi?. Ndiyo wakaamua kuwaondoa nyakati za usiku kweli je wanajua mtu yule ndani Kwacha nini na aliondoka na kitu gani.
 
Nashauri mkoa wa mwanza ungegeuzwa kuwa soko la wamachinga nchini,
Yalipoanzia ndio yamalizikie huku kwengine tuacheni, tukihitaji kitu tutakuja mwanza si sgr ipo? 🤣
 
Nashauri mkoa wa mwanza ungegeuzwa kuwa soko la wamachinga nchini,
Yalipoanzia ndio yamalizikie huku kwengine tuacheni, tukihitaji kitu tutakuja mwanza si sgr ipo? 🤣
HHaha kwani hali ilikua mbaya sana? Sijaenda Mwz kitambo sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…