Mwanza: Watu watatu wa familia moja waliuawa kikatili, kwa kunyongwa na watu wasiojulikana

Mwanza: Watu watatu wa familia moja waliuawa kikatili, kwa kunyongwa na watu wasiojulikana

Goodluck Mshana

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2011
Posts
1,272
Reaction score
1,120
Usiku wa kuamkia leo jijini Mwanza, kata ya Buhongwa kumetokea mauaji ya kinyama. Mauaji hayo yamefanywa leo saa kumi usiku.

Watu watatu wa familia moja akiwemo Mtoto wa miezi saba (7) waliuwawa kikatili, kwa kunyongwa, ndani ya nyumba yao na watu wasiojulikana. Kwa habari za awali ni kwamba, watekelezaji wa mauji hayo walifanikiwa kuingia ndani ya nyumba hiyo pasi na kuvunja mlango.

Licha ya nyumba ya marehemu hao kuzungukwa na nyumba zingine. Hata hivyo hakuna aliyefanikiwa kutoka ama kusikia wakati unyama huo ukiendelea. Kila aliyeulizwa alisema hajui chochote juu ya tukio hilo. Mama na mtoto wa miezi 7 walinyongwa, baba akachinjwa!

Miili ya marehemu hao bado ipo ndani ya nyumba ikisubiri uchunguzi zaidi. Askari nao wamefika eneo la tukio na uchunguzi unaendelea.

Source: ITV Breaking News

My concern: Je, mtoto wa miezi 7 alikuwa na ugomvi na nani hadi na yeye kunyongwa?

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Ni habari mbaya sasa tutamalizana hivi
mpaka lini ? Hii ni aibu nyingine kama
ya wakati ule ya kuwauwa ndgzetu Albino.
 
Someone is behind this sio wizi tu hawawezi kuuwa mpaka kichanga hakina hata kosa lolote
 
Taifa au jamii ya watu waliokata tamaa utawajua kwa matendo yao, hili nalo ni dalili mojawapo ya hizo. Pale ndugu zetu Albino walivyotaka kumalizwa ni wachache waliojua kuwa hata hao tusio Albino tutageukana wenyewe kwa wenyewe. Habari mbaya sana!
 
Poleni sana ndugu mliopotelewa na ndugu zenu kwa kuuawa! Mungu awalaze mahali pema peponi.
Mshana, kama ungeweza kurushiamo na kapicha kidogo
 
Poleni sana ndugu mliopotelewa na ndugu zenu kwa kuuawa! Mungu awalaze mahali pema peponi.
Mshana, kama ungeweza kurushiamo na kapicha kidogo

Iwe olikyomasi!akashwahili nkakwangao!!
 
Dah! huu ni unyama wa hatari, hao wa2 inabidi watafutwe hata kwa rimote controll!, na ikibidi wanyongwe na wao!
 
Wewe siumesema mida ya saa 10 hapo hapo hakuna aliyesikia sasa umejuaje kama ndiyo mda huo walikuja hao waharibifu walio laaaniwa inasasikitisha POLEN WAHANGA
 
poleni wafiwa,Mungu azipumzishe roho za marehemu wote mahala pema peponi. AMINA
 
Taifa au jamii ya watu waliokata tamaa utawajua kwa matendo yao, hili nalo ni dalili mojawapo ya hizo. Pale ndugu zetu Albino walivyotaka kumalizwa ni wachache waliojua kuwa hata hao tusio Albino tutageukana wenyewe kwa wenyewe. Habari mbaya sana!

Tutafanyeje kuondokana na hali hii. Tuanze kwenye familia na ndugu zetu kuzunguzana na kusaidiana.
 
Wewe siumesema mida ya saa 10 hapo hapo hakuna aliyesikia sasa umejuaje kama ndiyo mda huo walikuja hao waharibifu walio laaaniwa inasasikitisha POLEN WAHANGA

lnategemea kabla ya tukio family ilikuwa na kina nani ama ilikuwa wapi...na hivyo kuwa rahisi kukadiria muda wa tukio.
 
Jamani inasikitisha

as sijasoma habari zaidi ya hii, kama wanafamilia walikuwa hao hao basi ni revenge kubwa ya mtu wa karibu au ni juu ya mali au mke/mume alikuwa na kitu cha dhamani au walijua kitu.

ila mpaka kuua baby mara nyingi ni revenge au mtu kuzuia kitu kama uzao wa mtu mmojawapo wa marehemu hao wasije wazuia kula watakacho later.

Ila mmh i hope sio mapenzi mtu aliachwa solemba

RIP
 
kuua hadi kitoto..! hayo ni mauaji ya kimbali. hivi hawakua na ugomvi na wahamiaji haramu kweli..? mbaya sana hii.
 
Jf jana ilikera. Niliona uzi "MAUAJI YA KUTISHA BUGARIKA MWANZA". Nilishikwa na simanzi nikafungua uzi sambamba na kuuliza wadau wangu wa mwanza wakiwamo askari polisi. Nilichoshuhudia, ni mtu anaelezea kisa cha mwaka 1994. Ambapo jamaa àlitoswa àkaamua kuuwa demu na wazazi wake na yeye kujimaliza. Sasa hata cjasahau upuuzi ule, leo inarushwa wanafamilia watatu. To bad
 
Inasikitisha sna hii, ila kuna kaharufu ka kisasi hapa, roho za marehemu zipumzike kwa amani!
 
Back
Top Bottom