Mwanzilishi wa Wikileaks Julian Assange aachiwa huru kutoka gereza la Belmarsh nchini Uingereza ambako amekaa kwa miaka 12

Mwanzilishi wa Wikileaks Julian Assange aachiwa huru kutoka gereza la Belmarsh nchini Uingereza ambako amekaa kwa miaka 12

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
1719284429628.png

Julian Assange akipanda ndege maalum kuelekea Saipan

Mwanzishi wa WikiLeaks Julian Assange ameachiwa huru usiku huu kutoka gereza la Belmarsh nchini Uingereza ambako amekaa kwa miaka 12. Bwana Assange alikuwa akikaa gerezani hapo akisubiri kupelekwa Marekani kujibu mashtaka ya ubakaji ambako alikuwa akituhumiwa alifanya nchini Sweden.

Miaka 12 ilopita Julian Assange alikimbilia ubalozi wa Ecuador uliopo nchini Uingereza baada ya tuhuma hizo kutolewa na pia kuwepo kwa tuhuma zingine kutoka Marekani ambayo imekuwa ikimtuhumu kudukua taarifa za siri ambapo video ilionyesha wanajeshi wa Marekani wakifanya uhalifu wa kivita nchini Irak.

Kwa mujibu wa taarifa ilotolewa na kundi la siri la wadukuaji kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), Assange ameondokea uwanja wa ndege wa Stanstead uliopo mashariki mwa jiji la London na muda si mrefu atakutana na mkewe Stella Assange na watoto wao wawili ambao hwakuwahi kukaa na baba yao nyumbani.

Ndege hiyo itatua mjini Bangkok nchini Thailand kabla ya kuelekea mjini Saipan.

Hapo chini ni barua ya waendesha mashtaka wa Marekani wakielekeza mkutano wao na Juliana Assange mjini Saipan katika kisiwa cha Mariana. Kisiwa hichi chamilikiwa na Marekani na hakipo mbali kutoka nchi Australia ambako Assange alizaliwa.

1719285004249.png

Vyanzo vya habari hii: Reuters, EPA, AP , CNN na media outlets.

Julian Assange ni nani?

1719299044294.png

Julian Assange akiwa nje ya jengo la ubalozi wa Ecuador mjini London mwaka 2016. Picha na AP ilochapishwa na gazeti la The Standard.

Julian ni mhariri wa habari za kiuchunguzi, mwanaharakati na pia ni mchapishaji. Alizaliwa nchini Austalia mwaka 1971 na ni mwanzilishi wa mtandao wa WikiLeaks ambao ulianza rasmi shughuli zake mwaka 2006.

Julian ameishapokea tuzo kadhaa za uandishi wa habari na uchapishaji lakini ni mwaka 2010 ndipo alipokuja kujulikana kimataifa kwa kazi zake pale mtandao wake wa WikiLeak ulipochapisha nyaraka za siri kutoka Pentagon makao makuu ya jeshi la Marekani.

Nyaraka hizo zilionyesha video zilohusu majeshi ya Marekani kuwaua raia waso na hatia katika nchi za Afghanistani na Irak na pia mateso walokuwa wakiyapata wafugwa wa kigeni katika kambi ya Guantanamo.

Pia mtandao huo ulichapisha mawasiliano mbalimbali ya siri kati ya viongozi wa serikali ya Marekani na nchi zingine kadhaa ulimwenguni ikiwemo taarifa ya mauaji ya kisiasa nchini Kenya mwaka 2008 ambayo yalichapishwa na gazeti la Sunday Times.

Misukosuko dhidi ya Assange ilianza na nchi ya Sweden kutoa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa Assange ili kupelekwa Sweden kukabili mashtaka ya kumshambulia kimwili mwanamke mmoja wa nchi hiyo. Bwana Assange alijaribu kupinga hati hiyo ya kukamatwa na akashindwa jambo lilomfanya mwezi Juni mwaka 2012 akimbilie ubalozi wa Ecuador ulioko London nchini Uingereza ambako baadae mwezi wa August mwaka huohuo alipata hifadhi ya kisiasa.

Baadae mwaka 2019 nchi ya Sweden aliondoa mashtaka yalomkabili Assange na mwezi April mwaka huohuo Ecuador ikaondoa hadhi ya ukimbizi alokuwa nayo jambo lilowapa uwezo polisi wa Uingereza kuingia ubalozini humo na kumkamata Assange na kupelekwa gereza la Belmarsh akisubiri kupelekwa Marekani kujibu mashataka ya kudukua nyaraka za siri katika mifumo ya kompyuta ya Pentagon kupitia mwanajeshi alieitwa Chelsea Manning ambae alikuwa ni mchambuzi wa ujasusi wa jeshi la Marekani.

Assange ana kipaji cha udukuzi yaani "hacking" ambapo alianza shughuli hizo za udukuzi akiwa na umri wa miaka 16. Mwaka 1988 alitumia uhandisi jamii (kumrubuni mtu ataekusadia kazi) kudukua taarifa kutoka kamisheni ya mawasiliano ya Australia bila kuharibu mifumo yake ya Kompyuta..

Mwaka 1991 gazeti la he Guardian la Uingereza lilimpa sifa ya kuwa mdukuzi aliejitosheleza yaani "The most accomplished hacker" na hadi hapo tayari alikuwa amedukua mifumo zaidi ya elfu moja ikiwemo mifumo ya kompyuta ya Pentagon.

PIA, SOMA:
 
Hapo watamthibiti sana na kumtrack mpaka chooni. Hawawezi kukubali jamaa awe Snowden mwingine.
Wataangalia hukumu itayolingana na miezi alokaa gerezani (miezi 62) akisubiri extradition na akiachiwa ataingia Australia.

Kwa kuwa amekubali mashtaka kupitia "plea deal bargain" jaji wa mahakama kuu akikubali na ikikubalika (hiyo plea bargain yake) basi atapewa alama nzuri yaani "good credit" ambayo itampa haki ya kuachiwa huru moja kwa moja.
 
JULIAN ASSANGE IS FREE

Julian Assange is free. He left Belmarsh maximum security prison on the morning of 24 June, after having spent 1901 days there. He was granted bail by the High Court in London and was released at Stansted airport during the afternoon, where he boarded a plane and departed the UK.

This is the result of a global campaign that spanned grass-roots organisers, press freedom campaigners, legislators and leaders from across the political spectrum, all the way to the United Nations. This created the space for a long period of negotiations with the US Department of Justice, leading to a deal that has not yet been formally finalised. We will provide more information as soon as possible.

After more than five years in a 2x3 metre cell, isolated 23 hours a day, he will soon reunite with his wife Stella Assange, and their children, who have only known their father from behind bars.

WikiLeaks published groundbreaking stories of government corruption and human rights abuses, holding the powerful accountable for their actions. As editor-in-chief, Julian paid severely for these principles, and for the people's right to know.

As he returns to Australia, we thank all who stood by us, fought for us, and remained utterly committed in the fight for his freedom.
Screenshot_20240625_064936_X.jpg
 
Wataangalia hukumu itayolingana na miezi alokaa gerezani (miezi 62) akisubiri extradition na akiachiwa ataingia Australia.

Kwa kuwa amekubali mashtaka kupitia "plea deal bargain" jaji wa mahakama kuu akikubali na ikikubalika (hiyo plea bargain yake) basi atapewa alama nzuri yaani "good credit" ambayo itampa haki ya kuachiwa huru moja kwa moja.
Nashukuru sana kwa ufafanuzi huu, jamaa amepambana sana na mikono ya kisheria kila upande.
 
Ni swala la muda tu sasa. Huyu jamaa marekani kupitia vyombo vyake vya kijasusi watammaliza.
Hakuna kitu kama hicho.

Serikali ya Australia ndo imekuwa ikifanya kampeni ya kumrudisha nyumbani Assange ambae raia wake.

Hili suala likiisha kesho basi baadae ataondoka na kuelekea Australia kuungana na familia yake.

Taarifa zasema ndege ilombeba Assange ndo imeruka usiku huu kuondoka Bangkok kuelekea Saipan.
 
Updates: Assange atua salama mjini Canberra, Australia.

Julian Assange ametua salama mjini Canberra nchini Australia asubuhi ya leo baada ya kumalizana na mahakama ya kijeshi ilioko mjini Saipan.

Assange alipokelewa na mkewe Stella watoto wake wawili, ndugu jamaa na marafiki.

1719408057024.png

Julian Assange akimbusu mkewe Stella mara baada ya kutua mjini Canberra nchini Australia leo asubuhi. Picha na Reuters.

Asubuhi ya leo aliingia mahakamani kuonana na jaji katika kisiwa cha Mariana kilichoko kaskazini ya bahari ya Pasific ambacho kimo ndani ya himaya ya Marekani.

Assange amekiri kosa moja tu kati ya makosa 17 alokuwa akishtakiwa yakiwa ni kuiba siri za kijeshi au "Espionage". Kosa hilo ni kuingilia taratibu na sheria ya ujasusi wa ndani "Espionage" yaani Espionage Act na jaji kutia hatiani kwa adhabu ambayo tayari ametumikia nchini Uingereza katika gereza la Belmarsh ambako amekaa kwa miaka mitano.

Akizungumza baadae mwanasheria wa Assange Barry Pollack amesema kwa sasa familia ya Assange yaomba ipewe nafasi na faragha hadi hapo Assange mwenyewe atapokuwa tayari kuongea.
 
Updates: Assange atua salama mjini Canberra, Australia.

Julian Assange ametua salama mjini Canberra nchini Australia asubuhi ya leo baada ya kumalizana na mahakama ya kijeshi ilioko mjini Saipan.

Assange alipokelewa na mkewe Stella watoto wake wawili, ndugu jamaa na marafiki.

View attachment 3026693
Julian Assange akimbusu mkewe Stella mara baada ya kutua mjini Canberra nchini Australia leo asubuhi. Picha na Reuters.

Asubuhi ya leo aliingia mahakamani kuonana na jaji katika kisiwa cha Mariana kilichoko kaskazini ya bahari ya Pasific ambacho kimo ndani ya himaya ya Marekani.

Assange amekiri kosa moja tu kati ya makosa 17 alokuwa akishtakiwa yakiwa ni kuiba siri za kijeshi au "Espionage". Kosa hilo ni kuingilia taratibu na sheria ya ujasusi wa ndani "Espionage" yaani Espionage Act na jaji kutia hatiani kwa adhabu ambayo tayari ametumikia nchini Uingereza katika gereza la Belmarsh ambako amekaa kwa miaka mitano.

Akizungumza baadae mwanasheria wa Assange Barry Pollack amesema kwa sasa familia ya Assange yaomba ipewe nafasi na faragha hadi hapo Assange mwenyewe atapokuwa tayari kuongea.
Kuisha kwa hili sakata tunalingojea kwenye move sasa😀😀
 
Plea bargaining ndo imemtoa. Na hatujui amekubaliana nini na US. Pia, haruhusiwi kwenda US bila kibali. Yotekwayote US Yuko vitani anahitaji akina Assange wengi Sasa hivi.
 
View attachment 3025288
Julian Assange akipanda ndege maalum kuelekea Saipan

Mwanzishi wa WikiLeaks Julian Assange ameachiwa huru usiku huu kutoka gereza la Belmarsh nchini Uingereza ambako amekaa kwa miaka 12. Bwana Assange alikuwa akikaa gerezani hapo akisubiri kupelekwa Marekani kujibu mashtaka ya ubakaji ambako alikuwa akituhumiwa alifanya nchini Sweden.

Miaka 12 ilopita Julian Assange alikimbilia ubalozi wa Ecuador uliopo nchini Uingereza baada ya tuhuma hizo kutolewa na pia kuwepo kwa tuhuma zingine kutoka Marekani ambayo imekuwa ikimtuhumu kudukua taarifa za siri ambapo video ilionyesha wanajeshi wa Marekani wakifanya uhalifu wa kivita nchini Irak.

Kwa mujibu wa taarifa ilotolewa na kundi la siri la wadukuaji kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), Assange ameondokea uwanja wa ndege wa Stanstead uliopo mashariki mwa jiji la London na muda si mrefu atakutana na mkewe Stella Assange na watoto wao wawili ambao hwakuwahi kukaa na baba yao nyumbani.

Ndege hiyo itatua mjini Bangkok nchini Thailand kabla ya kuelekea mjini Saipan.

Hapo chini ni barua ya waendesha mashtaka wa Marekani wakielekeza mkutano wao na Juliana Assange mjini Saipan katika kisiwa cha Mariana. Kisiwa hichi chamilikiwa na Marekani na hakipo mbali kutoka nchi Australia ambako Assange alizaliwa.


Vyanzo vya habari hii: Reuters, EPA, AP , CNN na media outlets.

Julian Assange ni nani?

View attachment 3025454
Julian Assange akiwa nje ya jengo la ubalozi wa Ecuador mjini London mwaka 2016. Picha na AP ilochapishwa na gazeti la The Standard.

Julian ni mhariri wa habari za kiuchunguzi, mwanaharakati na pia ni mchapishaji. Alizaliwa nchini Austalia mwaka 1971 na ni mwanzilishi wa mtandao wa WikiLeaks ambao ulianza rasmi shughuli zake mwaka 2006.

Julian ameishapokea tuzo kadhaa za uandishi wa habari na uchapishaji lakini ni mwaka 2010 ndipo alipokuja kujulikana kimataifa kwa kazi zake pale mtandao wake wa WikiLeak ulipochapisha nyaraka za siri kutoka Pentagon makao makuu ya jeshi la Marekani.

Nyaraka hizo zilionyesha video zilohusu majeshi ya Marekani kuwaua raia waso na hatia katika nchi za Afghanistani na Irak na pia mateso walokuwa wakiyapata wafugwa wa kigeni katika kambi ya Guantanamo.

Pia mtandao huo ulichapisha mawasiliano mbalimbali ya siri kati ya viongozi wa serikali ya Marekani na nchi zingine kadhaa ulimwenguni ikiwemo taarifa ya mauaji ya kisiasa nchini Kenya mwaka 2008 ambayo yalichapishwa na gazeti la Sunday Times.

Misukosuko dhidi ya Assange ilianza na nchi ya Sweden kutoa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa Assange ili kupelekwa Sweden kukabili mashtaka ya kumshambulia kimwili mwanamke mmoja wa nchi hiyo. Bwana Assange alijaribu kupinga hati hiyo ya kukamatwa na akashindwa jambo lilomfanya mwezi Juni mwaka 2012 akimbilie ubalozi wa Ecuador ulioko London nchini Uingereza ambako baadae mwezi wa August mwaka huohuo alipata hifadhi ya kisiasa.

Baadae mwaka 2019 nchi ya Sweden aliondoa mashtaka yalomkabili Assange na mwezi April mwaka huohuo Ecuador ikaondoa hadhi ya ukimbizi alokuwa nayo jambo lilowapa uwezo polisi wa Uingereza kuingia ubalozini humo na kumkamata Assange na kupelekwa gereza la Belmarsh akisubiri kupelekwa Marekani kujibu mashataka ya kudukua nyaraka za siri katika mifumo ya kompyuta ya Pentagon kupitia mwanajeshi alieitwa Chelsea Manning ambae alikuwa ni mchambuzi wa ujasusi wa jeshi la Marekani.

Assange ana kipaji cha udukuzi yaani "hacking" ambapo alianza shughuli hizo za udukuzi akiwa na umri wa miaka 16. Mwaka 1988 alitumia uhandisi jamii (kumrubuni mtu ataekusadia kazi) kudukua taarifa kutoka kamisheni ya mawasiliano ya Australia bila kuharibu mifumo yake ya Kompyuta..

Mwaka 1991 gazeti la he Guardian la Uingereza lilimpa sifa ya kuwa mdukuzi aliejitosheleza yaani "The most accomplished hacker" na hadi hapo tayari alikuwa amedukua mifumo zaidi ya elfu moja ikiwemo mifumo ya kompyuta ya Pentagon.

PIA, SOMA:
Mke wake baada ya kuanzisha kampeni ya kuchanga pesa ya private jet na gharama za kumsafirisha, jamaa mmoja ambaye hajulikani alimchangia bitcoin 8 ambazo ni sawa na dola laki 5.
 
Back
Top Bottom