Mwanzo mgumu lakini mvumilivu hula mbivu

Ngosha hongera kakangu.yani adi nalitamani hilo shamba.Tufundishe na sie kilimo cha pilipili.
 
Kwa kuwa umejitahidi kuthubutu, nakupa maswali machache uyajibu. Majibu yake yanaweza kusaidia kupata wajasiliamali wengine kama wewe kwenye forum. Na hapo utaweza kuonekanan umefaulu zaidi.
1. Gharama ya green houce moja ni kiasi gani, na kwa uzoefu wako msimu mmoja unachukua siku ngapi? Mavuna unapata kiasi gani kwa green house.
2. Unaonekana kyumia drip irrigation. Gharama za kuingiza drip irrigation in kiasi gani?
3. Tafadhalii baada ya hapo piga gharama za uzalishaji ili uone profit, return on capital kama vipo poa
 


na kwa kuongezea tu,
me ningependa wana mahesabu mtusaidie ku calculate hiyo return on investment ni ya muda gani..
I mean hiyo capita mtu utakayoanzanayo na baada ya muda gani nitaanza kula faida.
Maana kuna watu wanapenda una invest leo then kesho uanze kupata faida.... lazima uvumilie kwanza
 
Hongera sana ndugu kweli ni darasa tosha, imetutia moyo tusiojua mashamba. Keep it up
 
naona kama picha za 2011 hivi na hii post ni ya leo so sijui zikojezikoje hizi
 
Mkuu ngosha naomba tuwasiliane walau nije kutembelea shamba lako nijifunze kwa utekelezaji zaidi. Please if you can PM me your contacts I would be appreciative

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
hiyo green house mbona ni kama niliwahi kuitembelea.. huo mradi unafadhiliwa na serikali ya japan.. na mbele ya hiyo house naona pia bendera ya marekani.. ujawaibia vijana
 
nafikiri kuna kauongo ndani ya hii post samahani kama nitakuwa nimekukwaza
 
Ngoshas kama ni kweli nakupa big up sana. Ni wachache wenye uthubutu kama wako. Ila kwenye hiyo green house pamoja na maeneo yanayoizunguka inaonekana kama kwenye maonyesho fulani hivi!! Naona vibao vinavyoonyesha aina ya mimea iliyooteshwa pamoja na bango kwenye hiyo GH, au ulikuwa na ugeni?? Nikupe hongera, ila usisahau kujibu maswali ya wadau kwa faida ya wengi, mimi mmojawapo.
 
Mkuu hongera sana na ni mfano mzuri wa kuigwa...God bless you!



 
big up kaka me naomba unipe mbinu ulizo2mia mpaka kufikia hapo ulipo.
 
KWANZA HONGERA MKULU KWA KUTHUBUTU NA PIA KULETA ISHU APA ILI ATA WALE WALIKUWA WANASITASITA SASA WAANZE MARA MOJA, na wengine tunaoendelea virearchi bubu tuelimike zaidi.
This thing is possible hususan ukipata ile mbegu ya nyanya ambayo inazaa daima (miezi zaidi ya sita).
katika robo eka unavuna kilo zaida ya elf25 kwa semi intensive technology kama ya uyu bwana au had kilo elfu60 kwa intensive technology ya kiyahudi (ipo kenya kwa amrani) google utaipata au Kenya agricultura department.
Kiukweli nafanya utafiti lakini kwa mahesabu ya haraka haraka inaonyesha inalipa.
kwa mfano
uko na shamba, karibu na mto au umechimba kisima.
na alafu umenunua iyo nylon toka kwa wenye mashamba ya maua ambayo ni used (kwa kawaida itatumika tena miaka kama mitatu ivi).
mbegu aina ya anna inapatikana kenya kimfuko cha eka 2 ni sh elf 70 ya tz.
inapandwa miche kama alfu ivi.
inazaa kilo 25-30 kila mche.
uuzaji wa jumla kilo sh 600 x 25,000 x miaka mitatu = 45,000,000 gharama kubwa ni kuanza baada ya hapo kuna gharama ndogo ndogo na inabidi kila siku ujue maendelea ya nyanya kama daktari anavoangalia mgonjwa.
kama huna shamba ingia ubia na wenye mashamba karibu na mji.
kule kenya iyo green house kit inagharimu kama mil4.5 kwa pesa ya tz plus elimu na inputs zingine kama mbolea na irrigation kiti ambayo ni ya gravity.
kama utapanga mambo yako vizuri benki ya equity nasikia wanatoa mkopo kwa sababu wanajua inalipa.
 
Mungu kasaidia mwaka huu nimefanikiwa kujenga greenhouse, nashukuru Mungu malengo yangu yameanza kutimia.
Hizo picha zina tarehe 8/2/2011.

Tuwekee za kwako hili iweze kutuhamasisha wengi na kukupa pongezi zaidi.
 
mwezi wa 11/2012 cpigi picha kila nikienda
 
Mkuu ngosha naomba tuwasiliane walau nije kutembelea shamba lako nijifunze kwa utekelezaji zaidi. Please if you can PM me your contacts I would be appreciative

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Tuwasiliane kuanzia feb 2013, ijumaa hii naenda zenji kurudi feb
 
hiyo green house mbona ni kama niliwahi kuitembelea.. huo mradi unafadhiliwa na serikali ya japan.. na mbele ya hiyo house naona pia bendera ya marekani.. ujawaibia vijana

Nimekuwekea picha hapo juu, vilevile naomba nikupeleke ukaone shughuli inayofanyika, ucjali usafiri ntakupatia
 

Nimepost picha hapo juu, nafikiri utakuwa umeiona, matayarisho ya kupanda nyanya nov 2012
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…