La hasha, mazoezi alikua anafanya viwanja vya chuo pale na sio ubungo bus station, kariakoo shimoni, manzese darajani au uwanja wa taifa.
1) Bila haka kadegree sidhani kama ningepata nafasi ya kuja huko Dar kwanza kujumuika na mijianaume ya huko ningeendelea tuu kubaki mkoani kwetu kufanya mambo mengine kwa sababu siwezi kukaa kwa mashemeji.
2) kwa ambao walipata wasaa wa kupitapita pale UDSM nadhani wanajua mazingira halisi yalivyo pale, bila haka kadegree chances labda ningekua mtuu wa mazoezi kuhudhuria kule uwanjani au labda Kama ningeajiriwa Kama mkata nyasi kule viwanjani.
3) Pia mara hizo chache nilizokua namuona huyo bwana, ni vile tuu nilikua na vipindi vya jioni vya workshop, workshops ambazo zipo jirani kabisa na uwanja kwa hiyo baada ya kipindi nilikua natelemka zangu uwanjani kuangalia misambwanda ya wamama na wadada wanaofanya mazoezi ndio nilikua namuona huyo jibaba labda ningekua natumia mdaa wangu college nyengine huenda nisingemuona huyo mtuu.
Nadhani tumeelewana mkuu, siku njema mungu akubaliki Sana.