Mwarabu hakuwahi kuweka National Park Tanzania, kwa nini?

Mwarabu hakuwahi kuweka National Park Tanzania, kwa nini?

Kumbuka Mwarabu alifika ardhi yetu ikiwa bikra, yani ilikuwa ni misitu na wanyama tu, unaambiwa enzi hizo msitu ulikuwapo hadi hapo kisutu, yani simba walikuwa wapo hadi magomeni, chui wapo hadi kigamboni, papa wapo hadi fukwe za mbezi beach, chatu wapo hadi Msasani, sasa kwa msingi huo national park za nini na ilibidi ardhi itumike kufanya mazingira bora ya kuishi, kumbuka binadamu sio mnyama pori.

Na hili ndio nchi zinazojielewa wanapambana sana kurudisha Hali hiyo na kuishi na wanyama au ndege na viumbe wa bahari

Kuna samaki walipotea kabisa karibu na miji kwa sababu ya watu kuendeleza kelele na fujo baharini na misitu kukatwa miti hovyo hivyo kusababisha wanyama kuhama au kufa pia ndege wengi wamehama pia

Mfano mdogo leo ukienda New York wale dolphin [emoji227] wamerudi kwa kasi kwa sababu wameweka restrictions nyingi sana baharini mpaka sasa na wale humpback [emoji229] wameonekana pia ambapo ni jambo la ajabu sana

Yaani unasimama NY leo unaona Nyangumi
Sasa hata Sisi tunaweza kuwa na hifadhi karibu na tukawapa heshima wanyama kwa kuishi bila bughudha

Kwanza sidhani hata kama kuna takwimu zinaonyesha ni ndege aina ngapi wamepotea Tanzania na kuisha kabisa au hata wanyama aina ngapi wametoweka au kuisha kabisa

Nakumbuka Egypt kuna kasa wadogo walikuwa wanaliwa sana mpaka wakawa extinctions kabisa kasoro tu waliobaki Zoo
Hivyo wazungu wakawaomba wawachukue na kwenda kuwakuza na kuzaliana kwenye hifadhi maalumu
Wamekuwa wengi na kuwarudisha tena Misri
 
Kabla ya ukoloni wa wazungu Mwarabu alitawala Zanzibar na Pwani ya Mashariki kuanzia Sofala ya Msumbiji hadi Kismayu Somalia

Pia alikuwa akifika hadi Congo kuchukua Watumwa na pembe za ndovu, na akikuwa na vituo vya biashara huko Tabora na Kigoma

Kasome Historia
Unachanganya madesa, kipindi hicho kulikuwa na hitaji la kutenga maeneo kama hifadhi, walikuwa na teritorial mandate? Je mazingira ya mwaka 1840 kurudi nyuma kabla ya mkutano wa berlin ambapo ujerumani ilikabidhiwa tanganyika.
Hitaji la kuwa na hifadhi za taifa na mapori tengefu limetokana na nini?
Achana na historia zako uchwara, jikite kwenye land ordinances & laws ,reforms na wildlife management reforms.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Miongoni mwa Mambo natamani yafutwe kwenye elimu yetu ni kusoma historia za kikoloni, sijui tulitawaliwa na nan, hii mentality inaenda vizazi na vizazi na ndio maana tunaendelea kuwanyenyekea wakoloni walewale

Kuna msemo those who don’t learn from History are doomed to repeat it, Historia ni muhimu vinginevyo utakuwa Mtumwa kama tulivyo sasa hivi, hata hatujuelewi, tunauza nchi yetu kwa Mzungu, Mwarabu, Muhindi au Mchina, tuko so kind kwa kila mtu isipokuwa mtu mweusi mwenzetu, …
 
Mwarabu hajawahi kutawala Tanganyika.Mtawala wa kwanza wa Tanganyika ni mjerumani,mjerumani akamwachia mngereza,kutawala.Hivi huko shule ulikwenda somea nini?Ambapo hujui,hata watawala waliotawala Tanganyika.
Mjerumani ndie aliyeijenga TANZANIA
 
Mwarabu hajawahi kutawala Tanganyika.Mtawala wa kwanza wa Tanganyika ni mjerumani,mjerumani akamwachia mngereza,kutawala.Hivi huko shule ulikwenda somea nini?Ambapo hujui,hata watawala waliotawala Tanganyika.

MKuu Tanganyika karibu yote ilikua ni sehemu ya Zanzibar ya asili kabla kumegwa na wazungu
 
Mwarabu ni jamii ya waharibifu..weka mbali na wanyama pori.

#MaendeleoHayanaChama
 
Walikuwepo miaka yote, walieneza Dini ya Uislamu na utamaduni wao ndicho pekee walichoacha, lakini kwa nini hawakuwahi kuunda National Park ?
Jiunge kisomo cha watu wazima chalii,lini Tanganyika ilikuwa koloni la Mwarabu?
Hata hivyo kuna hazina kubwa kuliko yote wamessidia kuwepo ni lugha ya Kiswahili, huwezi kuaandika sentensi hata moja iziyokuwa na neno lililo toholewa kwenye Kiarabu
Mwisho wajua maana ya ustaArabu
 
Back
Top Bottom