TANZIA Mwasisi wa Mapinduzi Zanzibar, Mzee Hassan Nassor Moyo afariki dunia

TANZIA Mwasisi wa Mapinduzi Zanzibar, Mzee Hassan Nassor Moyo afariki dunia

Mwanasiasa mkongwe na mwasisi wa Mapinduzi Zanzibar, Hassan Nassor Moyo amefariki usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake mkoani Tanga

Mzee Moyo ambaye pia ni Waziri Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa pia aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano #Zanzibar

Inna lillah wainna ilayhi rajiuna.



======

Mzee Moyo alikuwa mwanachama wa Chama cha Afro Shirazi (ASP) tangu kilipoanzishwa Februari 5, 1957 baadaye Februari 5, 1977 akajiunga na chama cha Mapinduzi akiwa na kadi namba 7.

Mzee Moyo ndiye alikuwa Mratibu Mkuu wa Maridhiano ya Zanzibar ya Novemba 5, 2009 yaliyowakutanisha Rais Mstaafu wa Zanzibar (awamu ya sita), Dk Aman Abeid Karume na Maaalim Seif Sharif Hamad katika kutafuta mbinu ya kuondoa tofauti iliyokuwepo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010.

Mzee Hassan Nassor Moyo alivuliwa uanachama wa chama cha mapinduzi CCM, hatua iliyofikiwa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa wa Magharibi, Unguja viswani Zanzibar

Mada mbalimbali zinazomhusu Mzee Moyo

- Mzee Hassan Nassor Moyo: Kauli yake juu ya Muungano na hatma ya Uanachama wake ndani ya CCM
- CCM yamvua Uanachama Mzee Hassan Nassor Moyo
- RAI: MASWALI na MAJIBU; HASSAN Nassor Moyo: Sio rahisi kuuvunja Muungano huu
Ni msiba mkubwa kwa Familia yake maana siku 12 zilizopita amefariki mtoto wake wa kiume ,ambaye pia alisemekana sana kuwa ni kipenzi chake.
Allah awape subra familià ya mzee Hassan Nasoro Moyo.
 
Mwanasiasa mkongwe na mwasisi wa Mapinduzi Zanzibar, Hassan Nassor Moyo amefariki usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake mkoani Tanga
Duh...!.
Huyu ndiye shuhuda pekee wa kusainiwa muungano wetu adhimu, aliyebaki kuwa hai.
Kifo hiki maana yake mashuhuda wote wa kusainiwa kwa The Articles of The Union Between Tanganyika and Zanzibar, wametangulia mbele ya haki.
Iwapo CCM itashindwa Zanzibar, Nini Majaaliwa ya Muungano?
RIP Mzee Hassan Nassor Moyo.
Inna lillah wainna ilayhi rajiuna

P
 
RIP! Naomba kuuliza , kwake ni Tanga, halafu akwa mwasisi wa siasa za Zanzibar, kwa vipi?
Mbona Hussein mwinyi kwako ni ukerewa lkn kapitishwa Dodoma aje agombanie urais Zanzibar kwahiyo Tanganyika ndio wanavo itawala zanzibar
 
Huwa mnakasi ya kipanga kupost nyuzi sijui kwa sababu gani tu!

Picha ina sura mbili, sasa nani ndiyo nani?

Ukiamua kuhabarisha umma, jitahidi kudhibiti maswali yanayojengwa juu ya maswali kwa kuifafanua mada na kuweka wasifu wa mhusika.

Acha hizo hata kama umeamka vibaya. Mzee picha inaonesha dhahiri ni nani hapo. Huyo nzee mwingine nywele kapaka black ni kijana.
Mzee Moyo kaumaliza mwendo, apumzike kwa amani. Pole kwa ndugu, jamaa na marafiki.
 
Mbona Hussein mwinyi kwako ni ukerewa lkn kapitishwa Dodoma aje agombanie urais Zanzibar kwahiyo Tanganyika ndio wanavo itawala zanzibar
Ok, wenzako wanasema huku ni kwa kuishi tu! nakubaliana nao kabisa
 
Mwanasiasa mkongwe na mwasisi wa Mapinduzi Zanzibar, Hassan Nassor Moyo amefariki usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake mkoani Tanga

Mzee Moyo ambaye pia ni Waziri Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa pia Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar

Inna lillah wainna ilayhi rajiuna.



======

Mzee Moyo alikuwa mwanachama wa Chama cha Afro Shirazi (ASP) tangu kilipoanzishwa Februari 5, 1957 baadaye Februari 5, 1977 akajiunga na chama cha Mapinduzi akiwa na kadi namba 7.

Mzee Moyo ndiye alikuwa Mratibu Mkuu wa Maridhiano ya Zanzibar ya Novemba 5, 2009 yaliyowakutanisha Rais Mstaafu wa Zanzibar (awamu ya sita), Dk Aman Abeid Karume na Maaalim Seif Sharif Hamad katika kutafuta mbinu ya kuondoa tofauti iliyokuwepo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010.

Mzee Hassan Nassor Moyo alivuliwa uanachama wa chama cha mapinduzi CCM, hatua iliyofikiwa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa wa Magharibi, Unguja viswani Zanzibar

Mada mbalimbali zinazomhusu Mzee Moyo

- Mzee Hassan Nassor Moyo: Kauli yake juu ya Muungano na hatma ya Uanachama wake ndani ya CCM
- CCM yamvua Uanachama Mzee Hassan Nassor Moyo
- RAI: MASWALI na MAJIBU; HASSAN Nassor Moyo: Sio rahisi kuuvunja Muungano huu
Poleni ndugu,jamaa na marafiki.
 
Poleni wafiwa. Hata Shein naye akimaliza kutawala Zanzibar atarudi nyumbani kwake bara. Na sasa Hussein Mwinyi anatafuta kutawala Visiwani, akimaliza arudi nyumbani kwake bara!
 
Back
Top Bottom