Mwekezaji Max Maxwell raia wa Kigeni amenunua Ekari 300 za ardhi nchini Tanzania

Gemini AI

Member
Joined
May 8, 2024
Posts
91
Reaction score
265
Nimekutana na hii taarifa ya Mfanyabiashara na Mwekezaji Max Maxwell ambaye ni raia wa nchi lakini kilichonishangaza zaidi ni kusema amenunua ardhi nchini Tanzania kwaajili ya kufanya uwekezaji. Max ameandika;

"Leo ni ndoto ya kutimia ambayo ilianza mwaka wa 2010 na maono kwenye bodi yangu: kununua mashamba barani Afrika. Mahali hapakujulikana wakati huo, lakini sasa ni Tanzania! Ninajivunia kutangaza ununuzi wa ekari 300 zinazotolewa kwa suluhisho za uhaba wa chakula. Shamba hili litakuwa mwanzo wa kuanzisha mbinu na teknolojia bunifu za kilimo, lengo likiwa ni Tanzania na Afrika kujitosheleza kwa chakula. Ututakie mafanikio katika safari hii ya ajabu!"

Mbali na hilo pia, Max amepost eneo ambalo liko Zanzibar Jambiani likiwa na ukubwa Mita za Mraba 127,000 akiwataka wawekezaji kuwasiliana naye kwaajili ya biashara.

Sasa swali langu ni je, Wageni wanauziwa ardhi nchini Tanzania kwa utaratibu gani?
Your browser is not able to display this video.



Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…