Mwekezaji wa Simba SC, Mohammed Dewji, Awaonesha Mashabiki Ramani Mpya ya Mo Simba Arena

Mwekezaji wa Simba SC, Mohammed Dewji, Awaonesha Mashabiki Ramani Mpya ya Mo Simba Arena

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mwekezaji wa Simba SC Mohammed Dewji (MO), amewaonesha Wapenzi na Mashabiki wa Simba ramani mpya ya Mo Simba Arena akisema huo ni mradi mkubwa ambao utaweka msingi wa mafanikio ya Club hiyo baadaye.
IMG_0083.jpeg

Akiongea leo October 06,2024 kwenye Mkutano Mkuu wa Club hiyo, Mo Dewji amesema "Hii ni ramani mpya ya Mo Simba Arena, mradi mkubwa ambao utaweka msingi wa mafanikio yetu baadae, tunatarajia kujenga kambi bora ya mazoezi itakuwa na gym, majengo ya malazi, kituo cha lishe, bwala la kuogolea, kituo cha burudani, viwanja vitano vya kisasa zaidi ya hayo kujenga makumbusho ya klabu na kuanzisha chuo cha maendeleo ya Vijana ili kulea vipaji vya soka Nchini"

"Ili kufanikisha yote haya tunasubiri mchakato wa mabadiliko ya Simba kukamilika, tuko katika hatua za mwisho, ujenzi wa miundombinu hii unakuja na gharama kubwa, ni ngumu kuanza huu ujenzi bila mfumo kubadilika"



Pia, Soma:

PICHA: MO Dewji na Mangungu washikana mikono kwa mara ya kwanza
Hotuba ya Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi Simba SC Mo Dewji kwenye mkutano mkuu wa Club 2024
 
Uwanja wa KMC umejengwa na municipal ya kinondoni Sio na club ya mpira /KMC
Simba na Yanga ni taasisi hazishindwi ku raise fund ya kujenga hivyo viwanja hata kutafuta wawekezaji wakaweka hela wakajenga viwanja haishindikani tatizo ni serikali yenyewe tu. Mbona Arsenal ilipata Wawekezaji wa Emirates wakajenga ule uwanja wao ?
 
Hivi Mo hawezi kufanya chochote Simba bila kutanguliza jina lake?
Gunners mwenzangu kuna timu inaitwa Chelkenge haina kiwanja badala yake ina haki za kutumia jina. Sawa na Milan na Inter.

Kibiashara hana kosa kabisa kwa kua na haki ya kutanguliza jina analoona linamfaidisha kibiashara.
 
Simba na Yanga ni taasisi hazishindwi ku raise fund ya kujenga hivyo viwanja hata kutafuta wawekezaji wakaweka hela wakajenga viwanja haishindikani tatizo ni serikali yenyewe tu. Mbona Arsenal ilipata Wawekezaji wa Emirates wakajenga ule uwanja wao ?
In theory hizi timu mbili ilitakiwa ziwe na viwanja tangu miaka ya 2000. Ila in practice ndiyo wakitaka kuanza hiki mara wanakuja wazee kudai timu au makomando kunyang'anya timu.
 
Mwekezaji wa Simba SC Mohammed Dewji (MO), amewaonesha Wapenzi na Mashabiki wa Simba ramani mpya ya Mo Simba Arena akisema huo ni mradi mkubwa ambao utaweka msingi wa mafanikio ya Club hiyo baadaye.
View attachment 3116797
Akiongea leo October 06,2024 kwenye Mkutano Mkuu wa Club hiyo, Mo Dewji amesema "Hii ni ramani mpya ya Mo Simba Arena, mradi mkubwa ambao utaweka msingi wa mafanikio yetu baadae, tunatarajia kujenga kambi bora ya mazoezi itakuwa na gym, majengo ya malazi, kituo cha lishe, bwala la kuogolea, kituo cha burudani, viwanja vitano vya kisasa zaidi ya hayo kujenga makumbusho ya klabu na kuanzisha chuo cha maendeleo ya Vijana ili kulea vipaji vya soka Nchini"

"Ili kufanikisha yote haya tunasubiri mchakato wa mabadiliko ya Simba kukamilika, tuko katika hatua za mwisho, ujenzi wa miundombinu hii unakuja na gharama kubwa, ni ngumu kuanza huu ujenzi bila mfumo kubadilika"

View attachment 3116805

Pia, Soma:

PICHA: MO Dewji na Mangungu washikana mikono kwa mara ya kwanza
Hotuba ya Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi Simba SC Mo Dewji kwenye mkutano mkuu wa Club 2024
Mwamedi again kuelekea tarehe 19🤣🤣
Kuna kipindi aliunda tume kwa ajili ya mechi ya watani. Sasa hivi naona amekuja kivingine😅
 
Hiyo arena itakuwa mali yake sio ya Simba na ndio maana ina jina lake.

Siku akiamua kusepa, Simba hawana chao.
 
Hivi Mo hawezi kufanya chochote Simba bila kutanguliza jina lake?
Sasa madam ulitaka tu atoe kama vile sadaka msikitini? Lazima aangalie atanufaika vipi akitoa pesa zake!
 
Plan nzuri isiishie kwenye makaratasi tu.
 
Mwekezaji wa Simba SC Mohammed Dewji (MO), amewaonesha Wapenzi na Mashabiki wa Simba ramani mpya ya Mo Simba Arena akisema huo ni mradi mkubwa ambao utaweka msingi wa mafanikio ya Club hiyo baadaye.
View attachment 3116797
Akiongea leo October 06,2024 kwenye Mkutano Mkuu wa Club hiyo, Mo Dewji amesema "Hii ni ramani mpya ya Mo Simba Arena, mradi mkubwa ambao utaweka msingi wa mafanikio yetu baadae, tunatarajia kujenga kambi bora ya mazoezi itakuwa na gym, majengo ya malazi, kituo cha lishe, bwala la kuogolea, kituo cha burudani, viwanja vitano vya kisasa zaidi ya hayo kujenga makumbusho ya klabu na kuanzisha chuo cha maendeleo ya Vijana ili kulea vipaji vya soka Nchini"

"Ili kufanikisha yote haya tunasubiri mchakato wa mabadiliko ya Simba kukamilika, tuko katika hatua za mwisho, ujenzi wa miundombinu hii unakuja na gharama kubwa, ni ngumu kuanza huu ujenzi bila mfumo kubadilika"

View attachment 3116805

Pia, Soma:

PICHA: MO Dewji na Mangungu washikana mikono kwa mara ya kwanza
Hotuba ya Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi Simba SC Mo Dewji kwenye mkutano mkuu wa Club 2024
Mudi siyo wa kumuamini kivile, alishawahi kuwainyesha check ya bilioni 20.
Walipomuuliza ameiweka kwenye account ipi akadai ipo kwenye account ya club ila kama una dhambi hauwezi ukaiona🤣
Mwaka mwingine alipoulizwa tena akamjibu mwandishi "unaijua bilioni 20 wewe? Siyo hela ndigo hiyo, bilioni 20 unaweza ukaanzisha bank"
 
Napata ukakasi kwa hilo jina" MO SIMBA ARENA"
hyo arena ndo ule uwanja wa mazoezi au kuna arena itajengwa kwa ajili ya kuchezea mechi za ligi.?
sema tuna jenga uwanja wetu.
Ila kwa lile eneo pale😄😄😁.Mo anatupanga
 
Back
Top Bottom