Mwelekeo wa sera za Tanzania kwa kuzingatia maudhui ya Ilani ya CCM ya 2020-2025: Je serikali itaweza kutimiza ahadi hizi zote kwa wakati?

Lakini, katika ilani hii, haikutajwa ahadi ya “bima ya afya kwa watu wote.” Hii ni ahadi ya jukwaani. Mwisho wa kunukuu!

Pia umeweka picha ya nani hapo juu kabisa ya bandiko lako?

Queen Esther
 
Queen kama alitamka kwenye kampein hutasiliwa kama ahadi za kampen ambazo wananchi wengi hawatabaini kama alitamka tu na haipo kwenye ilani so lazima itekelezwe
 
Queen kama alitamka kwenye kampein hutasiliwa kama ahadi za kampen ambazo wananchi wengi hawatabaini kama alitamka tu na haipo kwenye ilani so lazima itekelezwe

Lakini, nadhani pointi ya kwamba tofauti kati ya ahadi ya jukwaani na ahadi ambayo iko kwenye ilani haiondoi ukweli kwamba zote ni ahadi halali anaielewa.

Kwa mfano, Rais Magufuli ametoa ahadi zaidi ya 10 jukwaani kwenye kampeni ambazo hazimo ktk ilani, na zote ni ahadi halali.

Tatizo lake ni kukurupuka:

Yeye amejishtaki, na kuna mchangiaji mmoja amemjibu vizuri.

Queen Esther amesoma aya ya kwanza (Afya) akahitimisha kwamba bandiko linamshambulia Rais Magufuli na kuiponda Ilani ya CCM.

Basi akaanza kubutua hoja ambayo hajaielewa, kwani alikuwa bado hajafanya argument analysis, evaluation, and rebutting.

Anasema kuwa, yeye amesoma hiyo aya moja inayomhusu, na anawaomba "wenzake" wasome aya baki.

Nilicheka sana.

Kwa maoni yangu, tatizo lake hajafunzwa vema rules of text analysis, argument analysis, argument evaluation and argument rebutting.

Au ndio ametoka hivi karibuni kule Malindi (ya Zanzibar).

Kusudi aweze kupambana na magwiji wa hoja kama Mama Amon anapaswa atulie, akubali kufundishika.

Ujuzi wa aina hii hauji haraka.

Ni matokeo yauzoefu wa zaidi ya miaka mitano.

Akikua ataacha papara.

Jambo zuri kwake, ni mzalendo kweli!

Tehe tehe teeeeeh!
 
Hakuna anayekubishia kuwa rais alishinda na sisi wanaccm humu jukwaani tunashangilia ushindi huu hoja ni je sekta ya afya inaweza kuwa imara hasa ukizingatia kuwa hoja ya bima ni mtambuka na haipo kwenye ilani


Waziri gwajima amepinga maiti kushikiliwa sasa kibao kimegeuka hutibiwi mpaka uwe na pesa tutafia reception
 
Mama Amon kumbuka wakati wa vikao vya kuelekea uchaguzi mwaka 2025 lazima kutakuwa na uchambuzi wa ukamilishaji wa ilani kwa asilimia na hapo ahadi hizi holelela hupigwa chini kwa kuwa hazimo kwenye kitabu na hapo ndio wenye kumbukumbu na ahadi hizi huuliza na kutulizwa kuwa hazikuwa kwenye ilani

Hizi huitwa ahado hewa kama hazita tekelezwa na huitwa hisani ya rais zikitekelezwa na hapa ndio kuna shida

Katika hotuba ya kuvunja bunge rais atasema tumekalilisha ilani kwa asilimia mia na hizi za majukwani hakuna

USSR
 

USSR, uwezekano wa bima ya afya kwa wote upo.

Yaani, vyanzo vipya vipo.

Kinachohitajika ni wadau muhimu kukalishwa pamoja na kukubaliana, wakaandika technical ministerial paper iliyoshiba, kuiwasilisha ktk Baraza la Mawaziri, public consultation kufanyika, muswada kuandaliwa, sheria kutungwa, na utekelezaji kuanza.

Huko nyuma kulikuwa na kigugumizi kwamba vyanzo vya mapato ya serikali vilivyopo vitaguswa na kuleta mtikisiko wa kimapato serikalini.

Lakini, bado kuna vyanzo vingi havijaguswa.

Mfano, "Health Financing Strategy 2015-2025" inaeleza mengi.

Nitaiweka hapa baadaye.
 
Wale jamaa wakuhudumie bila pesa .naona rushwa itaota mizizi .

Private hospital zinaipiga sana pesa serikali wao wanataka bima tu waijaze wanavyotaka mzigo kwa serikali

Kwa nini Obama care imeshindikana USA?
 
Hizo taarifa ni sahihi kwa kiasi gani? Mabegi yalikutwa katika vituo vingapi kati ya vituo 800+? Na mabegi hayo yalikuwa na kura kweli? Kuna tofauti kati ya facts na hearsay. Bandiko langu linakaribisha verified data.

Karibu
Wasimamizi wameshaanza kukiri kwamba walizuiwa kuhesabu zilizokuwa kwenye masanduku halali bali wakalazokishwa kutangaza zilizoletwa na TISS. We dada nikikukamata nitakusugua mpaka ukome kunifahamu!
 
Wasimamizi wameshaanza kukiri kwamba walizuiwa kuhesabu zilizokuwa kwenye masanduku halali bali wakalazokishwa kutangaza zilizoletwa na TISS. We dada nikikukamata nitakusugua mpaka ukome kunifahamu!

Hearsay not acceptable evidence.
Halafu i dont date people who do not know basic issues like this one. Forget!
 
Umefanya analysis kwa vyama viwili pekee. Vipi ikiwa ungefanya kwa vyama japo kwa zaidi ya viwili Kama sio vyote ili tuwe na eneo Pana kwa kuwa vyama vyote vipikuwa na ilani yake. Kwenye sayansi kanuni zinaelekeza kuwa "more samples for treatment is more accurate becoming".
 

Noted. Lkn nilitumia focused sampling badala ya randome sampling. Yaani niliamua kushughulika na vyama viwili vikubwa kwa vile nilitaka kuwashawishi wasomaji waelekeze volitions zao huko. Lkn hilo linaweza kufanyika given time and other resources.
 
Wale jamaa wakuhudumie bila pesa .naona rushwa itaota mizizi .

Private hospital zinaipiga sana pesa serikali wao wanataka bima tu waijaze wanavyotaka mzigo kwa serikali

Kwa nini Obama care imeshindikana USA?

Hiyo inaweza tafitiwa.
 
Hoja yako namba 4 naipinga;

- Chadema iko Mbeya, Tarime, Nkasi- Kaskazini lakini bado kuna watu mnakuja na propaganda ya ukanda mpaka leo?!

- Udini; sijui ni kigezo gani kimetumika kuhalalisha hii hoja yako, umewahesabu walutheri walioko Chadema ukaona idadi yao inazidi madhehebu mengine au dini nyingine? au umeangalia juu juu kwa baadhi ya viongozi ndio ukaja na hii hoja yako?

- Usiasa-biashara; hii nayo ni hoja dhaifu, nadhani kwa hii dunia tunayoishi kwa sasa huwezi kulikwepa hili, sisi sio wajamaa tena, na huu mfumo umewekwa na CCM wenyewe, na wapo viongozi wengi wa CCM wanaofanya biashara kwa kificho, midomoni wanajiita wazalendo lakini kiuhalisia hawana lolote, hivyo hapa napo kuilaumu Chadema haiwezi kuendesha nchi kwasababu haya ni maoni yako binafsi yasiyo na uhalisia wowote unakosea.

- Chadema kusema wataweka rehani madini kwa ajili ya mikopo; hili naona CCM mmeamua kulielezea mnavyopenda nyie, kiuhalisia, haya madini yetu hata leo hii mmeyaweka rehani siku nyingi sana kwa kumnufaisha mzungu wakati ndugu zetu maeneo ya uchimbaji bado wamezungukwa na umasikini wa kutisha, mikataba mliyosaini nao ni ya kinyonyaji, mmekula 10% hamuwakumbuki tena masikini wa nchi hii.

Sasa kama Chadema wao watakuja na mbinu nzuri zaidi itayomsaidia mtanzania kupata chochote toka kwenye madini waliyopewa na Mungu kwangu naona nafuu, kuliko madini kuishia kwa mzungu na sisi tunabaki na mashimo tu kwa sababu ya sera mbovu za serikali ya CCM.
 
Wamekili wapi? Leta ushahidi
Wasimamizi wameshaanza kukiri kwamba walizuiwa kuhesabu zilizokuwa kwenye masanduku halali bali wakalazokishwa kutangaza zilizoletwa na TISS. We dada nikikukamata nitakusugua mpaka ukome kunifahamu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…