Mwendokasi UDART mmefeli

Mwendokasi UDART mmefeli

Moshi25

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2022
Posts
2,555
Reaction score
4,118
Samahani Leo nimeamka sio poa!

Unafika kivukoni mabasi sita yamepaki mnasubiriwa mjazane dakika ishirini nzima mmekaa tu mmejaa hasira Kali eti mnasubiri bus na mnayaona yamepaki hatimae ghafla wanaachia basi moja la kimara wote mnakimbilia spidi kali kupanda kama wanyama pori manyumbu wengine mnapamia wazee wanaanguka mnaombana samahani.

Wengine wanaangusha cm na pochi hawajui masikini akili iko kwenye kuwahi siti dirishani basi abiria mnajazwa kama nyanya bus linaondoka humo ndani kuna harufu Kali mmejaa kama nyanya mtu hata kuhema mtu huwezi umebanwa hugeuki ukikaa vibaya unaibiwa cm na pochi! Halafu pale kuna Mgambo wa darasa la nne wanafokea watu na PhD zao, wanakwambia wewe panga mstari haraka uingie kwenye bus alaaa!

Saa zingine mara uko fire gari zinàkuja za kwenda kimara watu wamejaa hata mlango haufunguki gari ikifika fire ukiwaangalia abiria walioko ndani wamebanwa wametoa macho kama mijusi imebanwa na mlango wanapumua kwa shida majasho yanawavuja bàlaa wote wamekunja uso zao! Na hawataki wewe uingie!

Sasa Pale fire asubuhi labda unaumwa sana Sasa unasubiri bus la kwenda Muhimbili utakaa pale nusu saa nzima bus haliji mpaka unazidiwa na unaweza kudedi kama vipi eti mpaka mjazane kwanza ndo wapige cm eti mara ghafla utaona wanaleta bus moja tu mjazane kama nyanya mara wagonjwa wangine wako hoi!

Ukiwauluza kwanini mabasi ya Muhimbili ni machache sana asubuhi saa zingine wanasema eti trafiki wa fire akiconcerntrate kuruhusu magari ya morogoro road tu basi mabasi yanayotoka Muhimbili kwenda Gerezani yanakwama kwenye foleni na kusababisha uhaba wa mabasi ya kwenda Muhimbili. Basi wanaohusika please mwambieni yule trafiki anazingua.

Kiukweli wenye wanaendesha huu mradi wa mwendokasi na viongozi waliowapa tenda wote wataenda jehannam maana si kwa kutesa watu hivi.

Kiukweli viongozi wengi wa Tanzania wanatesa sana raia wa nchi hii masikini. Watu wanateseka sana na inajulikana watesi wao wengi wakifa watafikia jehannam sababu wamejaa kiburi na viongozi wengi hudhani wataishi duniani milele kumbe wakifika miaka 70 tu wengi wao hufa kwa pressure na kupooza sababu ya kuwa na matumbo makubwa yaliyoshiba sukari iliyonunuliwa kwa Tozo za watu masikini. Hawa viongozi wakifa huwa Kuna dawa inaitwa Formalin wanapakwa Ili miili yao iliyokwisha kuanza kuoza isitoe harufu Kali. Nawakumbusha formalin inatusubiri duniani tunapita tu!

Idadi ya mabasi ni ndogo mno kulinganisha na abiria kama vipi mabasi yaongezwe asubuhi na jioni!

Nyie wababe UDART Wekeni route ya Kivukoni - Muhimbili kama vipi just for fun ikiwapendeza!


Good day!
 
Lengo kuu la mwendokasi ni kubeba abiria wengi. Unayaona hayo mabasi yamejaa ila watu wengi hujaa milangoni.
 
Hayo magari watu wanajazana mlangoni ndani kweupe sana ingekuwa wanagunguwa mlango mmoja watu wanaingia kwa mstari miwili uku na uku then kati kati, ila utaratibu mbovu na watu hawaendi bila kusimamiwa.
 
Kiukweli viongozi wengi wa Tanzania wanatesa sana raia wa nchi hii masikini.
Ili kiongozi aonekane anafanya kazi ni lazima awape matatizo ili siku akitatua mmpigie makofi
 
Hayo magari watu wanajazana mlangoni ndani kweupe sana ingekuwa wanagunguwa mlango mmoja watu wanaingia kwa mstari miwili uku na uku then kati kati, ila utaratibu mbovu na watu hawaendi bila kusimamiwa
Watanzania tumekosa ustaarabu na wenye kampuni nao wamekosa weledi
 
Lengo kuu la mwendokasi ni kubeba abiria wengi. Unayaona hayo mabasi yamejaa ila watu wengi hujaa milangoni.
Abiria wa Kimara wanaotokea kivukoni na gerezani ni wengi na wanajaa sana, nafuu iko wanaojiongeza kuenda kupandia Morocco. Abiria wanaofaidi Mwendekosi ni Kinondoni
 
Udart wanajidalalia wenyewe kwa bus zao hapo ingekua ni Kampuni inayojitambua hizo mambo za watu kujazana zisingekuwepo maana kila dakika bus linalipita hasa asubuhi na jioni wao kazi yao ni kubeba tu abiria bara bara yao ila wanashindwa ingekuwa pana ushindani sijui ingekuwaje?
 
Yaani kama route zako ndo kama hizo Bora kununua ka baby walker mchuzi wa 20k una cruise unachoka
 
Nunua hata pikipiki kama gari lako mwenyewe inakushinda. Watu wanashindwa kupumua kuna aliyekufa kwa kukosa pumzi, mara wamebanwa kama mojusi wametoa macho je kuna aliyepatwa na majeruhi muda huu yuko hapo muhimbili.

Malalamiko mengine hayana maana. Acha watu watafute pesa bhana. Kelele zingine kausha. Kuna uber na bolt ulishindwaje kujiopngeza.

Fyuu
 
Soma Isaya 50 mstari wa 11. Laana ya kukimbiza mwenge ni kulala kwa huzuni.

Kila kitu kinakuwa na mwisho mbaya. Badala ya furaha tunaambulia huzuni. Cheki uwanja wa taifa, cheki katiba mpya, ilitumia mabilioni mwisho wa siku hamna kitu, cheki mradi wa gesi, nchi imetumia ma trilioni, mwisho wa siku hamna kitu. Laana ya mwenge.
 
Nunua hata pikipiki kama gari lako mwenyewe inakushinda. Watu wanashindwa kupumua kuna aliyekufa kwa kukosa pumzi, mara wamebanwa kama mojusi wametoa macho je kuna aliyepatwa na majeruhi muda huu yuko hapo muhimbili.
Malalamiko mengine hayana maana. Acha watu watafute pesa bhana. Kelele zingine kausha. Kuna uber na bolt ulishindwaje kujiopngeza
Fyuu
Mwananchi ana haki ya kupata huduma bora kwa bei nafuu, sio bora huduma
 
Hili uweze kishi Dar sifa ya 1 uwena uwezo wa kukimbia basi kuwai nafasi huna uwezo ludi huku kwetu au nunua galilako
 
Hayo magari watu wanajazana mlangoni ndani kweupe sana ingekuwa wanagunguwa mlango mmoja watu wanaingia kwa mstari miwili uku na uku then kati kati, ila utaratibu mbovu na watu hawaendi bila kusimamiwa
Kwamba waajiriwe na MAKONDAKTA ili wawapange watu? Maana abiria bongo walishazoea kupangwa na makondakta.
 
Back
Top Bottom