BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Vyuma vimekaza Mkuu lakini ngwini mkaza vyuma hataki kusikia ukweli kuhusu ukurupukaji wake uliodidimiza uchumi na hatimaye vyuma kukaza. Kazoea kusema uongo na kudanganywa kwamba uchumi wetu ni bora sana katika Afrika kuliko nchi yoyote ile wakati ni UONGO MTUPU!!
Wadau nipo kwenye biashara ya Hardware mwaka wa pili sasa, mwanzo biashara ilikuwa poa mpaka nikawa najisemea biashara ndiyo hii!
Hali imechange sana mwaka huu japo mwaka jana hali ilianza kudorola taratibu, sasa mwaka huu hata kipindi ambacho huwa tunaona ni cha biashara mambo yamekuwa sio kabisa!
Kwakweli stress nilizonazo hazielezeki, mzigo umejaa dukan wateja hakuna mtu unakomaa kwa siku unaondoka na elf 20.
Hapa nawaza niswitch kwenda kwenye biashara gani nashindwa kuelewa!
Vipi huko wenzetu hali ya biashara ikoje, mtu asije akaniambia niingie Forex hiyo naifahamu tayari!