Mwenendo huu wa biashara hata siuelewi!

Mwenendo huu wa biashara hata siuelewi!

Vyuma vimekaza Mkuu lakini ngwini mkaza vyuma hataki kusikia ukweli kuhusu ukurupukaji wake uliodidimiza uchumi na hatimaye vyuma kukaza. Kazoea kusema uongo na kudanganywa kwamba uchumi wetu ni bora sana katika Afrika kuliko nchi yoyote ile wakati ni UONGO MTUPU!!

Wadau nipo kwenye biashara ya Hardware mwaka wa pili sasa, mwanzo biashara ilikuwa poa mpaka nikawa najisemea biashara ndiyo hii!

Hali imechange sana mwaka huu japo mwaka jana hali ilianza kudorola taratibu, sasa mwaka huu hata kipindi ambacho huwa tunaona ni cha biashara mambo yamekuwa sio kabisa!

Kwakweli stress nilizonazo hazielezeki, mzigo umejaa dukan wateja hakuna mtu unakomaa kwa siku unaondoka na elf 20.

Hapa nawaza niswitch kwenda kwenye biashara gani nashindwa kuelewa!

Vipi huko wenzetu hali ya biashara ikoje, mtu asije akaniambia niingie Forex hiyo naifahamu tayari!
 
Yaan acheni wandugu ..bisiness yangu from mauzo ya 10m kwa mwezi mpaka 5m kwa mwaka mzima .. Nimefunga rasmi naenda tra kusign out .. Naingia kilimoni tu basi..
Kuna wsliolima,wamekosa soko la uhakika la mazao yao. Watch out!
 
Daah !! Mimi viazi vyangu ekari 5 vimekomaa toka mwezi wa 10 havijapata mteja.
 
Acha tupige kelele weeeee, lakini walioingia darasani na wakasoma uchumi wanakijua fika kinachoendelea... Ni swala la muda tu
 
Mkuu hakuna biasha “tangible” ambayo leo inalipa vzr. Zote maumivu tu. Wengne mpaka tunajikuta tunasusua maana unaamka asubuh unaenda kufanya biashara unarud jion km ulivyoenda bora ww unarud na 20. Kiukweli mambo si mazur na mwenye macho aone..hii sio siasa ni life reality.
mi nilijua ni mimi tuu,kumbe tuko wengi
 
ndugu zangu msikate tamaa kwani hiki ni kipind cha mpito tu maana hakuna mfanya biashara asie lalamika kwani Tanzania yetu biashara asilimia kubwa tunamtegemea mkulima, Na msimu huu inaonesha kutakuwa na neema sana kwani hali ya mazao sio mbaya hivyo kuanzia April ni neema tu.
mkuu unaleta style za watoto wa kuku kila siku tutanyonya kesho,soko la mazao lenyewe halieleweki
 
Vyuma mkuu. Ukweli ni kwamba watu hawana pesa. Mie na store ya vyakula lakini mauzo ni ya ajabu. Mtu unauza shs 800000 kwa siku wakati tulishazoea 5000000 kwa siku!

Tafuta grees mkuu. Vyuma hivyo
Something is better than nothing
 
Vyuma vimekaza Mkuu lakini ngwini mkaza vyuma hataki kusikia ukweli kuhusu ukurupukaji wake uliodidimiza uchumi na hatimaye vyuma kukaza. Kazoea kusema uongo na kudanganywa kwamba uchumi wetu ni bora sana katika Afrika kuliko nchi yoyote ile wakati ni UONGO MTUPU!!
Aisee. [HASHTAG]#NgwiniMkazaVyuma[/HASHTAG]!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kulia na kupiga mayowe haitasaidia kwanza lazima ubadilike na wakati na hali iliyopo, pia unachopata unamshukuru Mungu, ulikua unapata milioni 5, sasa unapata laki 5 unalalamika nini?
 
Wadau nipo kwenye biashara ya Hardware mwaka wa pili sasa, mwanzo biashara ilikuwa poa mpaka nikawa najisemea biashara ndiyo hii!

Hali imechange sana mwaka huu japo mwaka jana hali ilianza kudorola taratibu, sasa mwaka huu hata kipindi ambacho huwa tunaona ni cha biashara mambo yamekuwa sio kabisa!

Kwakweli stress nilizonazo hazielezeki, mzigo umejaa dukan wateja hakuna mtu unakomaa kwa siku unaondoka na elf 20.

Hapa nawaza niswitch kwenda kwenye biashara gani nashindwa kuelewa!

Vipi huko wenzetu hali ya biashara ikoje, mtu asije akaniambia niingie Forex hiyo naifahamu tayari!
Chakula, dawa na usafiri wa abiria tu ndio salama kwa sasa
 
Mbaya zaidi ukiwa na mkopo benki afu mwisho wa mwezi unatakiwa kurudisha marejesho hapo ndio utajuta kuwa mfanyabiashara.....

Ila all in all huu ni upepo yote yatapita na mambo yatarudi kuwa kama yalivyokuwa mwanzo...
Upepo?mkuu bila hicho kisiki cha mpingo kilichopo magogoni kuondoka ndo tunageuka Zimbabwe polepole huku tunajiona!
 
Du hii hali ukiwaza unaweza jua upo pekeyako kumbe tupo wengi.....najiuliza wanaosema hali shwari wanaolalamika ni wapiga dili inamaana na Mimi na kale kabiashara kangu ndo ulikuwa upigaji dili!! Yote yatapita!!
 
Vyuma mkuu. Ukweli ni kwamba watu hawana pesa. Mie na store ya vyakula lakini mauzo ni ya ajabu. Mtu unauza shs 800000 kwa siku wakati tulishazoea 5000000 kwa siku!

Tafuta grees mkuu. Vyuma hivyo
Vyakula vya kuku?
 
Hahahaha hutaki kabisa kuhusu forex, umeunguza acc ngapi boss
 
Mkuu hakuna biasha “tangible” ambayo leo inalipa vzr. Zote maumivu tu. Wengne mpaka tunajikuta tunasusua maana unaamka asubuh unaenda kufanya biashara unarud jion km ulivyoenda bora ww unarud na 20. Kiukweli mambo si mazur na mwenye macho aone..hii sio siasa ni life reality.
...daladala hesabu iko palepale!
 
Back
Top Bottom