Pre GE2025 Mwenezi Makonda: Sifanyi mikutano ya kujaza watu kwa kutumia wasanii kwasababu tunataka kuona uhai wa CCM na jumuiya zake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2019
Posts
1,521
Reaction score
4,381
πŸ“ŒπŸ“Œ SIFANYI MIKUTANO YA KUJAZA WATU KWA KUTUMIA WASANII KWASABABU TUNATAKA KUONA UHAI WA CCM NA JUMUIYA ZAKE - MWENEZI MAKONDA

Asema CCM Inawapenda na Kuwajali Wasanii lakini kwasasa ni muhimu kuona Uhai wa Chama, Wasanii wataburudisha kipindi cha kampeni

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amebainisha kuwa hatopenda kuona CCM inahangaika kuombaomba kura bali anachokihitaji ni kuona Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kujipambanua kwa usimamizi mzuri wa utekelezaji wa Ilani yake na hatimaye kuendelea kujenga imani kubwa kwa Watanzania.

Mwenezi Makonda ameyasema hayo tarehe 20 Januari, 2024 akizungumza na Baraza la Wazee wa Tanga katika hafla fupi ya kula chakula cha usiku kwa pamoja.

Aidha, Mwenezi Makonda amesema hatopenda kuona kwasasa mikutano ya CCM inatumika kujaza watu kwa kutumia Wasanii na badala yake ijaze kutokana na kujipambanua kwa kazi na sera zake.

" Sitaki kufanya mikutano ya kujaza wasanii kwasababu nataka kuona uhai wa Chama Cha Mapinduzi na sio kujaza mikutano kwa kutumia wasanji, kusema hivi haimaanishi CCM hatupendi wasanii...hapana ni watu wetu na tunawapenda na tunatambua na wao wanaipenda CCM lakini kwasasa ni wakati wa kuchapa kazi na wakati wa burudani utafika huko mbeleni kipindi cha kampeni "

" Lazima tujipime tuone Chama Cha Mapinduzi tupoje na ndio tutaweza kumsaidia kazi Mwenyekiti wetu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuona Uhai wa Chama na Jumuiya zake "

Hayo yamesemwa na Mwenezi Ndugu. Paul Makonda.

#CCMKazini
#VitendoVinaSauti
#KaziIendelee


PIA, SOMA:

Matamko mengine ya Paul Makonda
 
Sahihi Kabisa

Kama Tundu Antipas Lisu hakunaga Wasanii LAKINI bonge la nyomi
 
Huyu Mtu anabezwa tu Wahuni ila Mungu amempa Kibali, Tazama Kila anachozungumza ndicho ambacho Mwananchi mwenye akili anataka kusikia.
 
Hivi kuna watu wenye uelewa mzuri kabisa wanaenda kwenye hiyo mikutano?
 
Sukuma gang kazini kwa posho ya buku 7
 
Sukuma gang kazini kwa posho ya buku 7
Unachokifanya hapa ni kuhubiri ukabila, unakuwa huna utofauti na Mwaipopo anayeligawa taifa kwa kuhubiri udini.

Acheni mambo haya kwa ustawi wa taifa.
 
Reactions: Tui
Mbona anampigia dongo mama Samiah anayejaza wasanii kwenye mikutano yake. All in all hakuna la maana CCM.
 
Kwa Makonda upo na Makonda anamtetea Rais ila Kwa Samia haupo 🀣🀣

We Suku gang huna unalolijua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…