Mwenye CV ya Msemaji Mpya wa Serikali atusaidie? Atueleze amewahi kufanya nini cha kukumbukwa kwenye maisha yake ya utumishi au siasa?

Mwenye picha ya msemaji mpya wa Serikali,sisi wengine tulikuwa hatumfahamu Mkuu wa wilaya Temeke
 
LOO, wee jamaa ni , mtunga hadithi mzuri.

Hebu niangalie jina, 'mubby777'; kumbe siyo yule tuliyemzoea humu, nani yule 'dudumizi', au kitu kama hicho.

Hivi vipaji vyenu kwa nini msiviendeleze ili kukuza hii fani? Kwanza kuna hela nzuri sana huko, kuliko kusubiri haya makombo ya akina Samia wanayowatupia hapa na pale wanapofurahi.
 
Duhh... kumbe Tz mambo mengi sana huwa yanatendeka hatujui
 
Kwa hiyo ameteuliwa kwa sababu yeye na mdogo wake ni watu wa vitengo?

Amewahi kufanikiwa katika jambo gani ambalo TAIFA linaweza kujivunia?

Creativity yake imelala kwenye maeneo gani? Is he from familia bora or bora familia?
Ushaambiwa kasoma na Kabila.. nadhani ushahisi anatoka kwa wala nchi... hahahahaaa
 
He! Tumesoma wote chuo cha AGM pale Maritime Sokoine huyu jamaa akionekana wa kawaida kumbe alificha makombora yote haya?!
 
Wa dini yangu
 
Nachojua alisoma na Joseph Kabila
 
Mobhare Matinyi ni mtu na nusu kuliko yule wa BBC milokuwa mkimpigia debe ... zaidi ya saba alioloondoka nalo hana zaidi.
 

Attachments

DAR ES SALAAM: Julai 2 mwaka huu Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Mwanahabari Mobhare Matinyi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam. Miezi mitatu baadaye amemteua Matinyi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Matinyi mbali na kuwahi kuwa mkufunzi katika Kituo cha Diplomasia cha Musumbiji-Tanzania amekuwa mwanahabari na mchambuzi wa maswala mbalimbali mengi yakilenga kuitetea Tanzania. Pia amewahi kuwa na ukurasa – column katika gazeti la kiingereza la ‘The Citizen’ – The Eagle’s Eye na ameandika Makala mbalimbali kupitia gazeti la Jamhuri.

Wengi wanamkumbuka Matinyi kwa uchambuzi wake tunduizi wa mabendekezo ya Chadema kuhusu Katiba mpya wakati huo akiwa kama Mshauri Mwelekezi huko nchini Marekani.

Hata hivyo, kabla ya kuwa Mkuu wa Wilaya, Mwanahabari huyu kitaaluma, alikuwa akitumika kwenye jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika maarufu kama SADC. Kwa sasa Matinyi anaenda kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Gerson Msigwa, aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.
 
Katiba inasemaje kuhusu hiyo nafasi?
kama hakuna muongozo piga kimya tu
 
Ni team Membe so ni team Nape.Nape ndo kampogia chapu kwa Samia .Imeenda hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…