mandingo6262
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 424
- 81
Jamani naombeni maelezo kidogo kuhusiana na hili, kuna rafiki yangu ni mjamzito ila baada ya kujikuta akisumbuliwa na maumivu ya tumbo alienda hospitali na kupigwa ultra sound walimwambia kuwa mimba imetunga karibu na mrija wa uzazi, cha ajabu ni kwamba ameendelea kuumwa tumbo na kutapika, hana hana hamu ya kula na hospitali walichosema ni kwamba asubiri kama akiona dalili za kutokwa na damu ukeni basi aende hospital. Naombeni mnieleweshe kuhusiana na hili