Mwenye Nyumba ameleta mganga wa kienyeji anatulazimisha tulambe unga anahisi kuna mchawi kwenye nyumba yake

Mwenye Nyumba ameleta mganga wa kienyeji anatulazimisha tulambe unga anahisi kuna mchawi kwenye nyumba yake

Habarini ndugu wanaJF,

Baba mwenye nyumba amemleta mganga kutoka kusini huko anadai kwenye nyumba yake kuna mtu anamchezea (mambo ya kichawi), sasa anatulazimisha tulambe ungaunga mweupe nimesikia wanauita 'usembe' ili kumbaini mchawi kwenye nyumba yake.

Binafsi nilikataa kulamba vitu visivyoeleweka na sina hizo imani, ila alinichimba mkwala hadi jtano nimpe jibu nikishindwa nihame kwake.

Dhumuni la kuleta hili jambo kwenu mnipe ushauri wa kufanya sababu alinipa siku tatu ambayo ya mwisho ndio leo na hapa nipo job nafikiria nikirudi home nimpe jibu gani.

Kwa kuongezea tumebaki wapangaji wawili ambao tumekataa kulamba hayo madude yake.

Je, yana madhara yoyote kiafya wataalam wa mambo?
Lamba unga huo
 
Usilambe hata iweje, ni bora liwalo na liwe kuliko kufanya maagano na wenye imani za kishirikina
 
NIMEKUJA NA MREJESHO

baada ya kupata ushauri kwa wadau mbalimbali humu maoni yenu wote niliyachukua na hiki ndicho kilichojiri,
Baada ya ile siku ya deadline ya kulamba unga ilipokwisha nikaamua kuuchuna kimya nikimtegea mwenye nyumba alete habari zake ili nikamfungulie kesi police kama mdau mmoja alivyonishauri hapo juu. Nayeye naona alishutkia(sijui alipitia huu uzi au machale tuh yalimtonya) but akawa amepause kwa mda bila kupata jibu, siku hiyo nimeamka mishale ya 12 nikakuta kuna viungaunga vimenyunyiziwa mlangoni kwangu mimi nikatoa fagio ndani nikafagia vyote then nikapita zangu nikaingia job. sasa ikabidi nitumie ukachero kujua sababu ya mimi kuwekewa vile mlangoni, ndio nikapenyezewa fununu kuwa mganga wake alichange plan kwamba kama mtu hataki kulamba basi wamwage mlangoni kwangu na wanivizie niko ndani coz nikitoka lazima niluke na kama ninauchawi basi sitoboi hata hatua 5. Kwa hilo walinikosa asee labda waje na plan nyingine halafu yule mganga wake naona ameshaondoka.
Nitaendelea kuwapa update wakuu ila siami hadi kodi yangu iishe yote na siachi hata siku moja. Update nyingine zitakuja kama drama zitaendelea 🙏🙏🙏
 
  • Thanks
Reactions: Cyn
Habarini ndugu wanaJF,

Baba mwenye nyumba amemleta mganga kutoka kusini huko anadai kwenye nyumba yake kuna mtu anamchezea (mambo ya kichawi), sasa anatulazimisha tulambe ungaunga mweupe nimesikia wanauita 'usembe' ili kumbaini mchawi kwenye nyumba yake.

Binafsi nilikataa kulamba vitu visivyoeleweka na sina hizo imani, ila alinichimba mkwala hadi jtano nimpe jibu nikishindwa nihame kwake.

Dhumuni la kuleta hili jambo kwenu mnipe ushauri wa kufanya sababu alinipa siku tatu ambayo ya mwisho ndio leo na hapa nipo job nafikiria nikirudi home nimpe jibu gani.

Kwa kuongezea tumebaki wapangaji wawili ambao tumekataa kulamba hayo madude yake.

Je, yana madhara yoyote kiafya wataalam wa mambo?
Nenda serikali za mitaa then akuandikie notes na serikali z mita wakiwa mashahidi na kama kakutishia pia mripoti mpaka polisi ukae na rb ili aambiwe kabisa usalama wako uko mikononi mwake. then muda ukiisha ndo uhame asikutishe kibwege..kuhama wewe hama tu kwani hiyo nyumba ya kwako? Au ikiungua utabaki hapo? Sema asikutoe ghafla tu wakat hujajipanga
 
Back
Top Bottom