Uchaguzi 2020 Mwenye picha ya Magufuli 2015 akiwa amepiga magoti jukwaani kuomba kura aniwekee hapa

Uchaguzi 2020 Mwenye picha ya Magufuli 2015 akiwa amepiga magoti jukwaani kuomba kura aniwekee hapa

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Mwaka 2015 Mh. Magufuli alikuwa anaomba uongozi wa nchi kwa mara ya kwanza. Alikuwa Bandidu hasa na style ya push ups kuonesha kuwa yuko imara kiafya kuliko mpinzani wake mkubwa Eddo Lowassa ambaye afya ilitetereka kipindi hicho.

Waafrika tunategemea mwanaume anapokwenda kuposa mara ya kwanza anakuwa mnyenyekevu na ndo siku hizi tunawaona wengine wanapiga magoti kuwavika Pete wachumba wao. Lakini kwa Magufuli aliamini atapata tu tena kwa kuonesha "maguvu" jukwaani kwa kupiga push ups na Mapanga Shaaa ya Wanaume Temeke. Alikuwa kibri na mwenye kauli zilizosimama kimamlaka japo alikuwa hajapata mamlaka hayo.

Leo mamlaka anayo maana Katiba yetu yenye viraka na matobo inaendelea kumpa kofia 2 kwa wakati mmoja, Lakini ghafla tumemuona majukwaani si Mara moja kapiga magoti anaomba kura kwa unyenyekevu ambao tunaambiwa kwa wapambe wake anao lakini yeye anakataa na kusema ni Jiwe.

Sasa kama ni tabia yake siku zote, naomba aliye na picha yake ya 2015 akiwa amepiga magoti jukwaani kama alivyofanya juzi Kawe, Wiki iliyopita Njombe nk aniwekee hapa!

tapatalk_1601389064750.jpeg
 
Amejifunzaaaa unyenyekevuuu
 
Kumbe hata na Kawe alipiga magoti kama kule Njombe?
 
Na bado akashinda uchaguzi, 😂 😂 😂 , sasa juzi kapiga tena magoti, panga la kunyolea ni lile lile
 
Hahahahah! KUna watu wamezibuka sio kawaida.

Nimeona bango la Tundu akisema wamchague kwa ajili ya uhuru, haki na maendeleo ya watu. Nikaona ni kauli nzito sana, maana unaweza kusema katika awamu hii tulichoshuhudia ni kunyimwa uhuru, ukosefu wa haki hadi watu kuuliwa kwa kuipinga tu serikali na Magufuli na maendeleo ya vitu yasiyojali watu kabisa. Watu wanakufa mafuriko Dar sie tunashangilia Dreamliner zilizopaki, na bado watu hawaoni kuwa hilo ni tatizo.
 
MWENYE PICHA YA TUNDULISU AKIWA ANASEMA KAMA TUKIGUSIA MIKATABA YA MADINI TUTANYOLEWA NYWELE BILA MAJI, ATUWEKEE HAPA.
 
Bora mie namsubiri "Niguse Ninuke"😛
 
Ingekuwa inawezekana hawa wagombea wangekuwa wanawekwa kisiwani na kufanya kampeni kwa TV na mitandao ili kuwa na usawa, yeyote anayetukana au kumkashifu mwenzake chanel yake inafungwa kwa siku kadhaa ndipo aruhusiwe, ilivyo sasa inakuwa ngumu sana kuwatofautisha
 
Mkuu nimejaribu kupiga google kwenye kabati yangu na searching key words "Magu Magoti 2015" inakuja hiyo picha chini sijuwi nakosea wapi ku sechi?
Mwaka 2015 Mh. Magufuli alikuwa anaomba uongozi wa nchi kwa mara ya kwanza. Alikuwa Bandidu hasa na style ya push ups kuonesha kuwa yuko imara kiafya kuliko mpinzani wake mkubwa Eddo Lowassa ambaye afya ilitetereka kipindi hicho.

Waafrika tunategemea mwanaume anapokwenda kuposa mara ya kwanza anakuwa mnyenyekevu na ndo siku hizi tunawaona wengine wanapiga magoti kuwavika Pete wachumba wao. Lakini kwa Magufuli aliamini atapata tu tena kwa kuonesha "maguvu" jukwaani kwa kupiga push ups na Mapanga Shaaa ya Wanaume Temeke. Alikuwa kibri na mwenye kauli zilizosimama kimamlaka japo alikuwa hajapata mamlaka hayo.

Leo mamlaka anayo maana Katiba yetu yenye viraka na matobo inaendelea kumpa kofia 2 kwa wakati mmoja, Lakini ghafla tumemuona majukwaani si Mara moja kapiga magoti anaomba kura kwa unyenyekevu ambao tunaambiwa kwa wapambe wake anao lakini yeye anakataa na kusema ni Jiwe.

Sasa kama ni tabia yake siku zote, naomba aliye na picha yake ya 2015 akiwa amepiga magoti jukwaani kama alivyofanya juzi Kawe, Wiki iliyopita Njombe nk aniwekee hapa!

 

Attachments

  • images1.jpg
    images1.jpg
    9.4 KB · Views: 3
Back
Top Bottom