Mwenye uzoefu na biashara ya kubandika sticker kwenye pikipiki na magari

Mwenye uzoefu na biashara ya kubandika sticker kwenye pikipiki na magari

stabilityman

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2024
Posts
259
Reaction score
483
Habari nina ofisi jilani na gereji ya pikipiki nimewaza kuwa nifungue ofisi ya kibandika sticker. Mwenye uzoefu naomba uje unipe moja mbili tatu
 
Nenda kwa anayefanya hiyo kazi akupe a b c nadhani ni graphics design iyo kuna machine inabidi uwe nayo na laptop na elimu au uzoefu.
 
Inategemea unataka uanzie level ipi ya hiyo biashara ila kama unataka uown ofisi iliyo complete itabidi uwe na large format printing machine ambayo hii ile ndogo kabisa inauzwa around million saba na nusu then uwe na kijana wa graphics ambae huyu ndio atakua anakusaidia kwenye kudesign hizo stickers pamoja na kufanya branding kwenye hizo pikipiki, bajaji na magari baada ya kupritiwa kwenye mashine.

Ila pia kama huna hiyo budget basi unaweza ukafungua ofisi tu na ukamuweka huyo mtu wa graphics yeye akawa anadesign then baada ya kudesign mnapeleka kazi kwa watu ambao wako na mashine wanaprint then ninyi mnafanya branding yaani kubandika kwenye chombo husika.

Bei za sticker huwa zinaprintiwa kwa mita na huwa zinatofautiana kulingana na material unayohutaji kwamfano contra vision huwa ni kuanzia 12k hadi 18k kwa square metre moja na pvc yaani hizi sticker za kawaida huwa ni kuanzia 7k hadi 9k kwa square metre na kadhalika na kadhalika.

Hapo ndio unaweza kuanzia then baadae utaadvance kwa kununua plotter, digital na kadhalika.
 
Back
Top Bottom