Mwenyekiti Freeman Mbowe kuachia tu uenyekiti haitoshi anapashwa kukamatwa, kuchunguzwa na kufikishwa mahakamani ili arejeshe fedha zote za CHADEMA

Mwenyekiti Freeman Mbowe kuachia tu uenyekiti haitoshi anapashwa kukamatwa, kuchunguzwa na kufikishwa mahakamani ili arejeshe fedha zote za CHADEMA

Kuna mambo tunaweza kubishana pengine ili kulinda itikadi au falsafa zetu ila kamwe hatuwezi kubishana ili kulinda uhalifu na uovu mkubwa kwa kiwango hiki kwenye taasisi kubwa kama CHADEMA.

Nimemsikiliza Makamu Mwenyekiti Tundu Lissu anasema endapo atashinda na kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA ngazi ya Taifa basi atafutilia mbali utaratibu wa mtu mmoja kupita peke yake kwa wadau ili kukusanya fedha kwaajili ya kuendesha na kuendeshea shughuli mbalimbali za chama utaratibu ambao umedumu kwa kipindi Cha zaidi ya Miaka 20 sasa.

Kwa lugha nyepesi huenda ama ni kweli Freeman Mbowe ni mnufaika mkubwa wa fedha za CHADEMA kuliko hata CHADEMA yenyewe kwa miaka hii 20 aliyokaa madarakani,

Najaribu kuwaza ni kiasi gani Cha fedha Mwenyekiti Freeman Mbowe amejizolea toka kwa wapenzi, Wafuasi, wanachama na Viongozi wa CHADEMA wasiotaka kujulikana kwa majina ila tu kwa Mwenyekiti wa Chama Freeman Mbowe kwa kipindi chote hiki Cha miaka 20.

Najiuliza zaidi ni jambo gani lililomfanya Mwenyekiti Freeman Mbowe asitumie kabisa akaunti ya CHADEMA kwa sharti la wadau hao wa CHADEMA kutoandika majina yao rasmi ( watumie fictious names ) kwa lengo la kukuza usiri na kuepa mkono wa CCM na dola.

Mwanafalsafa mmoja wa Kigiriki aliwahi kusema " Yeyote unayemwona mbele yako jua kuwa mtu huyo ni mwizi kwa asili" baada ya falsafa hii ya kila binadamu ni mwizi kwa asili ndio maana utaona leo kila sehemu ya pesa lazima ihusishe watu zaidi ya wawili au wawili mfano hata Password ni mtu wa pili,

Kwa dhana hii ya kila mtu ni mwizi kwa asili, Je falsafa hii haitamuhusu Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa kipindi hiki chote cha zaidi ya miaka 20? Ninani anajua Mwenyekiti huyu kakusanya kiasi gani Cha fedha za wadau hata sasa? Je, hao wadau wataendelea kumwamini Mwenyekiti Freeman Mbowe hata baada ya Uchaguzi huu?

Nahitimisha hivi, kama kweli Mwenyekiti Freeman Mbowe amekuwa akifanya haya kwa miaka yote 20 ya uongozi wake basi Freeman Mbowe ndio Mtanzania pekee aliyejikusanyia pesa nyingi zaidi za Watanzania kwa mgongo wa kuzipeleka CHADEMA na huenda Sasa Uenyekiti wake ukawa wa faida zaidi hata ya Urais wa nchi na madhara yake huenda ikawa ni ngumu zaidi kumwondoa kwenye nafasi hii hasa baada ya kujitengezea Wafuasi binafsi na Vibaraka kwa kutumia michango hiyo ya siri ya Wafuasi, wapenzi na Wanachama wa CHADEMA ambayo haitozwi Kodi, haikaguliwi na CAG wala haijulikani kwa mtu yeyote ila yeye.

Na kwa ujumla wake nimepata na tumepata majiibu ya kwanini Mwenyekiti Freeman Mbowe pamoja na mateso na manyanyaso mengi toka kwa dola na Serikali lakini bado Mwenyekiti huyu anaifurahia nafasi yake hiyo kwa miaka zaidi ya 20.
Kesi ya uhujumu uchumi inamhusu
 
Huwezi kuandika process za kitaalamu kutoka kichwani kwako.

CDM na Tanzania kwa ujumla taasisi zote za vyama vya siasa na serikali; taratibu zao za ukaguzi wa accounting (ni internal auditing) na CAG.

Kama CAG miaka yote hakuona shida na mfumo wa CDM (maana yake ni legal) uwezi shinda kesi. System ya kulinda finance za CDM ni jukumu la accountants wao.

Taasisi chache sana Tanzania (tena za zenye guaranteed debts za serikali) ndio zimeajiri private auditors na firms zenyewe ni zilezile big four accounting firms za dunia.

Na ukisoma report zao hao auditing firm zipo kulinda contract zao, kushinda kukupa picha halisi if they can get away with it.

Juzi China wame fine PwC $62 million dollars na kuwafungia kazi miezi sita ndani ya China kwa kutofanya ukaguzi thabiti wa hesabu za Evergreen (kampuni ya ujenzi sawa na NHC Tanzania) kuwasaidia kuficha hesabu cooking of the books ili waonekane wapo vizuri ilihali walikuwa na miradi luluki ya hasara kushinda madeni yao.

Sisi wengine tunaweza soma hizo report za mashirika pamoja na upishi wao ukawaambia serikali hapa hamna kitu hiyo report imepikwa na kweli shirika likapata hasara, serikali ikachukua madeni, kuwapa ruzuku na CEO aliesababisha hiyo hasara akatunukiwa nafasi nyingine ya ushauri wa biashara serikalini.

The nonsense hawa ndio wenye external auditors. sasa sijui Lissu ana challenge vipi taratibu za CDM bila ya mapungufu yaliyoonyeshwa na CAG huku CDM aina external auditors wengine.

Ni mtu wa kukurupuka vita inataka kujipanga kwanza (tactics).
Umeelewa lakini nilichoandika?

Utaratibu anaoutumia Mwenyekiti Freeman Mbowe unaweza kukagulika na CAG?
 
Umeelewa lakini nilichoandika?

Utaratibu anaoutumia Mwenyekiti Freeman Mbowe unaweza kukagulika na CAG?
Ulichoandika ni mambo ya kutoka kichwani kwako tu, labda na kwa kumsikiliza Lissu (mkurupukaji).

Lakini Mbowe hawezi fanya upuuzi huo (ni mfanyabiashara) ambae anajua auditor anaweza omba details za bank statements ya taasisi ya biashara kufanya bank reconciliation ya vitabu.

Pili Mbowe anajua msingi wa separation ya owner and organisation legal entity ndio maana umeona keshaporwa biashara nyingi na majengo kwa kutolipa kodi za majengo na biashara; bila ya kumfilisi yeye mwenyewe.

Tatu uwezi sajili taasisi ya umma bila ya kuwa na account yake rasmi na ukawa na external auditor (hata kama ni wa hovyo kama CAG) hiko ndio anachokagua kwenye kilichoingia na kutoka. CAG akagui account ya Mbowe.

Hela ya ruzuku ya chama serikali haiwezi lipa kwenye account ya mtu, vinginevyo watakuwa wameshiriki kwenye fraud, lazima ilipwe kwenye account ya taasisi.

Ni upuuzi ulichoandika logically au ukumuelewa Lissu (binafsi sijamsikiliz bado sijapata muda) Iła kusema hela za chama zinaweza kwenda kwenye account ya Mbowe ni kutoelewa mambo.

Sasa aina maana Mbowe hana mbinu za kutumia hela zinazoingia kwenye account ya chama kwa ubadhirifu; hizo ni accusations mbili tofauti.

Kutumia account ya chama atakavyo na hela kuingia kwenye account yake sio kitu kimoja. The former is possible, the latter is impossible.
 
Yeye alisema huwa hagombei mwenyewe bali wanachama wanamlazimisha . Binafsi nadhani si kukamatwa tu bali akikamatwa afungwe pingu na kitambaa cheusi usoni
Hizo huwa kauli tu na mbinu za kung'ang'ania madarakani.

Hakuna mtu anayelazimishwa kwenye jambo la hiyari.
 
Kwanini tusianzie na CCM kwanza na Serikali kwa ujumla..., Ukizingatia hao ndio wanakula sana Kodi zetu na Ruzuku....; Anyway nilishasema....

 
Kwanini tusianzie na CCM kwanza na Serikali kwa ujumla..., Ukizingatia hao ndio wanakula sana Kodi zetu na Ruzuku....; Anyway nilishasema....

CCM wanakusanya pesa kwa nani?
 
CCM wanakusanya pesa kwa nani?
Hivi hujui Kodi zako zinatumika kama Ruzuku kwa Vyama kila Mwezi ? Na CCM kutokana na so called wawakilishi wengi (Wabunge) AKA Rubber Stampers wanapokea pesa lukuki kila mwezi..., In short haya maigizo yanaligharimu sana hili Taifa....

 
N a baado Hmajasema ! Mtasema tu !!
Bila Mwamba Mbowe saa hizi Lissu angekuwa shimo la Tewa !!
 
Hela ya ruzuku ya chama serikali haiwezi lipa kwenye account ya mtu, vinginevyo watakuwa wameshiriki kwenye fraud, lazima ilipwe kwenye account ya taasisi.
Mkuu hiki ndicho ninachofahamu, nashangaa hizi tuhuma kuwa zinawekwa katika akaunti binafsi 😯
 
Mkuu hiki ndicho ninachofahamu, nashangaa hizi tuhuma kuwa zinawekwa katika akaunti binafsi 😯
Ni uthibitisho wa Lissu ni mtu wa kukurupuka.

Hajui hata hesabu za taasisi ambayo amekuwa nwanachama wanavyokaguliwa na CAG.

Serikali haiwezi lipa ruzuku kwenye account ya Mbowe.
 
Kwa Namna mamlaka inatafuta mbinu za kuiangamiza Chadema, Mbowe angekuwa na hayo makando kando uliyoandika hapo msajili na ofisi nzima wangehamia ofisi za chadema.
 
Kuna mambo tunaweza kubishana pengine ili kulinda itikadi au falsafa zetu ila kamwe hatuwezi kubishana ili kulinda uhalifu na uovu mkubwa kwa kiwango hiki kwenye taasisi kubwa kama CHADEMA.

Nimemsikiliza Makamu Mwenyekiti Tundu Lissu anasema endapo atashinda na kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA ngazi ya Taifa basi atafutilia mbali utaratibu wa mtu mmoja kupita peke yake kwa wadau ili kukusanya fedha kwaajili ya kuendesha na kuendeshea shughuli mbalimbali za chama utaratibu ambao umedumu kwa kipindi Cha zaidi ya Miaka 20 sasa.

Kwa lugha nyepesi huenda ama ni kweli Freeman Mbowe ni mnufaika mkubwa wa fedha za CHADEMA kuliko hata CHADEMA yenyewe kwa miaka hii 20 aliyokaa madarakani,

Najaribu kuwaza ni kiasi gani Cha fedha Mwenyekiti Freeman Mbowe amejizolea toka kwa wapenzi, Wafuasi, wanachama na Viongozi wa CHADEMA wasiotaka kujulikana kwa majina ila tu kwa Mwenyekiti wa Chama Freeman Mbowe kwa kipindi chote hiki Cha miaka 20.

Najiuliza zaidi ni jambo gani lililomfanya Mwenyekiti Freeman Mbowe asitumie kabisa akaunti ya CHADEMA kwa sharti la wadau hao wa CHADEMA kutoandika majina yao rasmi ( watumie fictious names ) kwa lengo la kukuza usiri na kuepa mkono wa CCM na dola.

Mwanafalsafa mmoja wa Kigiriki aliwahi kusema " Yeyote unayemwona mbele yako jua kuwa mtu huyo ni mwizi kwa asili" baada ya falsafa hii ya kila binadamu ni mwizi kwa asili ndio maana utaona leo kila sehemu ya pesa lazima ihusishe watu zaidi ya wawili au wawili mfano hata Password ni mtu wa pili,

Kwa dhana hii ya kila mtu ni mwizi kwa asili, Je falsafa hii haitamuhusu Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa kipindi hiki chote cha zaidi ya miaka 20? Ninani anajua Mwenyekiti huyu kakusanya kiasi gani Cha fedha za wadau hata sasa? Je, hao wadau wataendelea kumwamini Mwenyekiti Freeman Mbowe hata baada ya Uchaguzi huu?

Nahitimisha hivi, kama kweli Mwenyekiti Freeman Mbowe amekuwa akifanya haya kwa miaka yote 20 ya uongozi wake basi Freeman Mbowe ndio Mtanzania pekee aliyejikusanyia pesa nyingi zaidi za Watanzania kwa mgongo wa kuzipeleka CHADEMA na huenda Sasa Uenyekiti wake ukawa wa faida zaidi hata ya Urais wa nchi na madhara yake huenda ikawa ni ngumu zaidi kumwondoa kwenye nafasi hii hasa baada ya kujitengezea Wafuasi binafsi na Vibaraka kwa kutumia michango hiyo ya siri ya Wafuasi, wapenzi na Wanachama wa CHADEMA ambayo haitozwi Kodi, haikaguliwi na CAG wala haijulikani kwa mtu yeyote ila yeye.

Na kwa ujumla wake nimepata na tumepata majiibu ya kwanini Mwenyekiti Freeman Mbowe pamoja na mateso na manyanyaso mengi toka kwa dola na Serikali lakini bado Mwenyekiti huyu anaifurahia nafasi yake hiyo kwa miaka zaidi ya 20.
Ni sahihi kabisa.Mbowe anapaswa kufurushwa na kukamatwa ashtakiwe.ameiba sana ruzuku na kuua wenzie
 
Back
Top Bottom