NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,587
- 13,425
Kipindi Tamasha la Simba Day linaendelea ilitokea sintofahamu baadhi ya mashabiki kutoruhusiwa kuingia uwanjani na tickets wanazo na hiyo ilitokea baada ya uwanja kujaa.
Benjamini Mkapa unachukua mashabiki elfu sitini (60,000) na taarifa zilitoka mapema tu kuwa tiketi zote zimeisha. Ina maana watu elfu sitini walinunua tickets.
Kwanini nasema kuwa Mwenyekiti kahusika kubariki zoezi la uuzaji tickets zaidi ya elfu sitini?
Kupitia kwenye jukwaa la kuhamasisha Wanasimba Buza, Mwenyekiti Mangungu alisema nanukuu "Hata kama uwanja utajaa tutafunga TV kubwa kwenye Uwanja wa Uhuru (Shamba la Bibi)," mwisho wa kunukuu.
Kutokana na hiyo baraka ya Mangungu watendaji wake waliendelea kuuza tickets japo kuwa tayari hitaji la uwanja limefikia tamati, na hiyo imefikia /imesababisha baadhi ya mashabiki kubaki nje ya uwanja na tickets zao.
Ombi langu: Mwenyekiti wa Simba SC Mangungu jitokeze mbele ya camera na uombe radhi mashabiki mliowatafuta kwa hali na mali mitaani kwani wamekosewa pakubwa sana, na kama hutofanya hivyo mashabiki waliodhalilika leo, kesho hutoweza kuwaona tena!
Benjamini Mkapa unachukua mashabiki elfu sitini (60,000) na taarifa zilitoka mapema tu kuwa tiketi zote zimeisha. Ina maana watu elfu sitini walinunua tickets.
Kwanini nasema kuwa Mwenyekiti kahusika kubariki zoezi la uuzaji tickets zaidi ya elfu sitini?
Kupitia kwenye jukwaa la kuhamasisha Wanasimba Buza, Mwenyekiti Mangungu alisema nanukuu "Hata kama uwanja utajaa tutafunga TV kubwa kwenye Uwanja wa Uhuru (Shamba la Bibi)," mwisho wa kunukuu.
Kutokana na hiyo baraka ya Mangungu watendaji wake waliendelea kuuza tickets japo kuwa tayari hitaji la uwanja limefikia tamati, na hiyo imefikia /imesababisha baadhi ya mashabiki kubaki nje ya uwanja na tickets zao.
Ombi langu: Mwenyekiti wa Simba SC Mangungu jitokeze mbele ya camera na uombe radhi mashabiki mliowatafuta kwa hali na mali mitaani kwani wamekosewa pakubwa sana, na kama hutofanya hivyo mashabiki waliodhalilika leo, kesho hutoweza kuwaona tena!